Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua changamoto za Viwanda vya Nguo nchini kwani ni viwanda vitatu tu kati ya 33 vinafanya kazi?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Swali la kwanza; kumekuwepo na uingizaji wa nguo hasa vitenge na kanga kwa njia za magendo kutoka nje ambavyo vinapelekea ukwepaji wa kodi na hivyo kupoteza mapato, lakini pia vinasababisha viwanda vyetu nchini kutokuwa shindani. Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba inatokomeza biashara hii ya magendo ili kuweza kusababisha viwanda vyetu viweze kuzalisha kwa tija? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; nchi yetu imekuwa na viwanda maarufu sana Afrika Mashariki na Kati, kama vile Kilitex, Urafiki, Mutex, Mwatex, lakini viwanda hivi vimeshindwa kufanya kazi kwa changamoto mbalimbali ikiwepo mitaji. Ningependa kujua Serikali ina mkakati gani angalau kuweza kutoa dhamana za mikopo kwa viwanda hivi ili viweze kujiendesha kwa tija pia? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli sekta ya nguo na mavazi nchini imekuwa na changamoto kubwa ikiwemo hiyo ya kuingiza bidhaa hizo kwa njia ya magendo. Tunajua na tulishaanza kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kudhibiti mipaka au zile sehemu ambazo wanaingiza kiholela katika maeneo ya bandari bubu, lakini pia na mipaka ya kutoka nchi za jirani. Pia kwa sasa kumekuwa na tabia ya kuingiza, kupitisha nguo hizo kwenda nchi za jirani halafu kurudisha nchini. Kwa hiyo tumeshaanza kuchukua hatua ikiwemo kudhibiti kwenye sehemu zote zinazoingiza bidhaa, lakini kuongeza watumishi kwenye Taasisi zetu ikiwemo TBS, FCC na wengine, kuhakikisha tunaongeza udhibiti katika mianya ambayo wanaingiza bidhaa hizo bandia hasa bidhaa za nguo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu viwanda ambavyo havifanyi kazi, ni kweli kuna viwanda ambavyo vimesimama ikiwemo kama alivyotaja ya Urafiki, lakini anajua Serikali tumekuwa na mkakati mara nyingi kuhakikisha tunavisaidia kwa kuweka dhamana na kuweza kuweka ruzuku mbalimbali ili viweze kufanya kazi. Ndiyo maana hivi viwanda tisa ambavyo vinaendelea kufanya kazi sasa, ni kutokana na juhudi hizi za Serikali mpaka vimefikia idadi hiyo kutoka vitatu mpaka tisa, nakushukuru.

Name

Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua changamoto za Viwanda vya Nguo nchini kwani ni viwanda vitatu tu kati ya 33 vinafanya kazi?

Supplementary Question 2

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mwaka 1998 Serikali ilitaifisha viwanda vikiwemo vya nguo na vingine. Mwaka 2017 viwanda hivi vilirejeshwa Serikalini katika Bajeti ya Viwanda na Biashara ya mwaka jana, Waziri alisimama hapa akasema viwanda hivi vitatangazwa kwa wawekezaji wenye uwezo ili waweze kuvifufua. Wananchi wetu na hasa vijana wanalalamika ajira, kwa nini Wizara iko kimya mpaka leo?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Lucy, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli viwanda ambavyo vilikuwa vimebinafsishwa na vikawa havifanyi kazi jumla viwanda kama 20 vilikuwa vimerejeshwa Serikalini. Kati ya hivyo 10 tutavitangaza, notice ilishatangazwa mwaka jana, lakini sasa tunaendelea na mchakato wa kupata wawekezaji.

Mheshimiwa Spika, vingine ambavyo tunadhani ni muhimu kama Serikali tuendelee kuviendeleza, vitakuwa chini ya Mashirika mbalimbali ya Serikali ikiwemo NDC, maeneo yale ya uwekezaji kwa ajili ya wananchi EPZA, na kadhalika. Kwa hiyo, Serikali inaendelea na mchakato wa kuona tunapata wawekezaji mahiri, hatutaki tena kwenda haraka tukapata wawekezaji ambao badala ya kuendeleza viwanda watavidhoofisha zaidi kama ambavyo ilitokea huko nyuma. Kwa hiyo tunaendelea na mchakato huo kuhakikisha tunavitangaza viwanda hivyo kwa wawekezaji wenye tija na wenye nia ya kuendeleza viwanda hivyo. (Makofi)

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua changamoto za Viwanda vya Nguo nchini kwani ni viwanda vitatu tu kati ya 33 vinafanya kazi?

Supplementary Question 3

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa asilimia 75 ya mafuta ya kupikia yanatoka nje ya nchi na kiwanda cha kuzalisha mafuta ya kupikia kilichopo katika Kata ya Wazo kinaitwa Family kimefungwa.

Je, Mheshimiwa Waziri ataambatana pamoja na mimi baada ya hapa ili kujua ni sababu gani kiwanda hicho kimefungwa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Mchungaji Josephat Gwajima, Mbunge wa Kawe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali sasa hivi mkakati wetu ni kuhakikisha tunajitolesheza kwenye mafuta ya kula. Kwa hiyo kama kweli kuna kiwanda ambacho kimefungwa na mimi kama Naibu Waziri kwenye sekta inayohusu viwanda, nitaambatana na Mheshimiwa Mbunge ili tuweze kuona changamoto gani zinakikabili hicho kiwanda ili kiweze kuendelea kuzalisha mafuta ya kula ili kupunguza changamoto hii ya mafuta ya kula nchini, nakushuru sana.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua changamoto za Viwanda vya Nguo nchini kwani ni viwanda vitatu tu kati ya 33 vinafanya kazi?

Supplementary Question 4

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Kwa kuwa Serikali inayo dhamira ya dhati ya kufufua Kiwanda cha Kilimanjaro Machine Tools na tayari wameshaanza kuleta mitambo mbalimbali. Swali langu, Serikali iliahidi kutupa bilioni 1.6 kwa ajili ya kujenga foundry machine yaani kinu cha kuyeyusha chuma. Je, ni lini Serikali itatuletea fedha hizo ili kiwanda kiweze kufanya kazi kwa asilimia mia moja?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Kilimanjaro Machine Tools ni moja ya viwanda ambavyo vilikuwa vinazalisha vipuri kwa ajili ya kulisha viwanda vingine ambavyo vinazalisha bidhaa mbalimbali ikiwemo viwanda vya nguo na kadhalika. Lengo la Serikali kama nilivyosema ni kufufua viwanda vyote na kuhakikisha vinapata vipuli. Sasa hivi Serikali imeshatoa milioni 700, kwa hiyo bado milioni 800 na kidogo ambazo zitaenda kukamilisha ujenzi wa foundry hiyo katika kiwanda cha KMTC. Kubwa zaidi commitment imeshatoka, Wizara ya Fedha itatoa fedha hiyo ili foundry hiyo iweze kujengwa. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba nia ya Serikali na lengo la Serikali ni kulitimiza kadri ambavyo tumepanga kwenye bajeti zetu, nakushukuru.