Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya Uvinza?

Supplementary Question 1

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naipongeza Serikali kwa majibu mazuri, lakini ninalo swali moja la nyongeza. Ni lini Serikali itapeleka Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Kalya na ni lini itapeleka Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo pale Buhingu? Ahsante. (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nashon, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tutawaepeleka hawa watendaji ambako kuna upungufu katika maeneo yao kwenye kipindi cha bajeti hii ambayo kimsingi ndiyo tunayoijadili sasa. Kwa sababu tuna eneo ambalo tutapata watumishi wapya ambap tutazingatia maeneo ambayo hayana watumishi. Ahsante. (Makofi)

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya Uvinza?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mwaka 2021 niliomba Mahakama kwenye Tarafa ya Ikuwo, Tarafa ambayo wananchi wake wanatembea zaidi ya kilomita 120 kwenda kufuata huduma Mahakama ya Mwanzo. Niliahidiwa kwamba nitapewa Mahakama, lakini tunaenda mwisho wa mwaka, hadi leo hatujajengewa Mahakama. Ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Mwanzo kwenye Tarafa ya Ikuwo ili iweze kuhudumia Kata ya Kigala na Mfumbi ili wananchi wao wasipoteze haki zao za Kimahakama ambazo wamekuwa wakizikosa kwa muda mrefu? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kumjibu Mheshimiwa Sanga swali lake la nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba ujenzi haujaanza na kama nilivyojibu jana swali la msingi, niliwaeleza juu ya mkakati wa mwaka mpya huu wa fedha ambao tunakwenda kuanza ujenzi wa sehemu kubwa sana wa zile Mahakama za Tarafa. Namwomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira kidogo katika kipindi hiki kinachofuata ambapo bajeti yake imeshaidhinishwa, tunaenda kuanzisha ujenzi ambao utakwenda kutibu kiu ya wananchi wetu hawa. Ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya Uvinza?

Supplementary Question 3

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa sisi Mahakama ilijenga Mahakama ya Wilaya na imekamilika na Naibu Waziri wewe ndio ulikuja kuhimiza ukamilishwaji wa ujenzi huo: Je, utakuwa tayari kushawishi Mahakama waje sasa kuifungua kwa mbwembwe zote? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge atararijie kwamba tunakwenda kuizindua, mbwembwe aziandae huko huko kwa wananchi wake wakati wa kufungua hii Mahakama, kwa sababu ni huduma ambayo kimsingi ni ya muhimu katika maeneo yale. Kwa hiyo, naomba watu wa Mahakama waweze kuweka utaratibu wa kwenda huko na ikiwapendeza zaidi wamwalike Mheshimiwa Waziri akaungane nao katika uzinduzi huo. Ahsante. (Makofi)

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya Uvinza?

Supplementary Question 4

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Mahakama ya Wilaya ya Meru ina majengo chakavu sana na hivyo kuzorotesha huduma za Kimahakama: Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati wa majengo haya? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zaytun, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyokuwa nikijibu jana maswali yale ambayo yalihusisha masuala ya ukarabati, naomba niwaahidi Waheshimiwa Wabunge wote, majengo yote ya Mahakama ambayo yamechakaa, yametengewa fungu maalum na kwa kipindi hiki ambacho tunakwenda kuanza kuitumia bajeti ambayo mmeiidhinisha nyie wenyewe, kimsingi tunaenda kuanza ukarabati kwenye maeneo yote yale ambayo mpango kazi wake umeshakamilika. Ahsante.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya Uvinza?

Supplementary Question 5

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Wilaya ya Kishapu haina Mahakama yenye hadhi na kwa bahati nzuri jitihada zimefanyika za kupata eneo kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama hiyo: Je, Serikali inaahidi nini kumaliza tatizo hili la Mahakama yenye hadhi katika Wilaya ya Kishapu?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumjibu Mheshimiwa Butondo swali lake la lini Mahakama itakwenda kujengwa kwenye eneo lake?

Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi tumeshaweka programu ya Mahakama zote za Wilaya ambazo katika mazingira ya kawaida mpaka kufikia 2025 tutakuwa tumekamilisha nchi nzima ujenzi wa Mahakama zetu. Sasa ni lini? Ninaomba tu Mheshimiwa baada ya majibu haya, kwa sababu programu hii ninayo, tuweze kumpitisha kwenye eneo lini tunakwenda kuanza ujenzi? Ahsante. (Makofi)

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya Uvinza?

Supplementary Question 6

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa kwenye Mkoa wa Dar es Salaam eneo lililobakia kuwa na Mahakama ya Wilaya ni Jimbo la Kibamba ndani ya Wilaya ya Ubungo na eneo tayari tunalo: Je, Serikali mko tayari kujenga Mahakama pale ya Wilaya katika mwaka huu 2022/2023?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kumjibu Mheshimiwa Mtemvu, Mbunge wa Kibamba, swali lake kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tayari mpango wa kuanza ujenzi katika eneo alilolitaja umeshakamilika. Nami naomba baada ya hapa tuweze kuwasiliana ili tuone ni lini tunaanza mpango huu? Ahsante. (Makofi)