Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ali Juma Mohamed

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. ALI JUMA MOHAMED aliuliza: - Je, kuna nchi ngapi zimefungua Ofisi Ndogo za Ubalozi Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. ALI JUMA MOHAMMED: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina masuala mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2025 iliielekeza Serikali kuhakikisha inaongeza Ofisi ndogo za ubalozi kule Zanzibar lakini pia mashirika pamoja na taasisi za kimataifa.

Mheshimiwa Spika, suala la mwanzo nililokuwa nataka kujua. Je, kuna ofisi ngapi na mashirika mangapi ya kimataifa ambayo yamefunguliwa kule Zanzibar?

Mheshimiwa Spika, suala la pili, nilikuwa nataka kufahamu ni sababu zipi ambazo zimesababisha kufungwa kwa Ofisi ndogo ya Ubalozi wa Egypt kule Zanzibar? Ukizingatia, Egypt ni nchi ya mwanzo baada ya mapinduzi ya mwaka 1964 kutambua Mapinduzi ya Zanzibar. Pia, kipindi chote imekuwa ikiisaidia sana Zanzibar katika sekta ya elimu na kilimo. Je, ni sababu zipi zimesababisha Ofisi hii kufungwa ambayo iko takribani miaka 40 sasa?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE (MHE. BALOZI MBAROUK NASSOR MBAROUK): Mheshimiwa Spika, mbali na Konseli kuu ambazo ziko Zanzibar lakini pia kuna ofisi za mashirika ya kimataifa hususani ya UN kama vile UNDP, UNESCO, UN AIDS, UN WOMEN, FAO, ILO na nyinginezo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu nchi ya Misri kufunga ubalozi wake mdogo Zanzibar. Katika ulimwengu wa kidplomasia, kufungua na kufunga ubalozi ni suala la kawaida. Mara nyingi sababu zinazopelekea nchi kufunga ubalozi au ubalozi mdogo inakuwa kwanza ni kutetereka au kuharibika kwa mahusiano baina ya nchi na nchi. Pia, kubadilika kwa muelekeo wa nchi kistratejia na kimaslahi, pia kuna suala la usalama na mwisho kuna suala la uchumi katika kubana matumizi.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Misri hawakueleza bayana sababu zilizosababisha kufunga ubalozi wao mdogo Zanzibar mwaka 2012. Vilevile naomba kulieleza Bunge lako Tukufu kwamba, mbali na Nchi ya Misri kufunga ubalozi wake hapo Zanzibar lakini uhusiano kati ya Misri na Zanzibar umeendelea kuimarika siku hadi siku. Pia, wanashirikiana katika katika masuala mbalimbali ya kimkakati kama vile kilimo na elimu. Ahsante sana.