Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza: - Je, zipi athari za mvua zilizonyesha Novemba, 2023 na Serikali imejipangaje kuzuia athari hizo kujirudia?

Supplementary Question 1

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Nina mambo mawili. La kwanza, naipongeza sana Ofisi ya Waziri Mkuu kwa sababu ya kujipanga kupambana na maafa ambayo kwa kweli sote kama Taifa tumeyaona. Tunawashukuru na tunawaomba waendelee kujipanga zaidi kwa sababu mambo haya ni ya kujirudia na hasa ukizingatia mabadiliko ya tabianchi ambayo yanaendelea na sote tunashuhudia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kwangu ni ushauri. Naomba sana Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa sababu mambo ya majanga ni mambo ambayo yasiyotabirika, na yanahitaji mafunzo na uwezo kwenye taasisi zake zote, na kwa sababu ni kazi zinazofanywa kwa ushirikiano kati ya Bara na Zanzibar, naomba Ofisi ya Waziri Mkuu, basi ione namna nzuri inavyoweza kuwasaidia wenzetu kwa upande wa pili ili nao waweze kujipanga vizuri kwa kuweza kukabiliana na maafa haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapokea pongezi za Mheshimiwa Zahor, nasi tunaendelea kumpongeza lakini pia tunampa pole kwa maafa yaliyotokea kule Jimboni kwake Mwera. Tunamhakikishia kwamba Ofisi ya Waziri Mkuu tuko imara na tutaendelea kujipanga zaidi katika eneo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia jambo la pili kuhusu ushauri, tumepokea ushauri wake. Kwa kuwa masuala haya pia yanaratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza, nasi Ofisi ya Waziri Mkuu tuna vikao vyetu vya mashauriano tunapitia Ofisi ya Makamu wa Pili, tutaendelea kuboresha ushirikiano huo ili kuendelea kuwafikia wananchi katika maeneo yote katika nchi yetu, ahsante sana. (Makofi)