Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 31 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 269 2022-05-26

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza:

Je, ni lini Serikali itajenga Shule za Sekondari katika Kata za Sasu, Nhwande, Makingi na Kanonge katika Jimbo la Ulyankulu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rehema Juma Migila, Mbunge wa Jimbo la Ulyankulu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha wa 2021/2022, Serikali imetuma fedha katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya za sekondari 15 kupitia mradi wa EP4R shilingi bilioni 15.0 na shule 232 kupitia mradi wa SEQUIP shilingi bilioni 109.57 katika kata ambazo hazina shule na maeneo ambayo yana wanafunzi wengi ukilinganisha na miundombinu ya shule zilizopo.

Mheshimiwa Spika, kati ya fedha zilizotumwa Jimbo la Ulyankulu limepokea fedha shilingi milioni 470 kwa ajili ya ujenzi wa shule moja ya sekondari ya kata. Lengo la Serikali ni kuhakikisha kata zote zinakuwa na Shule za Sekondari nchini zikiwemo Kata za Sasu, Nhwande, Makingi na Kanonge ambapo kupitia Mradi wa SEQUIP jumla ya shule za sekondari 1,000 zinatarajia kujengwa nchini ili kuwapunguzia umbali wa kutembea wanafunzi kufuata shule.