Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza:- Je, Serikali itawaunga mkono World Vision kuendeleza ujenzi wa Chuo cha VETA Choma?

Supplementary Question 1

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, taasisi binafsi zimekuwa wadau wakubwa katika suala zima la elimu ya ufundi na kuna uwekezaji mkubwa, je, Serikali haioni wakati umefika sasa wa kuwa na mikataba na waendeshaji wa vyuo hivi kama ilivyo hospitali binafsi kwenye mkataba wa DHH? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, Wilaya ya Kilosa ilitoa kwa makusudi Chuo cha VETA pale Mikumi kwa Serikali na toka nimekabidhi hakuna ukarabati wowote ambao umefanyika mpaka sasa; je, Serikali haioni wakati umefika sasa wa kurudisha chuo hiki kwa halmashauri ambayo ni miliki wa awali baada ya Serikali kushindwa kuwekeza chochote? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Londo, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, Mheshimiwa Mbunge, anatoa ushauri kwamba, kwa nini sasa Serikali haioni umuhimu wa kuingia mikataba ya ubia juu ya uendeshaji wa vyuo hivi? Kwa vile huu ni ushauri ambao Mheshimiwa Mbunge anatupa kama Serikali, nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba ushauri wake tumeupokea tutakwenda kuufanyia tathmini ya kina ili kuweza kuona maeneo gani ambayo Serikali inaweza ikaingia ubia pamoja na mashirika binafsi katika uendeshaji wa vyuo hivi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la pili, kuhusiana na Chuo hiki cha Mikumi nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge tumepeleka fedha katika mwaka uliopita wa fedha pale kwa ajili ya kufanya ukarabati, lakini na katika mwaka huu wa fedha 2023/2024 tumetenga fedha kwa ajili ya kuendelea na ukarabati pamoja na uongezaji wa majengo.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile mwakani 2024/2025 tumetenga fedha kwenye bajeti yetu kuhakikisha kwamba vyuo vyote vile vya zamani ambavyo tulivichukua kutoka kwa taasisi binafsi pamoja na halmashauri vinaenda kukarabatiwa, kuongezewa majengo, lakini vilevile kupeleka watumishi na vifaa kwa ajili ya mafunzo kwa vijana wetu. Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Munira Mustafa Khatib

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza:- Je, Serikali itawaunga mkono World Vision kuendeleza ujenzi wa Chuo cha VETA Choma?

Supplementary Question 2

MHE. MUNIRA MUSTAPHA KHATIB: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali ina mpango wa kujenga VETA kila Wilaya sambamba na hilo, je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapa vijana wanaosoma VETA mikopo? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, safari ni hatua na tulishaanza utoaji wa mikopo kwanza kwa vijana wetu ambao walikuwa wanasoma elimu ya juu, lakini mwaka uliopita tumeanza kutoa mikopo katika elimu ya kati na kwa vile tunaendelea na utaratibu huu kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha tunaweza tukafikia katika maeneo yote.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari Serikali imeshafanya kazi kubwa sana kwenye eneo hili la mafunzo ya VETA, kwa sababu ada ya vijana hawa au ada ya mafunzo kwa wale wanafunzi wa kutwa ni shilingi 60,000 na wale wanafunzi wa bweni ni shilingi 120,000. Serikali inachangia ruzuku kwa kila mwanafunzi zaidi ya shilingi 1,150,000 kwa kila mwanafunzi kwa mwaka. Kwa hiyo, tutaendelea kutoa ruzuku hii na tutaangalia vilevile uwezekano wa kuweza kutoa mikopo katika kada hii muhimu.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza:- Je, Serikali itawaunga mkono World Vision kuendeleza ujenzi wa Chuo cha VETA Choma?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa hii nafasi, je, ni lini ujenzi wa Chuo cha VETA kinachojengwa Kata ya Uwiro, Arumeru Mashariki utamalizika? Ahsante. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, nikiri kwamba kuna ujenzi ambao unaendelea katika Jimbo la Mheshimiwa Pallangyo, kule Arumeru na mimi mwenyewe nimeshafanya ziara zaidi ya mara mbili kwenye eneo lile kuangalia maendeleo ya chuo kile.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, malengo yetu ni kuhakikisha kwamba mpaka kufika mwezi Oktoba, mwaka huu vyuo hivi katika awamu ya kwanza viwe vimekamilika ili mwezi wa Novemba tuweze kuanza kutoa zile kozi za muda mfupi na Januari mwakani tuweze kuanza kutoa zile kozi za muda mrefu.

Kwa hiyo, hayo ndio malengo yetu tutahakikisha kwamba, ifikapo mwezi Oktoba, vyuo hivi vimekamilika, nakushukuru.