Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya marekebisho ya Kanuni za Uvuvi za mwaka 2020 ambazo zinalalamikiwa na wadau wa Sekta ya Uvuvi?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Niipongeze na niishukuru Wizara ya Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi kwa hatua ambayo imefikia, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; wakati Wizara inaendelea kurekebisha Kanuni hizi au inakwenda kufanya marekebisho ya Kanuni hizi, ilituma timu ya wataalam kwa ajili ya kufanya utafiti katika maeneo ambamo shughuli za uvuvi zinafanywa na wataalam hawa waliwasilisha ripoti ambayo nadhani Wizara ndiyo inafanyia kazi ikiwa ni kama msingi wa kutengeneza kanuni hizi. Swali la kwanza; je, maoni ya wataalam yatazingatiwa katika marekebisho ya kanuni hizi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Wizara imeshirikisha wadau mbalimbali katika kufanya marekebisho ya kanuni hizi ikiwa ni pamoja na Kamati ya Bunge inayohusiana na Sekta ya Mifugo. Je, Wizara ipo tayari wakati inaendelea kufanya marekebisho kanuni hizi kuwashirikisha pia Wabunge wanaotoka kanda za uvuvi ili kuongeza maoni? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Ally Mohamed Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, maoni ya wataalam yatazingatiwa nataka nimhakikishie yeye na Bunge lako Tukufu na Watanzania kwa ujumla, wataalam maoni yao tutayazingatia.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, je, Wabunge ambao walishiriki katika kuibua hoja hii wale wanaotoka katika maeneo ya uvuvi watashirikishwa? Hili pia tutahakikisha tunawashirikisha ili kusudi kuweza kutoka na Kanuni za pamoja. Ahsante.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya marekebisho ya Kanuni za Uvuvi za mwaka 2020 ambazo zinalalamikiwa na wadau wa Sekta ya Uvuvi?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Miongoni mwa kanuni ambazo zinalalamikiwa na wadau wa uvuvi ni pamoja na utitiri wa tozo unaotaka mmiliki alipe Dola 55, lakini chombo alipie Dola 55 na mvuvi alipe Dola 10. Ni lini watafanya marekebisho ya kanuni hiyo ambayo inakwenda kuwatesa hao wavuvi ambao ni Watanzania wanalipa kwa dola? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, lini tutarekebisha kanuni inayoonesha kwamba mmiliki wa chombo analipa leseni, mvuvi analipa leseni na chombo kinalipiwa leseni. Ni kweli kwamba, tunao utaratibu wa chombo cha chini ya mita 11 kinalipiwa leseni katika Halmashauri zetu za Wilaya kama ni sehemu ya mapato ya ndani. Kwa upande wa mmliki wa chombo na yeye analipishwa leseni na yule mvuvi analipishwa leseni ili tuweze kupata namba kwa maana ya takwimu ya wavuvi wangapi wanaoshiriki katika shughuli za uvuvi kila siku kwa kuwa na ile leseni. Hata hivyo, kwa maoni tuliyoyapokea kutoka kwa Wabunge tupo katika mchakato wa kuitafakari kanuni hii ili tuweze kuona namna iliyo bora ya kile cha kupata takwimu lakini vilevile ya kuweza kurahisisha shughuli zetu. Ahsante.

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya marekebisho ya Kanuni za Uvuvi za mwaka 2020 ambazo zinalalamikiwa na wadau wa Sekta ya Uvuvi?

Supplementary Question 3

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Miongoni mwa kanuni ambazo zinalalamikwa na wavuvi ni ile kanuni ambayo inamlazimisha mvuvi kutokuvua chini ya mita 50 kwenda chini.

Je, wakati Serikali inaendelea na mikakati ya kurekebisha kanuni haioni haja ya kupeleka mitungi ya oxygen kwa wavuvi wadogo wadogo ili kuweza kuwaokoa na athari ya kuzama maji?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Njau, kumradhi Mheshimiwa Felista Njau, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli wavuvi wapo wanaofanya shughuli za uzamiaji kwa ajili ya kuweza kupata rasilimali na hii ni katika zile kanuni tunazokwenda kuzifanyia kazi ya maboresho; na baadhi yao wanataka watumie zaidi ya mitungi 10, sisi tunadhani tunao uwezo wa kuruhusu lakini kwa uchache kwa sababu tunaamini matumizi ya mitungi mingi ni kinyume cha uhalisia wa kwenda kile anachokikusudia isipokuwa tu kama ana lengo lingine ambalo kinyume na uvuvi. Kwa hivyo, naomba Waheshimiwa Wabunge, wawe na subira ni katika kama jibu la msingi la mwanzo kwamba ni sehemu ya majibu tukakayoyatoa kwenye marekebisho ya Kanuni zetu. Ahsante.