Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza:- Je, Serikali haioni haja ya mikopo ya 10% inayotolewa na halmashauri kutolewa kwa mjasiriamali mmoja mmoja?

Supplementary Question 1

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Kwa kuwa Serikali imeona kwamba ipo haja ya kufanya tathmini ili kuweza kukidhi uhitaji wa kukopesha mjasiriamali mmoja mmoja, sasa nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; je, tathmini ambayo wanategemea kufanya, itakwenda sambamba na maboresho ya mikopo hii yanayoendelea hivi sasa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, ni lini Serikali itatuletea marekebisho ya Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa ili iweze kukidhi haja ya kukopesha mjasiriamali mmoja mmoja? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge, ni kweli kwamba Serikali inaona umuhimu wa kufanya mapitio na kuona uwezekano wa kukopesha mjasiriamali mmoja mmoja badala ya vikundi na hilo litafanyiwa tathmini na kuona ufanisi na uwezekano wake wa kufanyika vizuri.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa watu wenye ulemavu wanapata mikopo ya 10% hata akiwa mtu mmoja mmoja; kwa hiyo makundi yaliyobaki ni ya vijana pamoja na wanawake. Kwa hiyo tutalifanyia tathmini suala hilo. Suala hili tutalifanya baada ya kupitia sheria yetu ya mikopo ya 10%, baada ya maboresho ya mikopo hii ambayo inatarajiwa kuanza mwezi Julai mwaka huu wa fedha. Ahsante sana.