Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule ya Sekondari ya Igurubi iliyopo katika Wilaya ya Igunga kuwa ya kidato cha tano na cha sita?

Supplementary Question 1

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naishukuru na kuipongeza Serikali yetu ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutupatia fedha kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya elimu. Wiki iliyopita walitupatia shilingi bilioni mbili kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya elimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu, Shule ya Sekondari ya Igurubi ilianzishwa mwaka 2000 na sasa ina miaka zaidi ya 20. Ina madarasa 19 lakini yanayotumika ni tisa tu, madarasa kumi yamebaki, ambayo inaongeza idadi ya miundombinu ya majengo ambayo tunaweza tukaibadilisha ikawa mabweni na mabwalo. Je, nini kauli ya Serikali katika kuhakikisha tunapata kidato cha tano na sita kwenye Shule ya Sekondari ya Igurubi? Aahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, najibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ngassa, kwanza naanza kwa kumpongeza yeye Mheshimiwa Ngassa kwa kuweza kufuatilia sana suala hili ya Shule ya Igurubi. Amekuja ofisini mara kadhaa kwa ajili ya kufuatilia iweze kupandishwa hadhi na kuwa shule ya A level.

Mheshimiwa Naibu Spika, shule hii kama nilivyokwishasema kwenye majibu yangu ya msingi, tayari Serikali imeshapeleka fedha nyingi kwa ajili ya miundombinu mingine ya madarasa. Tutaendelea kutafuta fedha kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Igunga kwa ajili ya kujenga miundombinu inayohitajika kwa ajili ya kusajiliwa. Baada ya miundombinu hiyo kuweza kujengwa tutawasiliana na wenzetu wa Wizara ya Elimu kwa ajili ya kuweza kuipandisha hadhi shule hii na kuwa ya kidato cha tano na sita. (Makofi)