Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati kwenye skimu ya kilimo cha mpunga iliyopo Kata ya Bahi, Wilayani Bahi kwani miundombinu yake imechakaa sana na kupelekea upotevu wa maji?

Supplementary Question 1

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali hususani kwanza kufanya upembuzi yakinifu na baadaye utekelezaji wa bajeti 2023/2024.

Swali langu nilitaka niulize Serikali Mkoa wa Dodoma umekuwa unapata mvua kidogo, lakini pamoja na mvua kidogo tumekuwa na maji mengi ambayo yanapotea; je, nini ni mkakati mahususi hasa katika kuongeza mabwawa haya ya skimu hizi za umwagiliaji kutoka kwa Serikali ukoje? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kenneth Ernest Nollo, Mbunge wa Bahi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge hii imekuwa ni hoja yake na ameisema sana hapa Bungeni na sisi Wizara ya Kilimo kwenye bajeti inayokuja tulizingatia hilo. Tuna ujenzi wa mabwawa makubwa mawili katika Wilaya ya Chamwino eneo la Membe na Msagali Mpwapwa, kama sehemu ya kuanzia katika kuhakikisha kwamba tunakuwa na-reserve kubwa ya maji ili tuweze kufanya kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati kwenye skimu ya kilimo cha mpunga iliyopo Kata ya Bahi, Wilayani Bahi kwani miundombinu yake imechakaa sana na kupelekea upotevu wa maji?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi, Skimu ya Umwagiliaji ya Kitua Nimwezayo Kongriti iliyoko katika Kata ya Lunguza imeshatengenezewa usambazaji wa maji kutoka kwenye banio hadi kwenye mashamba katika hatua ya awali.

Ni lini hatua ya pili ya kutoa maji kwenye mifereji kuyaingiza kwenye mashamba itaanza?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Shangazi, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ya kwanza tuliyoifanya ilikuwa ni kurudisha njia za asili za Mto Umba ambao kazi hiyo imekamilika. Hatua ya pili itakuwa ni kufanya tathmini ya gharama halisi za ukarabati wa mifereji ili tupeleke maji hayo shambani. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba hatua ya pili itafanyika ili maji hayo yaweze kufika shambani. (Makofi)

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati kwenye skimu ya kilimo cha mpunga iliyopo Kata ya Bahi, Wilayani Bahi kwani miundombinu yake imechakaa sana na kupelekea upotevu wa maji?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwanza nishukuru sana Mheshimiwa Rais kutupatia shilingi 711,000,000 kwa Skimu ya Magisa, lakini skimu ile sasa inakwenda kuharibika kwa sababu ya uchakavu na uliniahidi kwamba utakuja kufanya ukarabati.

Je, ni lini utatekeleza ahadi ya Serikali ya kufanya ukarabati kwenye Skimu ya Magisa? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli skimu hii inahitaji ukarabati hasa baada ya kuwa tulituma timu yetu ambayo imepitia miradi yote na katika bajeti inayokuja, tumepanga miradi ya ukarabati natumai pia mradi huu ambao Mheshimiwa Mbunge ameusema utakuwemo katika kazi hiyo. (Makofi)

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati kwenye skimu ya kilimo cha mpunga iliyopo Kata ya Bahi, Wilayani Bahi kwani miundombinu yake imechakaa sana na kupelekea upotevu wa maji?

Supplementary Question 4

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi na mimi niweze kumuuliza Mheshimiwa Waziri swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Skimu ya Umwagiliaji ya Chinangali ni kati ya skimu kubwa na kongwe katika Mkoa wa Dodoma na skimu hii Serikali tayari mlikuwa mmeshaanza suala zima la ukarabati ili wakulima wale waweze kupata maji kwa ajili ya kukidhi kilimo chao.

Je, ni lini sasa Serikali mtaanza rasmi na kukamilisha ukarabati wa skimu ile, ili wakulima wetu wa zabibu waweze kupata tija katika kilimo chao cha zabibu mkoani hapa? Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kunti Majala, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Skimu ya Chinangali ni kati ya skimu kubwa ambazo zinazalisha sana zao la zabibu na Serikali kupitia TARI na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji tuliamua kwa dhati kabisa kuifufua skimu hiyo na hivi sasa ninavyozungumza kazi inaendelea na tunategemea mwaka wa fedha ujao kwa maana ya tarehe 1 Julai kazi zitaendelea kukamilisha skimu hii kubwa ili mwisho wa siku wakulima wa zabibu wa Dodoma waweze kuzalisha kwa tija na kwa malengo ambayo tumejiwekea kukuza zao hili la zabibu Mkoani Dodoma. (Makofi)

Name

Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati kwenye skimu ya kilimo cha mpunga iliyopo Kata ya Bahi, Wilayani Bahi kwani miundombinu yake imechakaa sana na kupelekea upotevu wa maji?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii; kwenye Jimbo langu la Korogwe Mjini tuna skimu kubwa mbili za umwagiliaji Bonde la Mahenge Nagoo lakini pamoja na Bonde la kwa Mngumi. Mwaka huu Serikali ilituahidi itatupatia shilingi milioni 600 kwa ajili ya ukarabati wa Bonde la Mahenge pamoja na Nagoo, lakini mpaka muda huu ninavyoongea hatujapata hata shilingi moja kwa ajili ya ukarabati huo.

Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Korogwe Mjini? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Alfred Kimea, Mbunge wa Korogwe Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, sababu za kwa nini fedha hazijafika mpaka hivi sasa ni kwamba skimu hizo mbili alizozisema zinategemea sana Bonde la Bwawa Mkomazi. Kilichofanyika hivi sasa ni kwamba tumeamua tuanze na zoezi kubwa la upembuzi yakinifu na usanifu wa Bonde la Mkomazi kwanza ili baadaye tuweze kuzifikia hizo skimu mbili. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba tarehe za mwanzo kabisa za mwezi wa saba consultant atapatikana kwa ajili ya Bonde hilo la Mkomazi na baadaye kazi hiyo ikikamilika tutaendelea na hizo skimu mbili ambazo amezitaja kwa Mkumbo na ile nyingine. (Makofi)

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati kwenye skimu ya kilimo cha mpunga iliyopo Kata ya Bahi, Wilayani Bahi kwani miundombinu yake imechakaa sana na kupelekea upotevu wa maji?

Supplementary Question 6

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia fursa. Skimu ya Umwagiliaji ya Naming’ong’o iliyoko kwenye makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Momba, Chitete ndio skimu ambayo tunaitegemea sana katika kuhakikisha wakulima wetu wanaweza kulima kwa ufasaha.

Je, ni lini Serikali itafanya maboresho ya skimu hii ya Naming’ong’o ili iweze kuleta tija ukizingatia mwaka huu hakukuwa na mvua na wakulima wengi wamekausha sana mpunga?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Condester, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, moja kati ya kazi kubwa ambayo tumeipa Tume ya Taifa Umwagiliaji ni kuhakikisha inazipitia skimu zote nchini Tanzania ili kufahamu status yake, kujau ipi inahitaji marekebisho na ipi ifanyike nini iweze kuboreshwa. Nimwahidi Mheshimiwa Mbunge na skimu aliyoitamka tumeweka katika mipango yetu kwa ajili ya utekelezaji ndani ya Serikali.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati kwenye skimu ya kilimo cha mpunga iliyopo Kata ya Bahi, Wilayani Bahi kwani miundombinu yake imechakaa sana na kupelekea upotevu wa maji?

Supplementary Question 7

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa na mimi nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Skimu ya umwagiliaji ambayo inaendeshwa na umoja wa umwagiliaji katika Kata ya Magoeko katika Jimbo la Tabora Mjini ilitengewa fedha mwaka 2022/2023; fedha hizo sasa zimehamishiwa kwenda wilaya nyingine ya Uyui na Mheshimiwa Waziri nilishakukabidhi malalamiko hayo. Sijui Serikali inasemaje kuhusu wanakijiji hao ambao tayari wameshachanganyikiwa kwa sasa hivi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mheshimiwa Mbunge amewasilisha jambo hili mezani na kwa sababu amelileta wiki iliyopita tu Alhamisi, naomba anipe muda, tutakaa mimi na yeye pamoja na tume ili tutafute ufumbuzi wa kudumu na mwisho wa siku tuweze kuwahudumia wananchi wote wa Mkoa wa Tabora.