Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG STELLA M. MANYANYA aliuliza:- Je, ni kwa nini Serikali isitoe rasilimali za Kiwanda cha Mang’ula Mechanical and Machine Tools kilichopo Kilombero kwa Taasisi za Ufundi kama DIT na nyinginezo ili ziweze kutumia?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri. Uzoefu unaonesha kwamba taasisi nyingi ambazo ziko chini ya NDC hazifanyi vizuri kutokana na ukosefu wa fedha kwa mfano General Tyre, Kilimanjaro Machine Tools na kadhalika.

Swali langu katika bajeti ya mwaka huu 2022/2023 Wizara imeanza kutenga fedha zozote kwa ajili ya kuendeleza kiwanda hicho cha Mang’ula Machine Tools?

Kwa kuwa kiwanda kile kimenyofolewa maeneo muhimu karibu yote kwa mfano sehemu za foundry imenyofolewa kiasi kwamba ni ngumu kukirudishia kama kilivyo na kitahitaji gharama kubwa sana. Kwa nini kwa sababu kuna majengo ambayo yanawezesha kukaa wanafunzi eneo hilo lisitumike kwa ajili ya kuendeleza taasisi za kiufundi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella Manyanya, Mbunge kama ifuatavyo:-

Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Stella Manyanya kwa kazi kubwa anayoifanya kufuatilia maendeleo ya sekta ya viwanda kwa sababu na yeye amekuwepo kwenye sekta hiyo kwa muda mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ni kweli Shirika letu la Maendeleo la Taifa (NDC) lina miradi mingi ambayo kidogo ina changamoto lakini tumeshaanza kuyafanyia kazi ikiwemo Kilimanjaro Machine Tools ambako tumepeleka fedha ya kutosha kwa ajili ya kuihuisha ili kutengeneza foundry ambayo inafanana fanana na ile iliyokuwepo kule Mang’ula.

Kwa hiyo tumeshaanza kutengea fedha, lakini kwenye hii mahsusi ya Mang’ula baada ya kuona uhitaji huu tunafanya utafiti wa kuona nini kitafanyika halafu baada ya hapo sasa ndiyo tutakuja na bajeti yenye uhalisia. Kwa hiyo, tuko kwenye hatua za awali za kufanya utafiti wa nini kitafanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusu mitambo iliyokuwepo ni kweli na ndiyo maana tunataka tukihuishe kwa maana tuone sasa nini kitafanyika kwa sababu mwekezaji aliyekuwa amepewa mara ya kwanza ni kweli aling’oa mitambo mingi ikiwemo ya foundry, ya forging na fabrication na kuuza. Kwa hiyo, kimsingi tutaanza kama upya lakini kwa sababu nia ya Serikali nia ya kuona tunahuisha viwanda hivi kwa hiyo Serikali imeweka mkazo na tutakifanyia kazi na kutenga bajeti ya kutosha ili tuhakikishe tunarudi kwenye uhalisia wake wa awali, nakushukuru.