Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Kituo cha Afya cha Nhobola kitafanyiwa ukarabati baada ya kuwa chakavu kwa kipindi kirefu ikiwa ni pamoja na upanuzi wa kituo hiki?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, kwanza, naomba nitoe shukrani kwa Serikali kwa taratibu na mipango iliyoiandaa kwa ajili ya kuhakikisha vituo hivi vinakarabatiwa ikiwa ni pamoja na kufanya upanuzi. Swali la kwanza; nataka tu nipate commitment ya Serikali, je, kwa huu mwaka wa fedha 2024/2025 unaokuja kituo hiki ni moja kati ya vituo ambavyo vitapewa kipaumbele na kukarabatiwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Kituo cha Afya cha Dulisi, Mwigumbi na Ng’wang’halanga ni moja kati ya vituo ambavyo vina upungufu mkubwa wa miundombinu japokuwa vina sifa ya kituo. Je, Serikali iko tayari kuvitazama vituo hivi na kuhakikisha kwamba miundombinu muhimu iwekwe pale ikiwa ni pamoja na wodi kwa ajili ya wagonjwa, nyumba za watumishi na mochwari katika hivi vituo vya afya vitatu nilivyovitaja? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, katika mpango wa Serikali wa ukarabati wa vituo hivi vya afya tumeanza kwanza na kipaumbele cha ukarabati wa hospitali za halmashauri. Katika hospitali za halmashauri zilizoainishwa 50 tayari hospitali 39 zimeshafanyiwa ukarabati na bado hospitali 11 ambazo tunatarajia kuzikamilisha. Baada ya hapo tutakwenda kwenye ukarabati na upanuzi wa vituo vya afya vikongwe. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, tutakapoanza ukarabati wa vituo vya afya tutahakikisha pia hiki nacho kinapewa kipaumbele, kinakarabatiwa ili kiweze kutoa huduma vizuri zaidi.

Mheshimiwa Spika, la pili, kuhusiana na baadhi ya vituo vya afya ambavyo Mheshimiwa Mbunge amevitaja vyenye upungufu wa baadhi ya majengo. Serikali inatambua na tumeshaelekeza Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kote Nchini kuanza kutenga fedha za mapato ya ndani kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa miundombinu unaopungua kwa awamu. Hata hivyo, Serikali Kuu itatafuta fedha kwa ajili ya kuunga mkono kuhahakikisha majengo hayo yanakamilishwa, ahsante.

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Kituo cha Afya cha Nhobola kitafanyiwa ukarabati baada ya kuwa chakavu kwa kipindi kirefu ikiwa ni pamoja na upanuzi wa kituo hiki?

Supplementary Question 2

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Spika, ni lini Kituo cha Chikobe kitafanyiwa uboreshaji kwa sababu miundombinu yake ni mibovu sana? Nakushukuru.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Chikobe, kitafanyiwa ukarabati mara tutakapoanza kukarabati vituo vya afya baada ya kukamilisha ukarabati wa hospitali za halmashauri.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Kituo cha Afya cha Nhobola kitafanyiwa ukarabati baada ya kuwa chakavu kwa kipindi kirefu ikiwa ni pamoja na upanuzi wa kituo hiki?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Misha kilichopo kwenye Jimbo la Tabora Mjini hakijakamilika. Serikali ina mpango gani wa kukamilisha kituo hiki ili kiweze kuanza kufanya kazi kwa ufanisi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Misha katika Manispaa ta Tabora ni moja ya vituo ambavyo vilipewa fedha na Serikali kwa ajili ya ujenzi na ni kweli kwamba hakijakamilika na tunatafuta fedha kwa ajili ya ukamilishaji. Tumemwelekeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora kutenga fedha kwenye mapato ya ndani ili kuendelea na hatua za ukamilishaji. Ahsante sana.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Kituo cha Afya cha Nhobola kitafanyiwa ukarabati baada ya kuwa chakavu kwa kipindi kirefu ikiwa ni pamoja na upanuzi wa kituo hiki?

Supplementary Question 4

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, nataka nijue je, ni sahihi kituo cha afya kuwa na wodi moja inayolaza mama, baba, watoto na hata watu waliofanyiwa operation?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, utaratibu wa ujenzi wa vituo vya afya upo kwa mujibu wa mwongozo wa ujenzi wa miundombinu hiyo, lakini pia kwa mujibu wa Sera ya Afya. Vituo hivi vinajengwa wodi ya wanawake, wodi ya wanaume, wodi ya watoto lakini pia wodi ya wazazi, majengo ya upasuaji na majengo mengine. Kwa hiyo, siyo sahihi kwamba tunaweza tukawa tuna wodi moja ambayo inatumika na watoto, wanaume na wanawake jambo hilo halikubaliki. Kwa kweli nina uhakika kama kuna sehemu inafanya hivyo, tutachukua hatua kwa haraka, kwa sababu ni suala ambalo halipo katika utaratibu wetu.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Kituo cha Afya cha Nhobola kitafanyiwa ukarabati baada ya kuwa chakavu kwa kipindi kirefu ikiwa ni pamoja na upanuzi wa kituo hiki?

Supplementary Question 5

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Vituo vya Afya, Kata ya Kala, Kata ya Ninde na Kata ya Kate, Wilayani Nkasi? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, vipo vituo vya afya ambavyo bado havijakamilika kikiwemo Kituo cha Afya cha Ninde na vingine ambavyo Mheshimiwa Mbunge amevitaja. Nimhakikishie tu kwamba Serikali imeshaweka mkakati wa kwenda kukamilisha vituo hivi kwa awamu kwa sababu, tumejenga vituo vingi, tunakwenda kwa awamu. Kwa hiyo, nimhakikishie tu kwamba muda utafika, tutakwenda kukamilisha vituo hivyo ambavyo amevitaja.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Kituo cha Afya cha Nhobola kitafanyiwa ukarabati baada ya kuwa chakavu kwa kipindi kirefu ikiwa ni pamoja na upanuzi wa kituo hiki?

Supplementary Question 6

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itafanya ukarabati na upanuzi Kituo cha Afya Masama? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, kituo cha afya ambacho Mheshimiwa Saashisha amekitaja ni miongoni mwa vituo vya afya 202 ambavyo vipo kwenye mpango wa vituo kongwe vya kukarabatiwa na kuongezewa majengo. Ahsante sana.

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Kituo cha Afya cha Nhobola kitafanyiwa ukarabati baada ya kuwa chakavu kwa kipindi kirefu ikiwa ni pamoja na upanuzi wa kituo hiki?

Supplementary Question 7

MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Wilaya ya Nkasi, Kata ya Itete ina vijiji vinne na havina kituo cha afya. Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Itete?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, tulikwishaelekeza halmashauri kuainisha maeneo ya kimkakati ya kata zile ambazo zinakidhi vigezo vya kuwa na vituo vya afya kwa kuzingatia idadi ya wananchi, umbali kutoka kituo cha afya cha Jirani, lakini pia hali ya kijiografia ya eneo hilo. Kwa hiyo, naomba nichukue hoja ya Mheshimiwa Mbunge, Ofisi ya Rais, TAMISEMI tutawasiliana na Halmashauri ya Nkasi na Mkoa wa Rukwa tuweze kuona kama wanakidhi vigezo, baada ya hapo tuweke mipango ya ujenzi wa kituo hicho, ahsante

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Kituo cha Afya cha Nhobola kitafanyiwa ukarabati baada ya kuwa chakavu kwa kipindi kirefu ikiwa ni pamoja na upanuzi wa kituo hiki?

Supplementary Question 8

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itafanya ukarabati na upanuzi katika Kituo cha Afya Mkwedu kilichopo Jimbo la Newala Vijijini? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba nichukue hoja ya Mheshimiwa Mbunge kwamba twende tukakifanyie tathmini kituo hiki cha afya katika Halmashauri ya Newala Vijijini ili tuweze kuona kiasi cha fedha kinachohitajika na tuweke mipango ya kwenda kukarabati, ahsante sana.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Kituo cha Afya cha Nhobola kitafanyiwa ukarabati baada ya kuwa chakavu kwa kipindi kirefu ikiwa ni pamoja na upanuzi wa kituo hiki?

Supplementary Question 9

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza ni lini Serikali itakarabati Kituo cha Afya cha Msandamuungano, kilichopo ndani ya Jimbo la Kwela? Nakushukuru.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba nitumie nafasi hii kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kumwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Sumbawanga Vijijini kutuma wataalamu pale, Mganga Mkuu wa Halmashauri na engineer kufanya tathmini ya gharama zinazohitajika, lakini pia kuanza kuandaa bajeti kupitia mapato ya ndani na kuleta maombi Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kutafuta fedha kwa ajili ya ukarabati wa kituo hicho. Ahsante sana.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Kituo cha Afya cha Nhobola kitafanyiwa ukarabati baada ya kuwa chakavu kwa kipindi kirefu ikiwa ni pamoja na upanuzi wa kituo hiki?

Supplementary Question 10

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itakarabati Kituo cha Afya cha Lunguya? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, kituo cha afya ambacho Mheshimiwa Iddi Kassim amekitaja tutakwenda pia kukitafutia fedha tuweze kukikarabati kwa awamu, lakini pia kuongeza majengo ambayo yanapungua, ahsante sana.

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Kituo cha Afya cha Nhobola kitafanyiwa ukarabati baada ya kuwa chakavu kwa kipindi kirefu ikiwa ni pamoja na upanuzi wa kituo hiki?

Supplementary Question 11

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itakamilisha Kituo cha Afya kilichopo Kata ya Itale, Wilaya ya Ileje ili wananchi waweze kupata huduma iliyokusudiwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Serikali imeshatoa fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa vituo hivi vya afya, vipo vituo ambavyo vimepata milioni 500, lakini vipo ambavyo vimepata milioni 250.

Kwa hiyo, nitaonana na Mheshimiwa Mbunge kujua kituo hiki kilipata shilingi milioni 250, kinasubiri shilingi milioni 250 au kama kilipata milioni 500, tujue kwa nini majengo hayajakamilika na baada ya hapo tutafute fedha kwa ajili ya kukamilisha majengo hayo, ahsante sana.