Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA K.n.y MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, mazungumzo kati ya Serikali na mwekezaji wa Kiwanda cha Mbolea Kilwa kuhusu gesi asilia ya Songosongo yamefikia hatua gani?

Supplementary Question 1

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kwa kuwa Mheshimiwa Ally Mohamed Kassinge ameuliza swali hili mara nyingi hapa Bungeni; je, wananchi wa Kusini hasa Kilwa Kusini watarajie nini juu ya uwekezaji huu?

Swali la pili, Hanang katika Ziwa Gendabi pale kuna chumvi nyingi sana, tulipata mwekezaji na tukampa eneo lakini hakuna kinachoendelea.

Je, Wizara ya Viwanda na Uwekezaji watawasaidiaje wananchi wa Hanang ili kuhakikisha kwamba ile chumvi inaweza kuchakatwa na hatimae kuweza kutumika hapa nchini? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO K.n.y. WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inafanya kazi kwa taratibu na taratibu zilizopo ndiyo maana tunasema kwamba sasa tuko kwenye majadiliano na majadiliano ni lazima mfikie point ya win-win situation, kwamba kila upande uliridhike na majadiliano ambayo yatakuwa yanaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Government negotiation team inaendelea na haya majadiliano, yatakapokamilika maana yake wananchi wa Kusini watarajie kwamba kiwanda hicho kitajengwa na kitawanufaisha wananchi wote nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu eneo la Gendabi katika Jimbo la Hanang ambako kuna mwekezaji na bado anasuasua Wizara ya Viwanda na Biashara inapokea na itarudi kwenda kuzungumza na hao watu ili kuona namna bora ya kufanikisha jambo hilo ambalo litakuwa faida kwa wananchi wa Hanang na naamini kwa Taifa zima kwa ujumla. Ahsante.

Name

Aziza Sleyum Ally

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA K.n.y MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, mazungumzo kati ya Serikali na mwekezaji wa Kiwanda cha Mbolea Kilwa kuhusu gesi asilia ya Songosongo yamefikia hatua gani?

Supplementary Question 2

MHE. AZIZA S. ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, Serikali inatoa tamko gani kuhusu Kiwanda cha Nyuzi Tabora ambacho kwa muda mrefu kimefungwa hakifanyi kazi? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO K.n.y. WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, tunajua tulikuwa tunazungumzia suala la mbolea na Mheshimiwa Mbunge ameuliza kuhusu Kiwanda cha Nyuzi na sisi Wizara ya Kilimo pamoja na Viwanda na Biashara, jambo hili tunalifahamu. Tunafahamu changamoto ambazo zipo katika viwanda vingi vya nyuzi na moja ya mkakati wa Wizara ya Kilimo ambao tuko nao sasa hivi, ni kuhakikisha tunafufua viwanda vingi ili pamba yote inayozalishwa hapa nchini iweze kutumika na hivi viwanda viweze kufanya kazi. Kwa hiyo, mpango tulionao ni huo kwa sasa na tuko serious katika eneo hili, ahsante sana. (Makofi)