Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Chuo cha Ufundi VETA katika Mji wa Ifakara?

Supplementary Question 1

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi ya kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza nishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kweli inatusaidia sana. Tuliomba Chuo cha VETA Wilaya ya Kilombero tumepewa, tuliomba barabara ya lami tumepewa, Kiwanda cha Sukari shilingi bilioni 500 tumepewa, mradi wa maji shilingi bilioni 43 tumepewa, Hospitali ya Halmashauri tumepewa, kadhalika na kadhalika. Kwa kweli watu wanaochafua huko nje waache tunamshukuru sana Dkt. Samia kwa kazi kubwa anayoifanya. Naomba kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, halmashauri ambazo zipo katika wilaya hazikupata Vyuo vya VETA, tulikubaliana kwamba, ziatapata shule maalum za ufundi. Je, ni lini ujenzi utaanza wa Shule Maalum ya Ufundi katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Ifakara kuna Chuo cha Ufundi vile vya FDC ambavyo vina eneo kati kati ya Mji wa Ifakara na eneo lile limekuwa likipata wavamizi mara kwa mara, je, Serikali haioni umuhimu wa kwenda kuzungushia fence katika chuo hicho ili kulinda eneo la chuo hicho? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abubakari Damian Asenga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kupekee tupokee pongezi hizo za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, yeye ndio amewezesha hayo yote kutokea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la kwanza kwa kupande wa shule zile za ufundi nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge ni kweli Serikali ina azma ya kujenga shule za ufundi katika majimbo yale ambayo hayakujengewa Vyuo vya VETA. Tunafahamu kwamba hivi Vyuo vya VETA vinajengwa katika wilaya pia tunafahamu kuwa zipo wilaya ambazo zina majimbo zaidi ya moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, iwapo kama VETA imejengwa katika Jimbo moja na wilaya hiyo ina majimbo zaidi ya moja, tafsiri yake shule hizi za ufundi tunakwenda kujenga kwenye yale majimbo ambayo yamekosa fursa za kujengewa vile Vyuo vya VETA.

Kwa hiyo, nikuondoe wasiwasi hivi sasa tupo katika maandalizi ya fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule hizi zipo tayari. Tunafanya upembeuzi yakinifu pamoja na kufanya zile site visit kwa ajili ya kukagua yale maeneo ambayo zitajengwa shule hizi za ufundi na tunapofika Julai tunatarajia shule hizi ziweze kuanza kujengwa rasmi. Kwa hiyo, lini tunaanza? Tutaanza mwaka ujao wa fedha kwa maana Julai mwaka huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa pili kwenye vyuo vyetu vile vya FDC, ni kweli tuna vyuo vya FDC karibu 54 katika nchi yetu. Vilikuwa kwenye hali mbaya sana, vyuo hivi Serikali imeshafanya ukarabati, tumeongeza majengo kwenye baadhi ya maeneo ambako kulikuwa hakuna majengo, tumefanya ukarabati kwenye yale majengo ya zamani, tumenunua vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwenye vyuo hivi, kwa vile sasa shughuli hizi zote zilikuwa zinakwenda kwa awamu, awamu inayofuata sasa tunaangalia kwenye yale maeneo ambayo kuna uhitaji wa kujengewa uzio kwa ajili ya kujenga uzio.

Kwa hiyo, nikuondoe wasiwasi, tunaenda kwa awamu na uzio kwenye vile vyuo ambavyo viko mijini ambavyo tunaona kabisa kuna haja ya kujenga uzio tutakwenda kujenga uzio, ninakushukuru sana.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Chuo cha Ufundi VETA katika Mji wa Ifakara?

Supplementary Question 2

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Waziri, kwanza ninakushukuru kwa kunipa Chuo cha VETA Mbogwe, lakini kazi haifanyiki mpaka sasa hivi hata mafundi wametoka site. Mheshimiwa Waziri, shida ni nini? Kwa sababu wananchi walijua kwamba mwaka kesho tutaenda kuanza kukitumia hicho chuo. Ninahitaji majibu yako ili kusudi wananchi wa Mbogwe wajue, ahsante sana. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Maganga, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa vyuo hivi 64 vya wilaya pamoja na kile kimoja cha mkoa tunajenga kwa awamu na nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, baada ya kumaliza misingi kuna vifaa ambavyo inabidi tuagize. Tumefanya bulk purchase kutoka viwandani moja kwa moja. Katika zile karakana na majengo yale makubwa yote tunatumia Mfumo wa LGS (Light Gauge Steel), zile ni fabricated metals ambazo zinatoka kiwandani moja kwa moja. Kwa hiyo, unapoona ujenzi umesimama tayari tumesha-press order kwa ajili ya hizo fabricated metals na baada ya muda si mrefu zitakuja na zikishafika pale site ni kazi ya mwezi mmoja tu majengo yale yote yatakuwa tayari yameshanyanyuka.

Kwa hiyo, nikuondoe wasiwasi, kazi hiyo inaendelea, fedha zimeshalipwa kule ALAF na shughuli inaendelea kwa sababu zinakuwa imported. Mara baada ya kufika tutakuja hapo Mbogwe na kukamilisha hiyo kazi. (Makofi)

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Chuo cha Ufundi VETA katika Mji wa Ifakara?

Supplementary Question 3

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Halmashauri ya Moshi ina vijana wengi sana ambao wanahitaji elimu ya ufundi. Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika halmashauri hiyo? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimwia Mwenyekiti, ninaomba nijibu swali dogo la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyokwisha kujibu kwenye maswali ya msingi kwamba kwa sasa baada ya kukamilisha ujenzi wa vile vyuo 25 vya awamu ya kwanza katika wilaya 25 na hivi 64, tutakuwa hatuna wilaya ambayo haina Chuo cha VETA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu kwamba kunawezekana kukawa na umbali wa namna moja au nyingine lakini ninaamini pale Moshi tuna Chuo cha VETA ambacho kiko pale Moshi, ni chuo cha mkoa, lakini vilevile kina-save kama chuo cha wilaya, lakini kwenye zile wilaya nyingine za pembezoni, ukienda Rombo, ukienda Hai, ukienda Siha, kote kule tumejenga Vyuo vya VETA na yale majimbo ambayo hayana vyuo tunakwenda kujenga shule za ufundi ku-complement pale ambapo Chuo cha VETA kimekosekana. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Chuo cha Ufundi VETA katika Mji wa Ifakara?

Supplementary Question 4

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika ni miongoni mwa wilaya ambazo zimeanza ujenzi wa VETA eneo la Wilaya ya Tanganyika, lakini kwa bahati mbaya sana mpaka sasa tunavyozungumza ujenzi umekwama takribani zaidi ya miezi mitano. Ni lini Serikali itapeleka fedha kukamilisha ujenzi wa VETA Wilaya ya Tanganyika?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Kakoso, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali tumeshapeleka fedha na ninaomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, pesa tulizopeleka hizi shilingi milioni 324.6 katika kila site, hizi zimekwenda kwa ajili ya zile local materials, kwa maana ya mchanga, kokoto, mawe, maji, lakini pamoja na gharama za kulipa mafundi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zile materials nyingine zote Wizara inanunua kwa mfumo wa bulk purchase kwa maana ya simenti, nondo, mabati pamoja na zile LGS (Light Gauge Steel) kwa ujumla wake. Kwa hiyo, iwapo kama misingi yote imeshakamilika na maboma yameshanyanyuliwa, tafsiri yake kinachosubiriwa sasa ni vile vifaa kutoka kiwandani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Kakoso, hivi sasa tayari vifaa hivi vimeshaagizwa na mara baada ya kufika tutavipeleka katika kila centre kuhakikisha kwamba majengo hayo yananyanyuka. Lengo letu ifikapo mwezi wa 10 vyuo hivi kwa awamu hii ya kwanza yale majengo tisa yawe yamekamilika ili mwezi wa 11 tuweze kuanza kutoa mafunzo rasmi, ninakushukuru sana. (Makofi)

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Chuo cha Ufundi VETA katika Mji wa Ifakara?

Supplementary Question 5

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza nianze kwa kumshukuru sana Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia fedha shilingi 2,400,000,000 kujenga chuo bora kabisa cha VETA Wilaya ya Ikungi. Sasa hivi tunavyoongea chuo kimeanza kazi chini ya Mkuu wa Chuo Ndugu Mathias Luhanga na wanafunzi wako darasani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninataka niombe tu Mheshimiwa Waziri kwamba kwa ajili ya mambo ya kiutawala chuo chetu kinahitaji usafiri. Ninaomba sana kujua ni lini Serikali itawaletea gari kwa ajili ya kufanya kazi za kiutawala katika Chuo chetu cha VETA Ikungi? Ahsante sana (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nikijibu swali dogo la Mheshimiwa Mtaturu, Mbunge wa Ikungi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwenye vyuo vyetu 25 tuna changamoto ya usafiri lakini nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, safari ni hatua na hatua tumeshaanza, kimsingi kwanza tulianza kujenga yale majengo, lakini baadaye tukajaribu kutafuta watumishi kwa ajili ya mafunzo hayo kuanza na hivi sasa mafunzo yameanza. Tumeanza kupeleka vifaa na hatua inayofuata ni kupeleka sasa vile vyombo saidizi kwa ajili ya kuhakikisha wataalamu wetu, walimu wetu na watumishi wetu wanafanya kazi zao kwa ufanisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi, katika bajeti yetu ijayo tumeweka fungu kwa ajili ya ununuzi wa magari, kwa ajili ya vyuo hivi vya VETA, FDC pamoja na vyuo vyetu vya ualimu. Tunaamini katika utekelezaji wa bajeti ya mwakani mambo hayo yatakwenda kufanyika.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Chuo cha Ufundi VETA katika Mji wa Ifakara?

Supplementary Question 6

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, tunaishukuru Serikali kwa ukarabati mkubwa uliofanywa katika Chuo Tango FDC, Mbulu Mjini, je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kumalizia yale majengo yaliyobaki kukarabatiwa ili chuo kile kiwe na hadhi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nikijibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Zacharia, Mbunge wa Mbulu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli pale Tango tumefanya ukarabati mkubwa na baadhi ya majengo bado hatujakamilisha. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Zacharia, lakini ninakumbuka juzi ulikuja kwenye meza yangu tukalizungumza jambo hili pamoja na suala la kwenda kule Tango na nikakuahidi kwamba tusubiri tukamilishe shughuli za Bunge ili tuweze kwenda kuona hali halisi ilivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nikuondoe wasiwasi, katika Mradi wetu wa EP4R ambao tunataraji kuanza mwaka ujao wa fedha, tuna mpango wa kukarabati majengo yote katika vyuo vyote vya FDC ambavyo bado hatujafanya ukarabati. Kwa hiyo, kama nilivyokwisha kujibu kwenye swali moja la nyongeza hapa la FDC kule Ifakara, basi vilevile na Tango tutakwenda kufanya kama tutakavyofanya Ifakara. (Makofi)

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Chuo cha Ufundi VETA katika Mji wa Ifakara?

Supplementary Question 7

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa nafasi na ninaipongeza Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan chini ya Wizara ya Elimu, Waziri na Naibu Waziri kwa kuanza ujenzi wa Chuo cha VETA ndani ya Wilaya ya Missenyi. Chuo hicho ni matarajio makubwa ya Wana-Missenyi na kimeanza lakini spidi yake kwa kweli hairidhishi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini sasa tutapata vifaa vya ujenzi ili tuweze kwenda kwa speed na tuweze kupata chuo hicho ambacho ni matarajio makubwa kwa Wana-Missenyi? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kyombo, Mbunge wa Missenyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyokwisha kujibu kwenye maswali mengine ikiwemo na hili la Mheshimiwa Kyombo kule Missenyi, sasa hivi tunachosubiri ni vile vifaa ambavyo ni imported materials, zile fabricated metals (LGS) kwa ajili ya majengo yetu yale makubwa, makarakana yale manne yote yale yanahitaji materials hizo, lakini pamoja na bati ambapo nimesema tayari tumesha-press order, tumeshalipa na vifaa hivyo viko njiani kuja. Mara vitakapofika mtashangaa ile speed yetu tutakayokwenda kule, ndani ya mwezi mmoja yale majengo yote na mazingira ya pale yatakuwa yamebadilika kabisa na tunaamini mpaka itakapofika mwezi wa 10, Missenyi tutakuwa tumekamilisha yale majengo makubwa na huduma pale zinaweza kuanza mara moja.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Chuo cha Ufundi VETA katika Mji wa Ifakara?

Supplementary Question 8

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Mheshimiwa Waziri, kwanza niipongeze Serikali kwa ujenzi wa VETA nchi nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu, kutokana na kwamba dunia ya sasa mabadiliko ya teknolojia, maeneo mengi ya VETA ambazo zinajengwa, masomo yanayotolewa ni ya aina ile ile, ufundi ujenzi nyumba, ufundi cherehani na ufundi Seremala lakini soko la vijana nje linahitaji masomo mengine. Ufundi bomba, ufundi umeme wa magari, ufundi umeme wa majumba, lakini mitambo ya gesi kama usambazaji wa gesi unaoendelea nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni upi mkakati wa Wizara, wakati Mheshimiwa Rais anaendelea kujenga VETA nchini, ni upi mkakati wa Wizara kubadilisha syllabus ziendane na soko la sasa ili tuokoe vijana wengi wa Kitanzania wapate fursa hiyo? Ahsante. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la Mheshimiwa Sanga kama ifuatavyo, Mheshimiwa Sanga anatoa ushauri kwa maana ya kubadilisha mtaala, lakini nikuondoe wasiwasi Mheshimiwa Sanga tayari Mheshimiwa Rais alishaliona hilo na alishaagiza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeanza na maboresho makubwa ya mitaala yetu kuanzia shule za msingi, sekondari mpaka vyuo vikuu, lakini Mheshimiwa Rais aliagizwa kwamba, VETA hizi zinazojengwa, basi mitaala yake na masomo yake na kozi zake ziendane na shughuli za kiuchumi za sehemu husika, kwa maana tunakwenda kufanya customization katika vyuo hivi kwa lengo la kuhakikisha kwamba zile shughuli za kiuchumi zinazofanyika katika maeneo hayo ziweze kufundishwa katika vyuo hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, yale maeneo ambayo tunachimba madini tutakuwa na kozi za madini zinafundishwa kwenye vyuo hivi, yale maeneo ambayo tunashughulika na masuala ya uvuvi kutakuwa na kozi za uvuvi zinafundishwa kwenye maeneo haya, kule kwangu nako kimejengwa chuo kama hiki, kuna masuala ya utalii, lakini vilevile masuala ya hospitality yatafundishwa kwenye vyuo hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, lengo letu ni kuhakikisha kwamba tunakwenda kuhakikisha zile shughuli sasa za kiuchumi ndizo zitakazofundishwa, tukiongezea na hizi kozi nyingine za general ambazo kila mmoja wetu anapaswa kuzifahamu ili hata bomba likikatika pale nyumbani kwako huna haja ya kutafyta fundi, wewe mwenyewe unaweza kurekebisha kwa namna moja au nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, huo ndiyo mpango wa Serikali. Mheshimiwa Rais ameshatoa agizo na sisi kama Wizara ni lazima tutekeleze kwa kadri maagizo yalivyotolewa.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Chuo cha Ufundi VETA katika Mji wa Ifakara?

Supplementary Question 9

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Chuo cha VETA kilichopo Manispaa ya Shinyanga ni chuo kongwe na kinahitaji ukarabati wa miundombinu. Ni upi mpango wa Serikali kukarabati Chuo cha VETA Manispaa ya Shinyanga? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nikijibu swali dogo la Mheshimiwa Dkt. Mnzava, ni kweli tuna vyuo vyetu, baadhi ya vyuo vyetu vya mikoa ni vya muda mrefu, majengo yake ni chakavu na miundombinu mingine ni chakavu, hata vifaa vilivyokuwa vinatumika ni vile vya muda mrefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Dkt. Mnzava, tuna miradi mbalimbali ambayo tumeshafanya maandiko yake na maandiko hayo yatakapokamilika na miradi hii kuanza tutakwenda kufanya ukarabati kwenye vyuo vyetu vyote kongwe kikiwemo na hiki Chuo cha Mkoa wa Shinyanga. (Makofi)

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Chuo cha Ufundi VETA katika Mji wa Ifakara?

Supplementary Question 10

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwamba katika Kata ya Mwika Kaskazini kwenye Jimbo langu la Vunjo kwenye Shule ya Msingi ya Lole kuna Chuo cha VETA ambacho kimetelekezwa kutoka mwaka 2000. Majengo yamechakaa, lakini kuna baadhi ya tools za kutumia kufundishia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kinachohitajika pale ni kukarabati yale majengo na kupata walimu wa kufundisha, basi pamoja na kuongeza hasa hivyo vifaa vya kufundishia. Je, ni lini Serikali itachukua hatua?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii sijui ni mara yangu ya tatu ninauliza swali hili, lakini nimeona nirudie kwa sababu wale wananchi wanateseka sana. Jimbo la Vunjo liko pacha na Jimbo la Moshi Vijijini kwenye halmashauri moja. Kwa hiyo, kuna disadvantages nyingi sana ambazo tunapata kwenye ku-allocate hizi facilities. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nikijibu swali dogo la Mheshimiwa Dkt. Kimei ni kuwa jambo hili ulilolizungumza ninaomba tu tutoe maagizo kwa Mkurugenzi wetu wa VETA, kwanza kwenda kuona hilo eneo, lakini Mheshimiwa Dkt. Kimei kama utaridhia ninadhani ni muhimu na sisi tukaenda tukaona, wazungu wanasema; “the seeing is believing.” (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninadhani kuna umuhimu wa kupanga ratiba na sisi wenyewe kama Wizara, mimi binafsi niende nikaone tuweze kufanya tathmini ya kina ili tuweze kujua kitu gani, measures zipi tuweze kuchukua ili kama ni chuo ambacho kimeshakabidhiwa kwenye Wizara, basi tufanye ukarabati kama ulivyoshauri. Tupeleke vifaa pamoja na walimu ili mafunzo hapo yaanze kutolewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuanzia tunaomba tumwagize Mkurugenzi wa VETA aweze kwenda eneo hilo kwa haraka na sisi tukimaliza Bunge hapa tutakwenda. Mheshimiwa Dkt. Kimei tutapanga na nitakuja hapo kwako tupange ratiba ya kwenda huko haraka iwezekanavyo. (Makofi)

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Chuo cha Ufundi VETA katika Mji wa Ifakara?

Supplementary Question 11

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Wilaya ya Manyoni ina majimbo mawili. VETA inayoendelea kujengwa katika Manyoni iko katika Jimbo la Manyoni Mashariki. Unawaambiaje watu wa jimbo langu eneo la Itigi kuhusu ujenzi wa shule ambayo mmeitaja? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nikijibu swali dogo la Mheshimiwa Massare ni kwamba Mheshimiwa Massare anajua na tulishazungumza suala hili na alikuja ofisini na akaangalia orodha ya shule zitakazokwenda kujengwa za ufundi na Wilaya ya Manyoni, ilikuwa Manyoni imekosewa, Manyoni Kaskazini na Manyoni Kusini tukarekebisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Massare, shule yake ya Ufundi ipo, tumeshafanya marekebisho mwanzoni kulikuwa na typing error. Shule ile itakwenda kujengwa katika jimbo lake kama vile alivyoshauri yeye mwenyewe na kazi hii itaanza Julai mwaka ujao wa fedha. (Makofi)