Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga kingo za Mto Kanoni unaopita katikati ya Mji wa Bukoba?

Supplementary Question 1

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nina swali moja la nyongeza.

Je, wakati huo ambao taratibu za kujenga kingo zinaendelea, Serikali haioni haja ya kutoa fedha angalau Shilingi milioni 100 kwa ajili ya kusafisha Mto Kanoni ili kupunguza athari zake hususan Kata nne ambazo zinaathirika zaidi; Kata ya Bilele, Bakoba, Hamugembe na Nshambya? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver Daniel Semuguruka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Oliver Semuguruka kwa kadri anavyowakilisha wananchi wa Mkoa wa Kagera, lakini pia, anavyowasemea ipasavyo wananchi wa Mkoa huo. Vile vile nampongeza sana Mheshimiwa Stephen Byabato, Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini anavyowasemea na kuwawakilisha ipasavyo wananchi wa Bukoba na anavyoshirikiana na Waheshimiwa Wabunge wa Viti Maalum. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitambue kwamba wapo Waheshimiwa Madiwani, Mstahiki Meya na Mkurugenzi wa Bukoba Manispaa. Nitoe maelekezo kwa Mkurugenzi kuhakikisha wakati tunasubiri mradi huu wa ujenzi wa kingo kwa maana ya mradi wa TACTIC, watenge fedha kwa kadri inavyowezekana kuendelea kuboresha kingo na kina za Mto Kanoni ili kuzuia madhara hayo wakati bajeti hiyo inakuja kutekelezwa, ahsante. (Makofi)