Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuajiri watumishi wa kutosha katika kada za afya na elimu nchini?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Mbinga Mjini mahitaji ya walimu kwenye shule za sekondari ni idadi ya 370 lakini waliopo ni 279 kuna upungufu wa walimu 91 hasa kwenye masomo ya sayansi na hesabu. Shule za msingi mahitaji ni 1,026 waliopo ni 605 upungufu 421 na ikama ya wafanyakazi katika afya wanaohitajika ni 725 waliopo ni 294 upungufu ni 431. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na upungufu huu mkubwa na kwa sababu Serikali imeahidi kwamba inafanya ajira, nilitaka nijue, je, Naibu Waziri ananihakikishia kwamba katika mgao huo wa watumishi, jimbo langu litapata watumishi wa kutosha ili kuweza kuziba hilo pengo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika maelezo ya Serikali na mkakati uliopo ni kujenga vituo vingi vya afya nchini. Lakini Serikali haijaonesha kwamba kuna mkakati gani wa dharura wa kuajiri watumishi ili kuhakikisha kwamba tunaziba hili pengo la wafanyakazi? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jonas William Mbunda, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na upungufu wa watumishi wa sekta zote, sekta ya elimu na sekta ya afya naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeweka mikakati ya dhati na inatekelezwa ya kuajiri watumishi wa elimu na watumishi wa afya na ndiyo maana hivi sasa tunapoongea tunaajira ambazo zinaendelea kuchakatwa za maombi ya watumishi ambao watapelekwa kwenye vituo vyetu vya afya lakini pia kwenye elimu na tutaendelea kufanya hivyo. Ahsante.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuajiri watumishi wa kutosha katika kada za afya na elimu nchini?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Nkenge – Misenyi tunaishukuru Serikali kutujengea vituo vya afya vya Kanyigo, Kakunyu na Kabyaile. Je, ni lini Serikali itatupelekea watumishi wa afya katika vituo hivyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver Semuguruka Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Semuguruka amekuwa akifuatilia sana suala la watumishi katika vituo hivyo na nimhakikishie kwamba Serikali kama ilivyoanza kuajiri sasa tutahakikisha tunaendelea kuajiri, lakini pia kupeleka watumishi katika vituo hivyo. (Makofi)

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuajiri watumishi wa kutosha katika kada za afya na elimu nchini?

Supplementary Question 3

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, shida iliyopo Mbinga Mjini inalingana sawasawa na Mbinga Vijijini kwa wahudumu wa afya tulitakiwa kuwa nawatumishi 751 waliopo ni 210 tu tuna upungufu zaidi ya asilimia 80. Je, Serikali ipo tayari angalau kupunguza upungufu wa watumishi huu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kapinga, Mbunge wa Mbinga Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Kapinga nimhakikishie kwamba tunafahamu kuna upungufu wa watumishi wa afya lakini pia wa elimu katika Halmashauri ya Mbinga Vijijini na mkakati ni kwamba kufuatia tathimini yetu halmashauri zile zenye upungufu mkubwa zaidi kama Mbinga Vijijini tutaleta watumishi wa kutosha zaidi, ahsante. (Makofi)