Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuhakikisha wazee zaidi ya miaka 60 wanaostahili kupata huduma za afya bila malipo wanapata huduma hizo?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza naipongeza Serikali kwa kufanya zoezi la kuhakiki na kubaini wazee hao ambao hawana uwezo. Pia, pamoja na kuwabaini, Serikali ikawapatia vitambulisho vya ICHF kwa ajili ya kupata matibabu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto iliyopo ni kwamba pamoja na kupewa hivyo vitambulisho, wakienda kwenye maeneo ya kupata huduma za afya wanaishia kutangatanga kwa sababu hawapati dawa.

Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha kwamba wazee hawa sasa watapata dawa bila matatizo?

Swali la pili; huko nyuma kulikuwa na slogan ilikuwa inasema” Mpishe Mzee Kwanza” sasa hivi slogan hiyo imeanza kupotea, wazee wanahangaika, wakienda kupata huduma sehemu nyingine hata hospitali na maeneo mengine, hakuna anayejali.

Ni upi mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba tunarudi kwenye mkakati ule wa mwanzo wa kuhakikisha wazee wanapishwa ili kupata huduma kwanza ili wakaendelee na mambo yao mengine? Ahsante. (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hawa wazee kwenda kwenye vituo vya huduma za afya pamoja na vitambulisho vyao wanakuwa hawapati huduma, tutafanya ufuatiliaji kwa sababu huenda wako watu ambao hawawathamini wazee hawa waliotambuliwa kuwa hawana uwezo kwa mujibu wa mwongozo uliowekwa na Wizara Mama ya Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, tutashirikiana na Mabaraza ya Wazee yaliyopo nchini kote ili kufuatilia na kupata maoni ya wazee hawa wasiopata hizo huduma ni kwenye maeneo gani hasa, kwa sababu vipo vituo vya afya vingine vinafanya vizuri sana. Huenda ni baadhi ya maeneo ambayo tutayafuatilia tuyaibue na tushirikiane na Mheshimiwa Waziri wa Afya kuchukua hatua stahiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala hili la kampeni ya “Mpishe Mzee, Mzee ni Tunu Apate Huduma”, kama kuna mahala pameanza kusinzia pia tutafanya ufuatiliaji maana kampeni hii ni endelevu na tuliianzisha mwaka 2021 na imeendelea vizuri mwaka 2022. Sasa kama kuna mahala panalegalega, napeleka tu salamu kwa wale wanaotakiwa kufanya kazi hiyo wakiwemo Maafisa Ustawi wa Jamii wakishirikiana na Wakuu wa Vituo kupitia Waziri mwenye dhamana ya afya, tutafanya ufuatiliaji ili kuiinua tena kampeni hiyo. (Makofi)