Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Mahakama ya Wilaya ya Urambo?

Supplementary Question 1

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya kuendelea kuboresha mahakama zetu hapa nchini na hii itatusaidia hata ukienda kuhukumiwa kule uende vizuri vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina swali moja tu la nyongeza. Kwa kuwa Serikali ina mpango wa kujenga mahakama ikiwemo hiyo ya Urambo aliyojibu, lakini Halmashauri ya Wilaya ya Uyui mpaka leo tunatumia majengo ya Mkuu wa Wilaya: Je, ni lini Halmashauri ya Wilaya ya Uyui nayo itajengewa Mahakama ya Wilaya? Nashukuru.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Venant Daud, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Venant Daud, Mbunge wa Uyui pamoja na Mheshimiwa Almas Maige, wamekuwa wakifatilia ujenzi wa mahakama katika Wilaya yao ya Uyui. Pia nampongeza Mheshimiwa DC kwa kutupatia ofisi yake na majengo ili kazi za mahakama ziendelee. Nimjulishe Mheshimiwa Venant kwamba tunajenga Mahakama ya Uyui mwaka huu wa fedha, na tayari utaratibu unaendelea kumpata mkandarasi.