Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kufufua Skimu za Umwagiliaji za Ikindwa, Malolo na Nhalanga – Bukene ili zifanye kazi kwa tija?

Supplementary Question 1

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, pamoja na majibu yanayoleta matumaini kutoka kwa Waziri, nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilitumia fedha nyingi miaka kadhaa iliyopita kujenga skimu hizi za umwagiliaji, hasa hii Skimu ya Kamalanga ambyo iliigharimu zaidi ya shilingi bilioni moja lakini na hii Skimu ya Malolo pamoja na ya Ikindwa. Sasa Mheshimiwa Waziri amesema kwamba Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kufufua skimu hizi za umwagiliaji ambalo ni jambo jema na fedha hizo ziko kwenye mwaka huu wa fedha.

Je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari wakati wakiendelea na hatua za mwanzo za kufufua skimu hizi, aweze kuongozana na mimi baada tu ya Bunge hili tuende Bukene akayaone hayo Mabwawa ya Malolo, Ikindwa na Nhalanga ili aweze kutia msukumo na kuhakikisha mabwawa hayo yanafufuliwa na yanaleta tija katika kilimo cha mpunga ambacho tunakitegemea sana kwenye Jimbo la Bukene? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge Selemani Zedi, nipo tayari na nitaongozana naye kufika katika maeneo yote niliyotaja, nimhakikishie tu Mheshimiwa Dkt. Samia ametuthibitishia kwamba maeneo hayo yatafikiwa na yatajengwa, ahsante. (Makofi)