Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. KHAMIS MBAROUK AMOUR aliuliza: - Je, Serikali ina mikakati gani ya kuwasaidia wamachinga ili waondokane na umachinga na kuongeza mapato ya nchi?

Supplementary Question 1

MHE. KHAMIS MBAROUK AMOUR: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na nimshukuru Waziri kwa majibu yake mazuri, kimsingi nina swali moja tu la nyongeza.

Je, Serikali ipo tayari kuwatambua hawa wajasiriamali wamachinga, nakusudia wa Tanzania nzima, wawe wa Tanzania Bara na Visiwani, halafu wakawaandalia mazingira ya kukopesheka benki? Je, Serikali ipo tayari kufanya hivyo? Ahsante.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Khamis Mbarouk Amour, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tayari Serikali imeshaanza kutambua wamachinga Tanzania nzima ikiwemo Visiwani, lakini kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge kwa sababu anafuatilia sana suala hili, tutaongeza juhudi na kuweka mipango stahiki ya kuwatambua na kuwawezesha wamachinga wote ikiwemo upande wa Zanzibar ambao tunaamini wanatakiwa kupewa fursa sahihi ili waweze kuendelea kufanya biashara zao kwa ukamilifu na kwa ufanisi. Nakushukuru.

Name

Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. KHAMIS MBAROUK AMOUR aliuliza: - Je, Serikali ina mikakati gani ya kuwasaidia wamachinga ili waondokane na umachinga na kuongeza mapato ya nchi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kati ya changamoto kubwa zinazowapata wafanyabisahara wadogo hawa tunaowaita machinga ni uwezo wa kupata mikopo kwenye hizi financial institutions zetu, na sababu kubwa ni kutokidhi vigezo, hasa dhamana na wale wachache ambao wanapata mikopo haswa kwenye hizi micro-finance riba ni kubwa sana hivyo inasababisha wao kushindwa kuendeleza biashara zao.

Je, Wizara imejipanga namna gani ili kuweza kuwasaidia watu hawa kwenye sekta hii niliyoitaja? Ahsante. (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Alfred Kimea, Mbunge wa Korogwe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli, changamoto kubwa ambayo inawakumba wajasiriamali ikiwemo wamachinga ni changamoto ya kupata fedha au mitaji kwa ajili ya kufanya shughuli zao. Serikali inachukua jitihada mbalimbali ikiwemo kuweka fedha mahususi kwa ajili ya kuwasaidia wamachinga, kama ile asilimia 10 ya mikopo kupitia Halmashauri zetu, lakini pia zaidi kupitia taasisi zetu kama SIDO ambayo inahudumia viwanda vidogo na wafanyabiashara wadogo, tumeshaweka mahususi kwanza fedha, lakini pili tumekubaliana kupunguza ile riba ambayo mwanzoni ilikuwa ni kubwa kwa hiyo, itakuwa chini ya asilimia 10, lakini zaidi tunaendelea kuongea na taasisi za kifedha za binafsi na ninyi ni mashahidi, tarehe 11 Aprili Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, alifungua ile kampeni ya teleza kidijitali ambapo mfanyabiashara au mmachinga mdogo anaweza kupata fedha bila kuwa na dhamana au kwenda benki kupitia simu ya kiganjani, wanasema Mshiko Fasta kuanzia shilingi 50,000 mpaka 500,000.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hii ni jitihada kuhakikisha tunamkomboa mfanyabiashara mdogo au mmachinga kupata fedha kirahisi zaidi. Nakushukuru.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. KHAMIS MBAROUK AMOUR aliuliza: - Je, Serikali ina mikakati gani ya kuwasaidia wamachinga ili waondokane na umachinga na kuongeza mapato ya nchi?

Supplementary Question 3

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, pamoja na majibu mazuri ya mwisho ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nilitaka kumuuliza tu swali moja la nyongeza.

Kwa kuwa tunazungumzia sana asilimia kumi kama kuwafikia vijana, na tunatambua vijana wanaozungumzwa kwenye asilimia 10 zile asilimia nne zao ni vijana wanaoishia miaka 35 na machinga wengi wanazidi miaka 35.

Je, ni upi sasa mkakati wa Serikali katika kuwafikia machinga walio wengi zaidi ya hawa wa miaka 35? Ahsante.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Issa Mtemvu, Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli, asilimia 10 zile zimelenga zaidi akinamama, vijana na wale wenye ulemavu, lakini kwenye kundi hili la vijana ni kweli wakishavuka ule muda wao maana yake wanakuwa hawawezi kukopesheka.

Mheshimiwa Spika, lakini kama nilivyosema Serikali inaendelea na juhudi mbalimbali ikiwemo kupitia taasisi za kifedha ili kuhakikisha wamachinga hawa, hawa wajasiriamali ambao watakosa fursa kwenye ile asilimia 10 ambayo inatengwa katika Halmashauri, basi wapate fedha kupitia taasisi nyingine kama nilivyosema SIDO na taasisi za kifedha nyingine ambazo zinatoa mikopo kwa wajasiriamali. Nakushukuru sana.

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. KHAMIS MBAROUK AMOUR aliuliza: - Je, Serikali ina mikakati gani ya kuwasaidia wamachinga ili waondokane na umachinga na kuongeza mapato ya nchi?

Supplementary Question 4

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru na napenda kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, maeneo mengi kwenye Halmashauri wametenga maeneo kwa ajili ya wamachinga, namaanisha wamewajengea vibanda na vibanda hivi wanakwenda kuwapangisha. Hawa wamachinga mtaji wao ni kuanzia shilingi 20,000 mpaka shilingi 4,000,000; je, Halmashauri ziko tayari kuwapatia bure hivi vibanda kwa ajili ya kufanya biashara zao?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli katika mikakati ya kuhakikisha tunawezesha wajasiriamali na hasa wamachinga ni kuwatengea maeneo, lakini pia kuwawekea miundombinu wezeshi ikiwemo vibanda hivyo ambavyo vinasaidia kufanya biashara zao katika mazingira mazuri, lakini kama ulivyosema katika Halmashauri huenda wanakusanya fedha kidogo kwa ajili ya kuvikarabati au kuhakikisha vile vibanda vinakaa muda mrefu viweze kuwasaidia wajasiriamali au wamachinga hao. Kwa sababu ametoa wazo hilo nadhani tutaongea na wenzetu wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ili kuona namna gani ya kuwasaidia vizuri zaidi wajasiriamali au wamachinga ambao hawana uwezo wa kulipia vibanda hivyo kutokana na hali halisi na maeneo husika. Nakushukuru sana.