Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 31 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 271 2022-05-26

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua changamoto za Viwanda vya Nguo nchini kwani ni viwanda vitatu tu kati ya 33 vinafanya kazi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, sekta ndogo ya nguo na mavazi nchini ina jumla ya viwanda tisa vinavyofanya kazi hivi sasa. Serikali inaendelea kutatua changamoto zinazokabili viwanda vya nguo, ikiwa ni pamoja na kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara nchini, kudhibiti bidhaa zisizo na ubora na bidhaa bandia kutoka nje ya nchi, kuongeza ushuru wa forodha kwa kanga na vitenge vinavyotoka nje ya nchi, kuhamasisha Taasisi za Umma na Watanzania kwa ujumla kununua bidhaa za nguo zinazotengenezwa na viwanda vya hapa nchini na kuweka miundombinu wezeshi.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.