Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 32 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 278 2022-05-27

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG STELLA M. MANYANYA aliuliza:-

Je, ni kwa nini Serikali isitoe rasilimali za Kiwanda cha Mang’ula Mechanical and Machine Tools kilichopo Kilombero kwa Taasisi za Ufundi kama DIT na nyinginezo ili ziweze kutumia?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA, alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mhandisi Stella Martin Manyanya, Mbunge wa Jimbo la Nyasa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeamua kukihuisha upya kiwanda cha Mang’ula Mechanical & Machine Tools Co. Ltd. kupitia Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) ili kiendelee kutekeleza majukumu yaliyokusudiwa hapo awali. Ikiwa kutakuwa na haja ya kuzihusisha Taasisi za Ufundi Serikali itafanya hivyo.