Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amina Ali Mzee

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuliwezesha Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kujiendesha kibiashara?

Supplementary Question 1

MHE. AMINA ALI MZEE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, Serikali haioni sasa ipo haja ya kuharakisha utungaji wa sheria hiyo, Ili shirika liweze kujiendesha kibiashara?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, Serikali haioni haja ya kuhakikisha inalipatia magari shirika liweze kujiendesha na liweze kujitegemea ili liendane na soko nchini? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali ya nyongeza la Mheshimiwa Amina, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa Shirika la Utangazaji (TBC) ambalo linaongozwa kwa notice ya Serikali 186 ya mwaka 2007 kutokana na Sheria ya Mashirika ya Umma ya mwaka 2002. Serikali ipo katika mchakato huo wa kuhakikisha kwamba utungaji wa sheria ya mwaka 2003 unafanyika kwa haraka. Sasa tayari tupo katika hatua ya pili ya uchambuzi, baada ya kuwa tumepata maoni mahususi kutoka Wizara ya Fedha. Hivyo, utungaji wa sheria huu upo katika hatua nzuri na baada ya hapo tutafikisha katika Bunge lako tukufu kwa ajili ya utaratibu unaotakiwa.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, tayari Serikali ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kuboresha vitendea kazi. Vitendea kazi ni pamoja na magari, ni kweli kabisa tunahitaji kuwa na OB Van za kutosha katika kanda zetu, lakini katika mikoa kulingana na ukubwa wa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, tayari ametoa fedha kwa ajili ya kuboresha studio zetu za TBC kwa kiwango ambacho kinaendana na teknolojia ya sasa. Tayari ametoa Shilingi bilioni 3.235 kwa ajili ya studio iliyopo Barabara ya Nyerere, kwa ajili ya TBC Taifa na TBC FM. Vile vile alitoa Shilingi milioni 601.8 kwa ajili ya kuboresha studio yetu ya hapa Dodoma.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tuendelee kumshukuru Mheshimiwa Rais, kwa kazi kubwa anayoifanya, kwa sababu hiki ni chombo cha umma ambacho kipo kwa ajili ya kuelimisha, kuburudisha na kutoa huduma kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kukushukuru sana.