Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe?

Supplementary Question 1

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwanza naomba nishukuru kwa majibu mazuri ya Serikali.

Kwa kuwa mahitaji ya Chuo cha VETA ni ya muda mrefu sana katika Jimbo la Vwawa na katika Mkoa wa Songwe, ni lini zabuni za ujenzi wa chuo hicho zitatangazwa ili kuhakikisha kwamba kwa kweli chuo hicho kinakamilika katika mwaka huo wa fedha?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa vijana wengi wa Jimbo la Vwawa na Mkoa wa Songwe wamekuwa wanahitaji sana hiki chuo na inaweza ikachukua muda mrefu sana kukimalisha kukijenga.

Je, Serikali itakuwa tayari kutumia majengo mbadala kutoa mafunzo hayo kwa vijana ambao wanahitaji mafunzo hayo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Japhet Hasunga, Mbunge wa Vwawa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye ujenzi tunakuwa na taratibu au models tofauti tofauti sana za ujenzi. Tuna model hii ya sasa hivi ambayo Serikali tunaitumia ya force account, lakini tuna model ile ya zamani ya kutumia wakandarasi. Kwa hiyo kwamba ni lini Serikali itatangaza zabuni itategemea na model ambayo tutakayotumia na mara nyingi sana kwa ujenzi wa vyuo vyetu vya VETA huwa tunatumia force account. Kwa hiyo, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge mara tu Mwaka wa Fedha ujao utakapoanza mwezi Julai, taratibu za ujenzi zitaanza kwa sababu sasa hivi tunaandaa zile tittle kwa ajili ya kumilikisha lile eneo kwenye Wizara ya Elimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini eneo la pili amezungumza utayari wa kutumia majengo. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge baada ya Bunge hili tukufu tuweze kufanya ziara na timu yetu ya wataalam. Twende tukafanye tathmini ya hayo majengo anayoyazungumza ambayo tunaweza tukayatumia katika kipindi hiki kifupi wakati tunaendelea na ujenzi. Tutakapofanya tathmini hiyo na tukajiridhisha kwamba majengo hayo yanajitosheleza katika utoaji wa huduma hii, basi tunaweza tukafanya hivyo. Nakushukuru sana.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni miaka mitatu sasa toka wananchi wa Tarafa ya Chamriho wameahidiwa kujengewa VETA na wameshatoa eneo bure ekari 55. Ni lini sasa hiyo VETA ya Tarafa ya Chamriho itajengwa? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Getere, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi za wananchi za kutenga eneo hilo kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA. Lakini nimuondoe wasiwasi na niwaondoe wasiwasi Waheshimiwa Wabunge wote ambao maeneo yao bado Vyuo vya VETA vya Wilaya havijajengwa, katika mwaka wa fedha ujao dhamira ya Serikali kama ilivyo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi, lakini kama ilivyo kwenye Sera kwamba tunakwende kujenga Chuo cha VETA katika kila Wilaya ikiwemo na Wilaya hii ya Mheshimiwa Getere katika mwaka ujao wa fedha tunaamini kabisa tutaweza kuanza ujenzi katika eneo hili. Nakushukuru.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe?

Supplementary Question 3

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, katika Jimbo la Kilwa Kaskazini hakuna chuo chochote ambacho kimewahi kujengwa na Serikali. Je, ni lini Serikali itaweka mkakati wa kujenga Chuo cha VETA katika Jimbo la Kilwa Kaskazini?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyozungumza katika majibu yaliyopita ni Sera ya Serikali na ipo vilevile kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi, lakini ipo vilevile kwenye Dira ya Maendeleo ya Miaka Mitano na Dira ya Maendeleo ya Mwaka Mmoja kuhakikisha kwamba tunafikisha Chuo cha VETA katika kila Wilaya nchini ikiwemo na Wilaya ya hii ya Kilwa. Nimuondoe wasiwasi kaka yangu, ndugu yangu, katika eneo la Kilwa Kaskazini katika mwaka ujao wa fedha tunaamini chuo hiki katika eneo hili tunaweza kuanza ujenzi ili kuhakikisha vijana wetu katika eneo hili wanapata huduma hii ya elimu. Nakushukuru sana.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya swali la nyongeza. Nishukuru commitment ya Wizara kuja kujenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Kilwa ambayo ina Majimbo mawili ya Kaskazini na Kusini. Pale Kilwa Kusini tuna Chuo cha Maendeleo ya Wananchi ambacho ni chakavu, kuna baadhi ya miundombinu inahitaji maboresho. Nini kauli ya Serikali katika eneo hili?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, katika mwaka huu wa fedha unaoendelea kwenye vyuo hivi vya FDC Serikali ilitoa fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa zaidi ya bilioni 6.8. Lakini vilevile katika mwaka uliyopita wa fedha tumeweza kufanya ukarabati pamoja na ujenzi wa miundombinu.

Kwa hiyo, nikuondoe wasiwasi mchakato huu au taratibu hizi bado zinaendelea, tunaamini kabisa vifaa hivi vitafika Kilwa. Lakini tunaamini katika mwaka ujao wa fedha kwa vile programu ya kufanya ukarabati na ujenzi wa miundombinu mbalimbali katika vyuo vya FDC navyo vilevile tunaendelea kufanyia kazi tunaweza kufika eneo lile na kuweza kufanya kazi vizuri. Nakushukuru sana.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe?

Supplementary Question 5

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa nafasi. Wilaya ya Mbinga pamoja na ukongwe wake haina Chuo cha VETA. Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilaya ya Mbinga?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kapinga, kaka yangu, Mbunge wa Mbinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tukiri kweli Wilaya ya Mbinga ni Wilaya kongwe, lakini nikuondoe wasiwasi kaka yangu nazani ulishawahi kufika mpaka ofisini kwa ajili ya kufuatilia suala hili na Mheshimiwa Mbunge nadhani nilikueleza mpango wetu kama Serikali ni kuhakikisha kwamba Wilaya zile ambazo hazijafikiwa na ujenzi huu wa Vyuo vya VETA katika mwaka ujao tunahakikisha kwamba tunazipa kipaumbele hasa hasa zile Wilaya kongwe ambazo zina miundombinu hafifu lakini vilevile ni ngumu sana kufikika. Kwa hiyo, nikuondoe wasiwasi eneo hili la Mbinga tunakwenda kulifanyia kazi na tunahakikisha tunajenga chuo katika eneo hilo.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe?

Supplementary Question 6

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kuniruhusu na mimi niulize swali la nyongeza.

Ni lini Serikali itamalizia Kituo cha VETA kinachojengwa pale Iskizya, Uyui muda mrefu hakijakamilika?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Maige, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge katika fedha tulizozipata za UVIKO-19 zaidi ya bilioni 20 zilipelekwa kwenye maeneo ya vyuo vile 25 vilivyokuwa vinaendelea na ujenzi. Na ujenzi huo unaendelea, kama kutatokea mapungufu machache sisi kama Wizara tutakwenda kukamilisha eneo hilo la ujenzi. Kwa hiyo, nimuondoe wasiwasi ndani ya kipindi hiki kifupi kijacho tunakwenda kukamilisha ujenzi katika chuo kile cha Uyuwi. Nakushukuru sana.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe?

Supplementary Question 7

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwa kuwa Chuo cha VETA Nyasa ni chuo malkia kwa sababu Wilaya nzima haina chuo kingine zaidi ya kile na kile bado hakijaanza shughuli zake. Ni lini shughuli hizo zitaanza kwa sababu wananchi wanakiulizia sana?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Manyanya, Mbunge wa Nyasa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Manyanya kwa ufuatiliaji wa karibu, lakini nimuondoe wasiwasi katika kipindi cha mwaka huu wa fedha Serikali imetoa zaidi ya bilioni 8.8 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa kwenye vyuo vinne ambavyo vilikuwa vya Wilaya vilivyokuwa vimekamilika ambavyo ujenzi wake ulikamilika, lakini vifaa kulikuwa hakuna ikiwemo na chuo hichi cha Nyasa, Chuo cha Ruangwa, Chuo cha Kasulu pamoja na Chuo hiki cha Kongwa. Kwa hiyo, vifaa hivi tayari vimeshanunuliwa na tunaamini mara tu vifaa vitakapofika katika eneo hili la Nyasa ufundishaji au ufunguzi wa chuo hiki utaanza kwa kozi fupi lakini ifikapo Januari mwakani tutaanza kwa zile kozi ndefu. Nakushukuru sana.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe?

Supplementary Question 8

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, iko dhamira ya Serikali ya kujenga vyuo hivi vya VETA katika Halmashauri zetu.

Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Halmashauri ya Itigi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Massare, Mbunge wa Itigi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tufanye marekebisho, vyuo hivi havijengwi kwenye Halmashauri, vyuo hivi vinajengwa katika Wilaya. Kwa hiyo, zipo Wilaya ambazo zina Halmashauri zaidi ya moja, kwa hiyo, naomba nifanye marekebisho madogo kwenye eneo hilo kwamba hatujengi kwenye Halmashauri, lakini tunajenga katika Wilaya. Kwa hiyo, nimuonde wasiwasi Mheshimiwa Mbunge katika Wilaya ya Itigi napo vilevile tutafikia eneo hili kuhakikisha kwamba tunajenga chuo katika eneo hilo kwa sababu ni Wilaya muhimu kujengewa chuo.