Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kurahisisha mfumo mzuri wa kutoa msamaha wa kodi kwa wakandarasi wanaojenga barabara Halmashauri ya Msalala?

Supplementary Question 1

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia fursa hii ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mamlaka ya utoaji msamaha wa kodi yamewekwa kwa Kamishna Mkuu wa TRA, sasa Serikali haioni haja ya kugatua madaraka na kuwapatia mamlaka mameneja wa mikoa ili waweze kutoa misamaha hiyo ya kodi ili kurahisisha kazi za ujenzi wa barabara ufanyike kwa haraka? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kumekuwa na malimbikizo ya madai ya VAT kwa wakandarasi, sasa Serikali haioni haja ya kuweka mchakato rahisi wa kuweza kuwalipa haraka wakandarasi hao ili waweze kutumia fedha zao ili kuijiendeleza kwenye miradi yao ya ujenzi wa barabara? Ahsante (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza, ushauri wake Mbunge umepokelewa na unaenda kufanyiwa kazi hasa katika kipindi hiki cha ukusanyaji wa maoni, Serikali itaangalia na wataalamu wetu watatushauri, kama ipo tija ya kupeleka mikoani, basi Serikali itafanya hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, madeni ya makimbikizo ya madai ya VAT Refund, yaliyo mengi tayari yameshahakikiwa na yamelipwa na yale ambayo yamewasilishwa siku za karibuni, yanahakikiwa na yakikamilika tu Serikali italipa refund hiyo. (Makofi)