Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kuongeza mnyororo wa thamani wa zao la Kahawa ikiwa ni miongoni mwa mikakati ya kukuza soko la Kahawa?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa kahawa yenyewe ni bidhaa ambayo ni malighafi, swali langu ni kwamba: Ni upi mkakati wa Serikali kuvutia sekta binafsi katika kuongeza thamani kwa maana ya kuzalisha bidhaa ambazo zitachukua kahawa kama malighafi kwa mfano perfume, dawa na bidhaa nyinginezo ndani ya nchi yetu? Ni upi mkakati wa Serikali kuvutia uwekezaji wa aina hiyo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa swali la msingi ambalo lina tija katika kuongeza thamani katika zao la kahawa. Miongoni mwa mikakati yetu ambayo tulikuwa tumeiweka ni pamoja na kuvutia wawekezaji wengi kuja nchini.
Mheshimiwa Spika, moja ya sababu ambayo tumeiweka hapo, mwekezaji yeyote atakayekuja nchini kuwekeza kwenye viwanda vyetu hususani vya kahawa, maana yake tumepunguza baadhi ya kodi ambazo zilikuwa ni kodi kero kwa wawekezaji ikiwemo kuzuia baadhi ya bidhaa ambazo zinatoka nje, zinazoweza kuua soko la ndani, pamoja na kuwapa vivutio vya muda wa kufanya kazi hizo pamoja na mazingira ya kibiashara kuyaongeza katika soko letu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimwondoe shaka Mheshimiwa Mbunge kwamba moja ya mkakati wa Serikali yetu ni kuvutia wawekezaji na kila mwekezaji atafanya biashara zake hapa katika hali ya usalama zaidi, ahsante sana. (Makofi)