Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 40 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 353 2022-06-08

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuunga mkono wananchi wa Jimbo la Manonga kwa kuwasaidia kujenga madarasa mawili katika kila shule?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Seif Khamis Said Gulamali, Mbunge wa Jimbo la Manonga kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua changamoto ya mahitaji ya vyumba vya madarasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali kupitia Mradi wa SEQUIP imepeleka shilingi milioni 470 kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari Seif Gulamali. Pia katika mwaka 2021 kupitia mradi wa Mpango wa Maendeleo ya Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO-19 jimbo la manonga lilipokea jumla ya shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 92 kwa shule za sekondari na shilingi milioni 160 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba nane vya madarasa ya shule za msingi shikizi.

Katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga shilingi milioni 200 kwa ajili ya ukamilishaji wa vyumba 10 vya madarasa katika Halmashauri ya Wilaya Igaunga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa kadri zitakapopatikana.