Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara ya kilometa tatu kwa kuanzia katika Halmashauri ya Geita?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, namshukuru Waziri kwa majibu mazuri, lakini mwaka 2020 wakati wa kampeni Mheshimiwa Rais aliposimama pale katika Makao Makuu ya Halmashauri ya Geita aliahidi kilometa tatu na mwaka 2021/2022 TAMISEMI, ilitenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kilometa moja, lakini mpaka leo tunaenda mwaka wa Serikali kumalizika hatujawahi kuiona hiyo kilomita moja.

Je, kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri ni kwamba sasa mtatekeleza kilomita mbili na sio kilometa moja?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKAO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Joseph Kasheku Musukuma, kama ifuatavyo;

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kama fedha hizi zipo katika bajeti ambazo zimetengwa, nitalifuatilia na nimelipokea ili kuhakikisha kwamba linatekelezeka kama ambavyo limeainishwa katika bajeti, ahsante.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara ya kilometa tatu kwa kuanzia katika Halmashauri ya Geita?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa Serikali imekuwa na utaratibu wa kutenga fedha kutokana na tozo mbalimbali; ni lini sasa itaweka vipaumbele kwenye majimbo ambayo yana changamoto kubwa sana za barabara ikiwemo Jimbo la Nyamagana Jijini Mwanza?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKAO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa Nyamagana kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inazingatia vipaumbele kulingana na mahitaji ya kila jimbo ikiwemo Jimbo la Nyamagana.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara ya kilometa tatu kwa kuanzia katika Halmashauri ya Geita?

Supplementary Question 3

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kuniruhusu niulize swali la nyongeza.

Kituo cha Afya cha Upugi kiko kilometa nne kutoka barabara kubwa ya Tabora - Nzega. Mheshimiwa Rais alipopita pale wananchi walimuomba awawekee barabara ya lami kwa sababu wagonjwa wakizidiwa kutoka kituo cha afya kwenda mjini inakuwa taabu sana. Je, Serikali iko tayari kuanza kujenga barabara hiyo ya kilometa nne?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKAO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Almas Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iko tayari kwa ajili ya kutekeleza maeneo yote yenye utata wa barabara ikiwemo eneo ambalo amelianisha Mheshimiwa Mbunge, isipokuwa kwa sasa tunatafuta fedha ili tuzitenge katika bajeti ili tuanze utekelezaji. Ahsante.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara ya kilometa tatu kwa kuanzia katika Halmashauri ya Geita?

Supplementary Question 4

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kuniona kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Liwale ni mji unaokua kwa kasi sana na ni miaka 42 sasa umri wa mji ule, lakini una kilometa 1.8 tu za lami pale mjini. Je, Serikali iko tayari kutuongezea mtandao wa barabara ya lami kwenye mwaka huu wa bajeti?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKAO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Jimbo la Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuambie tu kwamba Serikali iko tayari na tumetenga fedha na ninaamini eneo la Liwale ni sehemu ambayo tumewaanishia katika bajeti ya mwaka huu 2022/2023.