Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kwa mawe Korongo la Starehe ambalo linahatarisha maisha ya wananchi wa Kata ya Nyamisangara, Tarime?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika korongo lile zipo nyumba ambazo ziko jirani sana, wananchi na wakazi wa Mtaa ule wangependa kujua wale wananchi waliopo karibu na korongo zile kaya, je, Serikali ina mpango gani, watawafidia au itakuwa namna gani?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; korongo hili ni hatarishi sana; je, ni lini hasa Serikali itaanza ujenzi wa korongo hili? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kembaki; la kwanza hili la nyumba zilizopo jirani na korongo hili. Kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi kwamba Serikali itatenga fedha katika mwaka wa fedha 2024/2025 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa daraja hili kwenye korongo.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nichukue nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kumwelekeza Meneja wa TARURA, Mkoa wa Mara kwa kushirikiana na Meneja wa TARURA, Wilaya ya Tarime kwenda kufanya tathmini katika eneo hili na kuona hizi nyumba ambazo Mheshimiwa Kembaki amezitaja zipo umbali gani kutoka kwenye road reserve ambayo imewekwa na kisha kuwasilisha taarifa hii TARURA Makao Makuu.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili, nirejee tena majibu yangu ya msingi kwamba Serikali itatenga fedha mwaka wa fedha 2024/2025 na fedha hii itakapotengwa ndipo kazi hii itatangazwa na kuanza kujengwa daraja hili katika Bonde hili la Mto Starehe.