Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Mbinga Mpepai hadi Mtua kwa kiwango cha changarawe?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza naishukuru Serikali kwa kutenga shilingi milioni 947.2 kujenga kilometa 31. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza. Katika majibu ya Serikali ni kwamba, kilometa mbili zitajengwa kwa kiwango cha lami kupitia Mradi wa TACTIC. Nataka nifahamu, ni lini mradi huo utaanza kutekelezwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Ni lini Serikali itajenga Barabara ya Mbinga – Kikolo – Kihungu na barabara ya Mbinga – Kitanda hadi Miembeni?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tayari hatua zote za muhimu zimekamilika kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, mradi huu sasa utaanza kutekeleza ujenzi wa barabara hiyo ya lami ya kilomita mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili ambalo ameuliza juu ya ujenzi wa Barabara ya Mbinga Mjini – Kikolo mpaka Kihungu yenye urefu wa kilometa 30, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, katika mwaka wa fedha 2024/2025 zimetengwa shilingi milioni 60 kwa ajili ya kufanya marekebisho ya barabara hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kitanda ambayo yenyewe ina kilometa 28, kwenye mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali ilitenga kwenye bajeti shilingi milioni 80, lakini katika mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali imetenga shilingi milioni 47.18 kwa ajili ya marekebisho. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imelichukua suala hili la ujenzi wa barabara hizi kwa umakini mkubwa na itaendelea kutekeleza ujenzi huo.