Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, upi mkakati wa Serikali kuhakikisha Mradi wa Magadi Soda wa Engaruka unakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na ninashukuru kwa majibu ya Serikali. Mradi huu wa Magadi Soda wa Engaruka ni moja kati miradi ya kimkakati na ni mradi muhimu sana kwa ajili ya kutuongezea ajira pamoja na fedha za kigeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa taarifa zilizopo, wawekezaji wengi wanavutiwa kuwekeza kwenye mradi huu lakini changamoto kubwa ni ukosefu wa miundombinu sahihi inayoelekea kwenye mradi; Barabara ya Selela – Engaruka ni mbovu sana lakini hakuna maji wala umeme wa uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni upi mkakati wa Serikali sasa kuhakikisha Wizara hizi zinasomana ili miundombinu hii iweze kujengwa kwa haraka? Ahsante.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana, kwanza, ninachukua nafasi hii pia kumpongeza sana Mheshimiwa Zaytun Swai kwa kuendelea kufuatilia mradi huu muhimu sana. Kama alivyosema mwenyewe, kweli ni wa kimkakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutekeleza hii miradi ya kimkakati kama ambavyo alianza kwenye ule Mradi wa Liganga na Mchuchuma na sasa tunaenda kutekeleza Mradi huu wa Magadi Soda kwa sababu mradi huu unasaidia ukuaji wa viwanda vingi na utekelezaji wa mkakati ule mkubwa unganishi wa Maendeleo na Viwanda (Integrated Industrial Development Strategy).

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa katika mkakati huu mkubwa, moja ya mradi ni huu wa Magadi Soda. Kama nilivyosema, tumeshaanza kwanza kulipa fidia na kutoa elimu kwa wananchi ili kupisha mradi. Zaidi sasa nimesema kwenye jibu langu la msingi, tunachoenda kufanya sasa ni kuanza kuweka bajeti ya kuweka miundombinu wenzeshi ikiwemo hii ambayo Mheshimiwa Mbunge ametaja; barabara, maji, umeme na mambo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu mradi huu ili utekelezwe ni lazima haya yote yakamilike. Kwa hiyo, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wake na nia njema ya Mheshimiwa Rais wetu mpendwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, tunaenda kutekeleza mradi huu kama ambavyo tumeanza kutekeleza miradi mingine ili isaidie kupunguza uagizaji wa bidhaa au malighafi hii ambayo inatumika kwenye viwanda vingi ikiwemo viwanda vya vioo, sabuni, rangi, karatasi, kusafisha mafuta ya petroli na kadhalika, ambayo tunatumia fedha nyingi sana za kigeni kuagiza kutoka nje wakati tunayo hapa ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana.

Name

Abdi Hija Mkasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Micheweni

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, upi mkakati wa Serikali kuhakikisha Mradi wa Magadi Soda wa Engaruka unakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukiboresha Kituo cha TEHAMA kilichopo Wilaya ya Micheweni?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) ilitekeleza mradi wa ujenzi wa vituo 11 vya TEHAMA, Unguja na Pemba ambapo kwa kila wilaya kimejengwa kituo kimoja kwa madhumuni ya kuwapa fursa wananchi wa Zanzibar kujifunza na kutumia TEHAMA kwa ajili ya manufaa yao wenyewe ili kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kiutamaduni. Kituo cha TEHAMA Sokoni kilichopo Wilaya ya Micheweni ni miongoni mwa vituo hivyo ambapo kinaendelea kutoa huduma kama ilivyokusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mheshimiwa Mbunge ameuliza swali kuhusu kukiboresha kituo husika kilichopo katika Wilaya ya Micheweni, inaashiria kuwa ipo changamoto. Hivyo, Wizara kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi itafanya tathmini ili kujua mahitaji halisi ya kituo hicho kwa lengo la kufanya maboresho yanayohitajika. (Makofi)

Name

Abdi Hija Mkasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Micheweni

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, upi mkakati wa Serikali kuhakikisha Mradi wa Magadi Soda wa Engaruka unakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. ABDI HIJA MKASHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza (a) na (b) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Serikali imekiri kuwepo kwa changamoto katika kituo kile; je, ni lini itaharakisha kwenda kufanya tathmini hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa katika kituo kile kuna vijana ambao wanajitolea, je, Serikali ipo tayari kuwafanyia mpango angalau wa kupata posho ya kuweza kujikimu? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza, ninampongeza sana Mheshimiwa Abdi Mkasha kwa kufuatilia maslahi ya vijana ambao wako pale tayari wanafanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi, tayari sisi kama Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa Tanzania Bara tulishafanya sehemu yetu kupitia UCSAF na tayari tumeshakabidhi kwenye Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara hii ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi. Hivyo, ninapenda tu kukwambia kwa sababu tunafanya kwa ushirikiano basi nitawasiliana na wewe na kuona namna njema ya kukukabidhi kwa wenzetu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ili waweze kufanya haya wote mawili; kuharakisha katika maboresho, lakini vilevile kuangalia maslahi ya vijana. (Makofi)

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, upi mkakati wa Serikali kuhakikisha Mradi wa Magadi Soda wa Engaruka unakamilika?

Supplementary Question 4

MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa kuwa kituo hiki wamekuwepo vijana na wamejitolea kwa muda mrefu na kwa kuongeza kasi ya kuwapatia vijana mafunzo na kuzingatia maendeleo makubwa ya teknolojia, je, Serikali ya SMZ pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haioni haja ya kukaa pamoja kuwapatia ajira za moja kwa moja hawa vijana ili kuwapa moyo wa kufanya kazi kwa bidii zaidi? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na ninashukuru sana kwa swali zuri ambalo linaendelea kukazia maslahi ya vijana kuona sasa wanapata ajira. Tunafahamu taratibu za ajira za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zilivyo na sisi kama Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tuna Sekretarieti ya Ajira na tuna Wizara ya Utumishi, lakini haya yote kwa sababu tayari wako ndani, vigezo na masharti vitazingatiwa kuona namna gani wanaweza kupatiwa ajira. (Makofi)

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, upi mkakati wa Serikali kuhakikisha Mradi wa Magadi Soda wa Engaruka unakamilika?

Supplementary Question 5

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwenye Tarafa ya Nakopi, Kata ya Napacho, Kampuni ya Minara Tanzania ilipewa kazi ya kusimika minara katika eneo hilo, jambo ambalo sasa ni mwaka mmoja huo mnara haujasimikwa. Changamoto kubwa ni mawasiliano ya kufika katika eneo ambalo mnara unatakiwa kujengwa.

Je, Serikali iko tayari kuisaidia hii Kampuni ya Minara Tanzania wakatengeneza miundombinu ya barabara ili waweze kufika katika eneo ambalo limekusudiwa kujengwa mnara huo? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahya kuhusu barabara ya kufika katika maeneo ya ujenzi wa minara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Wizara tayari tumeshafanya mawasiliano na wenzetu wa TAMISEMI kuona TARURA inaweza kuingilia kati na kuona namna njema ya kusaidiana na hawa watoa huduma ili waweze kutengenezewa barabara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia wakati mwingine wananchi wanaweza wakatoa nguvu kazi kama inawezekana kulingana na jiografia ili kuona minara hii inajengwa na maeneo hayo yanaweza kupitika.