Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuchapisha sheria za Tanzania katika nakala ngumu na nakala laini ili kurahisisha upatikanaji wa sheria hizo?

Supplementary Question 1

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina utaratibu wa kuchapisha sheria na marekebisho yake kwa kuziunganisha pamoja kama ilivyo kwa law reports. Sasa tangu mwaka 2002 mchakato huo ulifanyika tena 2019.

Swali langu, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha utaratibu huu unafanyika mara kwa mara ili kuepusha matumizi ya sheria zilizopitwa na wakati?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali langu la pili, sheria zinaporekebishwa huwekewa RE yaani Revised Edition. Mwaka 2019 siyo sheria zote ziliwekewa Revised Edition. Serikali ina mkakati gani wa kuwekea sheria zote Revised Edition ili kuweza kurahisisha matumizi kwa wananchi? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Judith kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ule mchakato swali lake la kwanza la nyongeza, nipende tu kumjulisha Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeendelea kujaribu kuziweka hizi sheria katika mfumo ambao ameusema, lakini sehemu kubwa sana ni mkwamo wa fedha kwa ajili ya process nzima ya kuzi-¬combine. Lakini haya marekebisho mengine ambayo ameyazungumza, tumechukua wazo lake na kimsingi tutaendelea kufanya michakato mbalimbali kwa ajili ya kuziunganisha. Ahsante.

Name

Bahati Keneth Ndingo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuchapisha sheria za Tanzania katika nakala ngumu na nakala laini ili kurahisisha upatikanaji wa sheria hizo?

Supplementary Question 2

MHE. BAHATI K. NDINGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Ni lini Serikali itakamilisha mchakato wa kufanya tafsiri kwenye sheria zetu kutoka lugha ya Kiingereza kwenda Kiswahili ili wananchi wetu waweze kupata uelewa wa sheria zao? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kumjibu Mheshimiwa Bahati kwamba sasa hivi Serikali imeendelea na mchakato. Wataalam wetu wako kambini wanaendelea kuzitafsiri hizi sheria ili ziweze kuja sasa kwa sura ya lugha ya Kiswahili. Lakini ni matarajio yetu kufikia mwaka 2023 tutakuwa tayari tumekamilisha kwa sababu kuna miainisho mbalimbali ambayo ni process za kutengeneza hizi sheria kuziamisha kwa lugha mbalimbali. Ahsante.