Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Skimu ya Umwagiliaji Kata ya Kihungu, Mbinga?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza, naomba niishukuru Serikali kwa kuweka mpango wa kufanya usanifu pamoja na kujenga miundombinu katika skimu ya umwagiliaji kwenye eneo la Kata ya Kihungu kwa Mwaka 2024/2025. Nina swali moja la nyongeza. Katika Kata ya Mpepai eneo la Mtuwa na Ruvuma Chini nayo ni maeneo ambayo yanafaa kwa ajili ya kujenga za umwagiliaji;

Je, Serikali inampango gani wa kuhakikisha kwamba maeneo hayo yanajengewa skimu za umwagiliaji?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Moja, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha kwamba kilimo tunachokipeleka sasa ni kile ambacho kitakuwa kinategemea maji badala ya mvua. Yaani tunataka Mtanzania alime katika misimu yote, yaani kwa maana kipindi cha kiangazi awe na shughuli ya kufanya ya kilimo lakini na kipindi cha msimu wa mvua afanye hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo haya maeneo ambayo ameyaainisha Mheshimiwa Mbunge ni maeneo yote ambayo Tume ya Taifa ya Umwagiliaji inayapitia ili kuhakikisha kwamba yote tunayatafutia fedha na yanaingia katika mpango ili yaweze kutekelezeka, ahsante sana.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Skimu ya Umwagiliaji Kata ya Kihungu, Mbinga?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kule katika Jimbo la Mlalo Tarafa ya Umba kwa maana ya Kata ya Mng’aro, Lunguza, Mnazi lakini na Kijiji cha Kivingo tumeshatenga maeneo kwa ajili ya skimu hizi za umwagiliaji;

Je, lini miradi hii itaanza?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana naomba nimjibu Mheshimiwa Rashid Shangazi Mbunge wa Jimbo la Mlalo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua kwamba haya maeneo yote ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja ya Mng’aro, Lunguza, Mnazi na Kivingo wameshayaandaa kwa ajili ya shughuli hiyo. Tume ya Taifa ya Umwagiliaji inayafanyia kazi; na tukishamaliza kazi hiyo basi miradi hiyo itatekelezeka. Kikubwa ambacho niwaondoe shaka Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Rais ameweka commitment kubwa kwenye miradi yote ya umwagiliaji na fedha ipo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hii. Kwa hiyo, tutafikia takriban miradi yote nchini, ahsante sana.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Skimu ya Umwagiliaji Kata ya Kihungu, Mbinga?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji kwenye Kata za Minepa, Mazimba na Lupiro Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kama nilivyojibu swali la msingi, lakini vilevile swali la nyongeza la Mheshimiwa Rashid Shangazi, nimjibu tu Mheshimiwa Christine Ishengoma kwamba maeneo yote haya ambayo yanafaa kwa ajili ya umwagiliaji tumeiagiza Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kuyapitia yote nchini kuyaweka katika mpango makakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mpaka sasa hivi tumeshafikia takriban asilimia 70 ya maeneo yote ambayo yanafaa kwa kilimo. Kwa hiyo, hata haya nayo mengine yamefikiwa mengine tunaendelea na utekelezaji wake. Kwa hiyo nimuondoe shaka kazi hiyo inafanyika. Ahsante sana.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Skimu ya Umwagiliaji Kata ya Kihungu, Mbinga?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Skimu za mifereji ni skimu ambazo zilikuwepo na kule kwetu Vunjo zimekuwa zinaweza zikaleta matokeo chanya kwenye kuongeza tija kwenye kilimo. Kwa kuwa Tume ya Umwagiliaji imeshafika kutafiti na kuziangalia skimu hizi, je, Waziri anaweza akanihakikishia kwamba wataenda haraka na kuanza kukarabati mifereji ile?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Vunjo Dkt. Charles Kimei kwamba hiyo kazi tutaifanya kwa haraka iwezekanavyo kwa sababu tumepewa rasilimali zote kutekeleza jambo hili; kwa hiyo, liko ndani ya uwezo wetu. Ahsante sana.

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Skimu ya Umwagiliaji Kata ya Kihungu, Mbinga?

Supplementary Question 5

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Serikali kupitia Tume ya Umwagiliaji ya Taifa ilifika Ngara ikaanza kujenga Skimu ya Umwagiliaji ya Vigondo ila ikaitelekeza kwa miaka saba iliyopita. Naomba commitment ya Serikali;

Je, ni lini Serikali itafika Vigondo, Rulenge na Ngara kuja kukamilisha mradi wa Skimu ya umwagiliaji ya Vigondo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana nimjibu Mheshimiwa Ndaisaba Mbunge wa Jimbo la Ngara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati nzuri jambo lake tumelizungumza jana na tumeshalifikisha kwa Mkurugenzi wa Tume; kwamba miradi yote ya nyuma ambayo ilikuwa imesimama tunaipa kipaumbele itekelezeke na ikamilike kwa wakati, na miradi mipya ambayo tunataka isaidie wakulima wote nchini nayo itakamilika. Ndiyo maana nimesema kwamba bahati nzuri Mheshimiwa Rais kama ni fedha ametupa kwa ajili ya kutekeleza miradi hii na sisi tutaitekeleza kama maelekezo ya Mheshimiwa Rais na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, ahsante sana.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Skimu ya Umwagiliaji Kata ya Kihungu, Mbinga?

Supplementary Question 6

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi ya swali la nyongeza. Ni muda mrefu sasa tangu serikali itoe ahadi ya kupeleka wataalam ili wakafanye upembuzi na usanifu kwa ajili ya Skimu ya Umwagiliaji ya Makangaga Kata ya Kiranjeranje katika Jimbo la Kilwa Kusini kazi hiyo bado haijafanyika mpaka sasa; je, ni lini sasa Serikali itatekeleza ahadi yake ya kwenda kufanya usanifu huo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante Mradi wa Makangaga uko katika Mwaka wa Fedha 2023/2024 kwa ajili ya kufanyiwa usanifu, kwa hiyo unatekelezeka katika mwaka huu wa fedha. Ahsante.