Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Mnara wa TBC – Kiteto?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru, na nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri mafupi yenye time frame, kwa kweli wananchi wa Kiteto wamesikia na tangu uhuru hawakuwahi kusikia Redio Tanzania. Lakini pamoja na hayo nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kiteto ni kubwa sana, nataka kujua; Je, mnara huu wa Redio mnaojenga uta-cover eneo kubwa kiasi gani? Swali la pili; mwaka wa fedha 2023/2024 kuna vijiji takriba 20 na zaidi mlikuwa mmepanga kwamba mtajenga minara ya simu kwenye Kata za Dosidosi, Laiseri, Loolera, Magungu, Namelock, Ndirgishi, Njoro, Olboloti, Partimbo na Songambele. Nataka mniambie lini hasa miradi hii itaanza ili wananchi wa kiteto wapate mitandao ya simu.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Olelekaita kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa mtambo huu utakapokamilika utaweza kuhakikisha kwamba huduma hii inapatikana katika Wilaya nzima ya Kiteto na kwa bahati nzuri Mheshimiwa Mwenyekiti tunamtambo mwingine upo pale Kilindi, ule mtambo utaweza kusaidiana vizuri kabisa na mtambo ambao tutaukamilisha pale Kiteto, na Wilaya nzima ya Kiteto haitokuwa na changamoto yoyote ya mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ametaja Kata za Dosidosi, Laiseri, Lengatei nafikiri majina kama hayo lakini katika kata zote 12 kata moja ndiyo inaenda kuhudumiwa na Halotel, kata saba zinaenda kuhudumiwa na Airtel, kata tatu zinaenda kuhudumiwa na Tigo na kata moja ambayo ni ya Songambele inaenda kuhudumiwa na Vodacom.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mradi huu uko katika hatua nzuri kabisa kwa sababu nafikiri mmeshaanza kuona wanapita huko kwa ajili ya kutafuta maeneo kwa ajili ya kuingia mikataba ili ujenzi uanze rasmi. Nakuhakikishia Mheshimwa Mbunge tuendelee kushirikiana ili maendeleo kutokana na mawasiliano yaweze kupatikana. Ahsante sana.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Mnara wa TBC – Kiteto?

Supplementary Question 2

MHE. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa fursa.

Je, wakandarasi waliopewa kazi ya kujenga minara katika Kata za Uru Shimbwe, Kibosho Kati na Mabogini wako katika hatua gani? Kwani wananchi wanashauku kubwa kuona minara hii ikijengwa na ikianza kufanya kazi.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Profesa Ndakidemi Patrick Mbunge wa Moshi vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mradi wetu wa Tanzania ya Kidijitali Mheshimiwa Ndakidemi alipata kata tatu ambayo ni Uru Shimbwe ambapo mtoa huduma Tigo anaenda kuweka huduma ya mawasiliano. Pia na Kibosho Kati ni Tigo vilevile, na Mabogini tutakuwa na Vodacom.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu katika swali la nyongeza la Mheshimiwa Olelekaita, watoa huduma wako katika hatua mbalimbali; nafikiri Waheshimiwa wengi tayari wameshanipa mrejesho kwamba wameanza kuwaona wanapita kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wanapata maeneo kwa ajili ya kuingia mikataba ya ujenzi wa minara yetu ya mawasiliano. Ahsante sana.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Mnara wa TBC – Kiteto?

Supplementary Question 3

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Mheshimiwa Waziri nakuja kwako tena leo kwa mara ya saba, naomba commitment yako. Je, ni lini utatuboreshea mawasiliano kwenye Kata ya Mkomba, Kata ya Kapele na Ming’ong’o Chitete na maeneo mengine yote ambaypo kuna changamoto ya mawasiliano ndani ya Jimbo la Momba?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Condester Sichalwe kwa niaba ya wananchi wake wa Jimbo la Momba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa Mheshimiwa Mbunge amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba anawatetea wananchi wake wa Jimbo la Momba; lakini kwa bahati mbaya katika Mradi wetu wa Tanzania Kidijitali haikuweza kuchukua kata zote kwa sababu tunaelewa kwamba changamoto ya mawasiliano bado ni kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini habari njema sasa ni kwamba Mheshimiwa Rais ameshapata fedha na tayari Wizara yetu iko katika mchakato wa kukamilisha mambo ya mikataba ili tupate fedha kwa ajili ya kwenda kujenga minara mingine Zaidi. Ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kata ambazo amezitaja tutahakikisha kwamba zinakuwa sehemu ya utekelezaji wa mradi huo, ahsante sana.

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Mnara wa TBC – Kiteto?

Supplementary Question 4

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Je, ni lini Serikali itajenga minara ya kutosha kwa ajili ya Jimbo la Mwibara?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Charles Kajege Mbunge wa Mwibara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kajege tayari ameshanijulisha changamoto ya mawasiliano katika jimbo lake na tayari maeneo yake nimeshayachukua tutawatuma wataalamu wetu wakafanye tathmini ili tujiridhishe na ukubwa wa tatizo ili tupeleke ufumbuzi wa tatizo kulingana na changamoto iliyoko kule, ninakushukuru sana.