Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaruhusu ushindani wa kibiashara kwenye mazao ya chai na maziwa Wilayani Rungwe?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; Rungwe Tea Growers ambayo ilianzishwa mwaka 1966 na ikaishia mwaka 1976, ilikuwa ina wakulima wanaonunua chai wenyewe na walikuwa na Hisa asilimia 90 na asilimia 10 ilikuwa ya Serikali. Ni lini Serikali itawalipa hisa zao wakulima hawa ambao ni zaidi ya miaka mingi hawajapata hisa zao?

Swali la pili; Mheshimiwa Naibu Waziri, Waziri Mkuu aliunda Tume ya Wakulima kwa ajili ya kufuatilia wakulima wa chai. Sasa ni muda mrefu umepita. Ni lini Seriakli italeta majibu ya Tume hiyo kuelezea malalamiko ya wakulima wa chai na kuhusu maziwa ninaomba uende sehemu ya field ili upate majibu sahihi, ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kuhusu sula la hisa kwa wakulima wa Rungwe Tea Growers ambao hawajalipwa kwa muda mrefu, tumelipokea jambo hili na najua liko chini ya usimamizi wa Hazina, Wizara ya Kilimo pamoja na Hazina tutakaa pamoja na kuona namna ambavyo tunaweza tukalisaidia hili jambo kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Tume ambayo iliundwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu kupitia madai yaliyoletwa katika maeneo ya chai, hususan katika maeneo ya Rungwe, ninaamini tayari taarifa hiyo imeshakamilika na kuna mapendekezo ambayo yalishatolewa na yanaendelea kufanyiwa kazi. Kwa hiyo, Wizara tutaleta taarifa hiyo katika maeneo ambayo yanahusika na ikibidi katika Bunge lako Tukufu, ahsante sana. (Makofi)