Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafunga mitambo ili wananchi wa Tarafa ya Kilolo wapate matangazo ya Redio ya Taifa (TBC)?

Supplementary Question 1

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Awali ya yote niishukuru sana Serikali kwa majibu mazuri na kwa ahadi iliyotolewa ya kujenga mnara kwa ajili ya TBC. Niwapongeze pia kwa minara mingi ya simu ambayo inaendelea kujengwa katika Wilaya ya Kilolo, ambayo inatatua changamoto ya mawasiliano. Nawapongeza sana Waziri pamoja na Naibu Waziri, kwa kazi nzuri wanayoifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali yangu madogo ya ngongeza, kwa kuwa mawasiliano yanaendana na uwekaji wa Mkongo wa Taifa. Je, ni lini Serikali itaweka Mkongo wa Taifa kufika katika Wilaya ya Kilolo?

Swali dogo la pili, Kwa kuwa tayari huu ujenzi wa mnara wa TBC process imeanza, nijue ni lini unatarajia kukamilika ili wananchi pia waweze kupata matumaini ya kupata matangazo ya TBC kwa uhakika? Ahsante. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Justin Lazaro Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nitumie fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge, kwa kazi kubwa anayoifanya katika Jimbo la Kilolo na kwa kazi anayoifanya katika kushirikiana na Serikali pale ambapo tunafika katika Jimbo, lake ili kuhakikisha kwamba tunaweka miundombinu ya mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda katika swali lake la pili kwamba ni lini sasa TBC itaanza kufanya kazi pale. Kama ambavyo nimejibu katika jibu langu la msingi umepangwa kukamilika ifikapo Juni, 2024. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge, itakapofika Juni, 2024 naamini kwamba kazi itakuwa imeanza kwa wananchi wa Kilolo kupata huduma ya mawasiliano ya utangazaji ya TBC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza ni dhamira ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi inaongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuhakikisha kwamba Wilaya zote nchini, Wilaya 139 ifikapo Disemba, 2024 wote tutakuwa tumefikisha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano. Ifikapo Juni, mwaka huu tutakuwa tumekamilisha kufikisha Mkongo wa Mawasiliano katika Kata 99. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa sababu pale Mafinga tayari tuna pop yetu, pale Iringa Mjini tuna pop na kutoka Iringa Mjini mpaka Kilolo kuna kilometa 33, kwa hiyo tutahakikisha kwamba tumefikisha na tutajenga Kituo cha Mkongo katika eneo lake la Wilaya ya Kilolo. Nakushukuru sana.

Name

Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafunga mitambo ili wananchi wa Tarafa ya Kilolo wapate matangazo ya Redio ya Taifa (TBC)?

Supplementary Question 2

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Je, ni lini Serikali itajenga mtambo kwa ajili ya usikivu wa TBC, katika Tarafa ya Kilimarondo, Jimbo la Nachingwea? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu katika swali la Mheshimiwa Justin, tunao ujenzi wa vituo takribani 14 ambavyo vinaendelea, vilevile katika bajeti ijayo tunatarajia kuongeza vituo vingine nimuombe sasa Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu ni eneo specific ambalo sikutarajia angeweza kuligusia, akitoka hapa tukutane ili niangalie kama lipo katika vile vituo 14 ama vile vituo ambavyo tunaenda kuviongeza ili tuhakikishe kwamba tunakuwa na majibu ya uhakika kwa ajili ya wananchi wake wa Jimbo la Nachingwea. Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafunga mitambo ili wananchi wa Tarafa ya Kilolo wapate matangazo ya Redio ya Taifa (TBC)?

Supplementary Question 3

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Maeneo mengi katika Wilaya ya Simanjiro, hakuna kabisa mawasiliano ya simu.

Je, ni lini sasa Serikali itapeleka mawasiliano katika Kata ya Ruvu Remit, Kata ya Loiborsiret, Kata ya Oljoro No. 5, Kata ya Komolo, Kata ya Kitwai, Kata ya Msitu wa Tembo, Kata ya Naberera na Kata ya Loiborsoit? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti kuna maeneo mengi ambayo bado yana changamoto lakini kwa Jimbo la Simanjiro, katika miradi yetu 758 kuna Kata takribani nne ambazo tunazipelekea huduma ya mawasiliano. Katika Kata hizo kuna zingine ambazo amezitaja sina uhakika kama zitakuwemo lakini namuomba tukitoka hapa tuweze kuonana nizijue specific ni Kata zipi na tuone kama kutakuwa na uwezekano wa kupata fedha ili na zenyewe tuziingize katika utekelezaji na wananchi wote wa Simanjiro ambao ni wananchi na wapiga kura wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Wabunge wote waweze kupata huduma ya mawasiliano, nakushukuru sana.

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafunga mitambo ili wananchi wa Tarafa ya Kilolo wapate matangazo ya Redio ya Taifa (TBC)?

Supplementary Question 4

MHE. OMARI ISSA KOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. changamoto iliyopo kwenye Jimbo la Kilolo, ni sawa na changamoto iliyopo Mkoa wa Kaskazini Pemba, juu ya usikivu wa TBC. Je, Serikali inatoa kauli gani kuwatolea wananchi changamoto hii, ukizingatia TBC ni Redio ya Taifa?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kupokea changamoto ya Mheshimiwa Mbunge ili Serikali tukaifanyie kazi na baada ya hapo tutamshirikisha Mheshimiwa Mbunge ili atupatie ushirikiano specific katika maeneo ambayo ameyataja. Nakushukuru.