Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani kwa watumishi wanaokaimu nafasi kwa muda mrefu katika Vyuo vya FETA ikiwemo Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. AGNESS E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ninayo maswali mawili ya nyongeza.

(a) Je, kwa nini Serikali haiwalipi Mameneja wanao kaimu katika Vyuo vya Uvuvi pamoja na Wakurugenzi ambao wamekaimu kwa miaka zaidi ya 12?

(b) Wizara haioni imedumaza maendeleo ya Vyuo vya Uvuvi nchini ikiwemo Mikindani Mtwara kwa kuwakaimisha mameneja wake na kutokuwa na taratibu za uendelezaji? (Makofi)

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, nianze na hili la kwanza kwamba haiwalipi makaimu; utaratibu wa Serikali uko wazi kwamba mtumishi yeyote anaweza akakaimishwa nafasi yoyote kama ana vigezo na upekuzi ukikamilika anataeuliwa kushika nafasi hiyo rasmi kulingana na maelekezo ya Serikali yalivyo.

Mheshimiwa Spika, kwa kesi hii ya Mikindani, tumekuwa tukifanya upekezi kwa muda mrefu wenye sifa wanakosekana lakini tumeendelea kutafuta watu wenye uwezo wa kushika nafasi hizo katika maeneo hayo na sasa Serikali inaelekea mwishoni kukamilisha taratibu za uteuzi ili apatikane Mkurugenzi atakayekuwa ameshika nafasi katika eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na kwamba anafuatilia sana kwa karibu jambo hili kwa muda mrefu, nimhakikishie kwamba ndani ya muda mfupi tutakwenda kukamilisha jambo hili. Lengo la Serikali ni kuweka watu wenye weledi, wenye uwezo wa kushika nafasi hizo na si lengo kudumaza vituo hivyo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo naomba kuwasilisha.
SPIKA: Mheshimiwa Waziri, nadhani kulikuwa na swali la pili linalohusu kudumaa kwa wale wanaokaimu, kwamba wanashindwa kuendelezwa.

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi tumeendelea kutoa mafunzo mbalimbali kwa wataalam wetu, kwa hivyo wataalam wale wanapopata mafunzo wanaojiendeleza wanakuwa na sifa za kushika nafasi hizo, kwa hiyo tumekuwa tukiangalia katika hao tuliowapa mafunzo, Je, wapi wana uwezo wa kushika nafasi hizi za kukaimu nafasi za juu katika uongozi?

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tumeendelea kutoa mafunzo, mafunzo hayo yamezidi kuwasaidia wataalam wetu kujipatia uwezo wa kushika nafasi hizi na lengo la Serikali ni kuhakikisha kwamba wale wote wenye uwezo wa kushika nafasi hizi wanapewa nafasi hizo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.