Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA kwenye vijiji zaidi ya 40 Busanda?

Supplementary Question 1

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali kwamba tunae Mkandarasi CRJE ambaye anatakiwa kufanya kazi maeneo yetu. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali moja ni kwamba nini mpango wa Serikali kuwaunganishia umeme wananchi ambao wamekwishalipia umeme na wamekwishakuwa surveyed na wanasubiri umeme huu zaidi ya mwezi mmoja kuunganishiwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba taasisi zote kwenye vijiji ambavyo vimeshawekewa umeme zinaunganishiwa umeme ili wananchi na taasisi zile ziweze kutumika vizuri zaidi? Ahsante. (Makofi)

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tumaini Bryceson Magessa, Mbunge wa Busanda maswali ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza kwa ufuatiliaji mzuri wa maeneo ya vijiji katika jimbo lake ambayo hayajapatiwa umeme. Kuhusu suala la ambao wamekwishalipia na hawajaunganishiwa, Serikali imeanzisha programu maalum na kutafuta fedha na kutenga fungu la fedha maalum kwa ajili ya kununua vifaa ambavyo vilikuwa vinakosekana kwa ajili ya kuwaunganishia wateja wote takribani 100,000 ambao hawajaunganishiwa umeme na bahati nzuri kadri siku zinavyoenda tunapunguza hiyo back log. Kwa hiyo, kwa wananchi wa Busanda kazi inaendelea na watafungiwa umeme haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu taasisi kama unavyofahamu katika bajeti ya Wizara kwa mwaka ujao wa fedha tumetenga fedha mahususi kwa ajili ya kuunganisha umeme katika taasisi mbalimbali za umma ikiwemo shule na vituo vya afya.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA kwenye vijiji zaidi ya 40 Busanda?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Baadhi ya vijiji kwenye Jimbo la Ukerewe umeme umesogezwa mpaka kwenye transfoma lakini kwa zaidi ya mwaka mmoja umeme huu haujaweza kusambazwa kwenye makazi ya wananchi.

Nataka kujua mpango wa Serikali kuweza kusambaza umeme huu kwenye makazi ya watu. Nashukuru.

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Ukerewe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kulikuwa na changamoto hiyo ya kufikisha umeme katika maeneo ambayo watu wanaishi katika Jimbo la Ukerewe na napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba fedha zimepangwa, manunuzi yamefanyika ya vifaa vya kuweza kusogeza umeme katika makazi ya watu. Katika mwaka ujao wa fedha tutaongeza kasi ya kuwaunganishia umeme wananchi wa Jimbo la Ukerewe na kote nchini.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA kwenye vijiji zaidi ya 40 Busanda?

Supplementary Question 3

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Miezi nane sasa au saba, mkandarasi wa REA katika Jimbo la Mbulu Mji amesimika nguzo, hajaweka waya wala kuwasha umeme.

Je, ni lini mkandarasi huyo atafunga waya na kuwasha umeme katika Jimbo la Mbulu Mji? (Makofi)

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia, Mbunge wa Mbulu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kulitokea changamoto katika mradi unaoendelea wa REA wa kupanda kwa bei za vifaa ikiwemo transfoma na waya ambayo ilipelekea wakandarasi kuchelewa kukamilisha kazi walizokuwa wamepangiwa kufanya. Bahati nzuri Serikali imekaa na wakandarasi, tumepanga fedha za ziada kufidia gharama zilizoongezeka, tumeingia mikataba mipya na sasa kazi itaenda kwa kasi zaidi kukamilisha yale maeneo ambayo yalikuwa yamesimama.

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA kwenye vijiji zaidi ya 40 Busanda?

Supplementary Question 4

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, ahsante, nataka nijue nini kauli ya Serikali kuhusu wananchi kuuziwa nguzo za umeme, kwani mpaka hivi leo kuna wananchi wanataka kuingiza umeme kwenye majumba yao, wanauziwa nguzo?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rehema, Mbunge wa Ulyankulu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, sisi kama Serikali na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) hatukubali na haturuhusu watu kuuziwa nguzo katika umeme mkubwa. Pale ambapo ni sehemu ya gharama ya kuunganishiwa umeme inawekwa katika gharama hizo. Lakini pale ambapo Mheshimiwa Mbunge au mwananchi ana taarifa yoyote ya mwananchi kuuziwa nguzo ambapo ni wajibu wa TANESCO kuzipeleka, basi atuletee taarifa hiyo na tutashughulika na hilo tatizo haraka iwezekanavyo.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA kwenye vijiji zaidi ya 40 Busanda?

Supplementary Question 5

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona; kwa sababu Halmashauri yetu ya Mji wa Makambako ina maeneo ambayo ni vijiji na vitongoji. Je, Wizara haioni sasa ni muda wa kuwapelekea wananchi wa Makambako ambao wanalipa bei za kama mjini wakati mazingira ni vijijini yaliyo mengi? (Makofi)

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge wa Makambako kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, na Mheshimiwa Mbunge kama mtakumbuka wakati tunawasilisha bajeti ya Wizara ya Nishati kwa mwaka ujao wa fedha tulieleza kwamba tumepokea kilio cha wananchi wengi na Waheshimiwa Wabunge kwamba ni kweli yapo maeneo ambayo yapo katika maeneo ya mijini, lakini yana sifa ya maeneo ya vijijini.

Mheshimiwa Spika, tumeamua tuunde timu ya wataalam kutoka REA, TANESCO na Wizara ambapo itazunguka kwenye majimbo yote na kwa kushirikiana na Waheshimiwa Wabunge kukusanya taarifa za maeneo yenye sifa hizo. Baada ya hapo na kwa kweli hatutangoja miezi sita iishe, basi maeneo haya wananchi watalipia gharama za kuunganisha umeme kama wananchi wa vijijini. (Makofi)

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA kwenye vijiji zaidi ya 40 Busanda?

Supplementary Question 6

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Waziri kwenye Kata ya Lupila kuna sekondari na kuna kituo cha afya, umeme REA III Round Two haujaweza kufika kwenye eneo lile. Je, nini kauli ya Serikali kuweza kutuongezea scope ya kufika umeme kwenye eneo la taasisi hizi mbili?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Festo Sanga, Mbunge wa Makete kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni mpango wa Serikali kupeleka umeme na kuweka vipaumbele katika taasisi za umma. Lakini vilevile tunaongea na wenzetu ndani ya Serikali ikiwemo TAMISEMI kwamba pale ambapo kuna ujenzi wa hizi taasisi, basi kupeleka huduma ya umeme iwe sehemu ya gharama ya ujenzi wa hizo taasisi ili kurahisisha kazi ya upelekaji wa umeme.

Mheshimiwa Spika, lakini katika maeneo aliyozungumza Mheshimiwa Sanga ya Kata ya Lupila, naomba nikutane naye kwa mahususi ili tuweze kulifanya jambo hili kwa umahususi wake.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA kwenye vijiji zaidi ya 40 Busanda?

Supplementary Question 7

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kumuuliza Mheshimiwa Waziri kuwa je, ni kweli bei ya umeme imepanda kwa sababu naona kuna mabishano kwenye mitandao? (Makofi)

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stella Manyanya, Mbunge wa Nyasa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, si kweli kabisa kwamba bei ya umeme imepanda na Serikali inasikitishwa na wale wanaoeneza maneno hayo na uvumi huo kwenye mitandao. Tumeomba mamlaka husika zichukue hatua kwa udanganyifu na upotofu huo unaofanywa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mchakato wa kupandisha bei ya umeme ni mrefu, unahusisha maombi ya TANESCO kwa EWURA na unahusisha public hearing kwamba wananchi lazima wahusishwe na washirikishwe katika kutoa maoni yao pale bei ya umeme inapopandishwa. Ni mchakato mrefu ambao hauwezi kufanyika kwa siri. Kwa hiyo, hizi taarifa kwamba Serikali imepandisha bei ya umeme si kweli na naomba zipuuzwe na hatua zitachukuliwa kwa wale ambao wanaeneza uvumi huo. (Makofi)

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA kwenye vijiji zaidi ya 40 Busanda?

Supplementary Question 8

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii.

Katika Kata ya Msisima tuna sekondari ambayo inagharamiwa kwa shilingi milioni 600, lakini eneo hilo umeme haujafika. Je, Serikali itakuwa tayari kutupelekea umeme katika eneo la Kata ya Msisima kwenye Sekondari ya Msisima?

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Namtumbo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka ujao wa fedha tumepanga fedha mahususi kwa ajili ya kupeleka umeme katika taasisi za umma na bila shaka yoyote Shule ya Sekondari ya Msisima katika Kata ya Msisima na yenyewe itapata umeme katika programu hii.

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA kwenye vijiji zaidi ya 40 Busanda?

Supplementary Question 9

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, naomba kumuuliza swali Mheshimiwa Waziri; katika Jimbo la Shinyanga Mjini hususani Kata ya Kizumbi na Kitangia ambayo kimkakati ni maeneo ya viwanda, umeme haujafika katika maeneo mengi. Nini mkakati wa Serikali kupeleka umeme katika maeneo hayo? (Makofi)

Name

January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Salome Makamba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kwamba kuna baadhi ya maeneo siyo tu katika Jimbo la Shinyanga Mjini, lakini maeneo mbalimbali nchini ambapo kuna viwanda na ni maeneo ya uzalishaji na umeme haujafika. Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeanzisha programu maalum ya kupeleka umeme katika maeneo ya uzalishaji ikiwemo migodi, viwanda na kilimo kwa sababu pia ni maeneo ambayo yanaweza kuipatia mapato Shirika letu la Umeme Tanzania na maeneo haya katika Wilaya ya Shinyanga Mjini pia yatazingatiwa katika mpango huu mahususi.