Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: Je, ni lini Serikali itajenga Shule za Sekondari katika Kata za Sasu, Nhwande, Makingi na Kanonge katika Jimbo la Ulyankulu?

Supplementary Question 1

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, pamoja na majibu ya Serikali nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; kata hizi ambazo nimezitaja kwenye swali langu la msingi ziko mbali sana na mojawapo ina mto katikati, kwa hiyo wanafunzi wanapata shida sana kwenda shuleni. Shule inayo-accommodate wanafunzi wa kata hizi ambazo hazina kabisa sekondari ni Shule ya Sekondari Mkindo. Sasa je kwa nini Serikali isione umuhimu wa kuifanya hii sekondari ya Mkindo kuwa ni sekondari ya bweni ili iweze kuwasaidia wanafunzi ambao wanatoka maeneo ya mbali waweze kufikia ndoto zao?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Serikali iliona umuhimu wa kujenga vituo vya afya kwa kupitia pesa za tozo lakini pia pesa za COVID-19. Je, kwa kata hizi zenye maeneo ambayo hayana sekondari, kwa nini isilete mpango mahsusi kama ilivyofanya kwenye Wizara ya Afya ili kuhakikisha na hizi kata ambazo hazina sekondari na zenyewe zinapata sekondari?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Rehema Juma Migilla, Mbunge wa Jimbo la Ulyankulu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge amehitaji kwamba katika Kata ya Mikindo tuifanye kuwa shule ya bweni, tulipokee wazo hili na tutakwenda kufanya tathmini tutafute fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule hii.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Serikali ina mpango mahususi na mpango wetu ni kujenga sekondari 1,000. Mwaka wa fedha huu ambao unaisha 2021/2022 tumeshapeleka fedha katika kata 232, karibu bilioni 109.57 na katika mwaka wa fedha ambao Wabunge wameshatupitishia bajeti kwa maana ya 2022/2023 tutajenga shule za sekondari 234, manake tutapeleka katika kata zote katika majimbo ambayo bado hawajapata. Mwakani vilevile na mwaka kesho kutwa tutafanya hivyo hivyo. Kwa hiyo ndani ya miaka ya Mama Samia tutamaliza shule zote 1,000 ambazo Mheshimiwa Rais ameahidi kupitia mradi wa SEQUIP. Kwa hiyo nimwondoe shaka kwenye hilo. (Makofi)

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: Je, ni lini Serikali itajenga Shule za Sekondari katika Kata za Sasu, Nhwande, Makingi na Kanonge katika Jimbo la Ulyankulu?

Supplementary Question 2

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Kata ya Nyamagoma ni miongoni mwa Kata za Wilaya ya Ngara ambazo hazina shule ya sekondari. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Nyamagona? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Ndaisaba George, Mbunge wa Jimbo la Ng’ara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Kata ya Nyamagona ipo katika mpango ambao tunakwenda kujenga katika mwaka wa fedha unaokuja. Kwa hiyo nimwondoe shaka kwamba itajengwa katika mwaka wa fedha unaokuja wa 2022/2023.