Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Je, majosho mangapi yatajengwa katika Halmashauri ya Itigi katika Mwaka huu wa Fedha?

Supplementary Question 1

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Serikali, ninaomba nijue kuhusu majosho Mbogwe; mwaka jana yalikuwepo kwenye bajeti na hata mwaka huu yapo. Ni lini sasa utekelezaji wake utafanywa ili majosho hayo ya Mbogwe yakamilike? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Maganga. Mbogwe itakuwa miongoni mwa majosho yanayowekwa kwenye mpango wa bajeti ya 2025/2026. Mheshimiwa Mbunge, tuwe na subira kidogo tu, tutapata mahitaji haya.

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Je, majosho mangapi yatajengwa katika Halmashauri ya Itigi katika Mwaka huu wa Fedha?

Supplementary Question 2

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Spika, ninashukuru. Jimbo la Igunga ni moja ya majimbo yenye mifugo mingi sana nchini. Je, ni lini Serikali itaanza kujenga majosho kwenye Kata za Mwamashiga, Mwamashimba na Mwamakona? Ahsante.

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kama nilivyolieleza Bunge lako Tukufu katika swali la msingi ni kwamba tumeweka katika Mpango wa Bajeti inayokuja ya mwaka 2025/2026 kuendeleza ujenzi wa majosho yote hapa nchini yakiwepo majosho ya Mheshimiwa Ngassa kule Igunga.

Name

Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:- Je, majosho mangapi yatajengwa katika Halmashauri ya Itigi katika Mwaka huu wa Fedha?

Supplementary Question 3

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru. Ni lini Serikali itaanza ujenzi wa majosho manne ambayo yamekuwa yakitokea kila mwaka wa bajeti ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Chemba? (Makofi)

Name

Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kama nilivyojieleza kwenye jibu langu la msingi, tunaliweka kwenye makadirio ya fedha ya kipindi cha 2025/2026 ambapo tunakwenda kujenga majosho mengi kwa nchi nzima na jimbo la Chemba litakuwa sehemu ya mradi huo. (Makofi)