Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Kituo cha Afya Makambako kitapata mashine ya X-ray na Ultra Sound?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Hospitali ya Makambako imeshapata X-ray na Ultrasound naomba kuuliza swali moja tu la nyongeza; Kituo cha Afya Ikizu kina muda mrefu sana tukiwa na maombi ya X-ray na mwaka jana walisema wangepata lakini hawajapata. Ni lini sasa Kituo cha Afya Ikizu kitapata X-ray?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere, Mbunge wa Jimbo la Bunda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vituo vyetu vya afya vingi havina mashine za X-ray, lakini bado tutaangalia vigezo ambavyo vitapelekea baadhi ya vituo kupata kipaumbele kuliko vituo vingine, kwa hiyo, naomba nichukue hiki Kituo cha Afya cha Ikizu ili tukafanye upembuzi na kuona uhitaji wa X-ray lakini baada ya hapo tutatafuta X-ray kwa ajili ya kituo hicho pia, ahsante.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Kituo cha Afya Makambako kitapata mashine ya X-ray na Ultra Sound?

Supplementary Question 2

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Kituo cha Afya cha Maramba kinachohudumia kata sita Serikali iliahidi kupeleka X-ray; ni lini Serikali itapeleka X-ray?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dunstan Kitandula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Maramba ni kweli kwamba kinahudumia kata nyingi na katika mpango ambao tumeuweka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kituo hiki pia ni miongoni mwa vituo ambavyo tumepanga kitapelekewa X-ray, ahsante.