Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prosper Joseph Mbena

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:- Wananchi wa Wilaya ya Morogoro Vijijini kwa muda mrefu wamekuwa wakikosa huduma nzuri za matibabu katika hospitali ya Wilaya kama vile X-Ray, MRI, TSCAN dawa za kutosha, Madaktari Bingwa na Wauguzi kwa sababu tu Wilaya na Halmashauri yake zimechelewa kuhamia Mvuha suala ambalo Ofisi ya Rais, TAMISEMI inalishughulikia:- (a) Je, Serikali itakuwa tayari kuanza kujenga Hospitali ya Wilaya Mvuha mahali ambapo ndipo patakapojengwa Makao Makuu ya Wilaya? (b) Je, Serikali kwa sasa iko tayari kukiteua Kituo cha Afya cha Lukange ambacho ni bora sana kimejengwa na Kanisa Katoliki na kukikabidhi kitoe huduma kwa wananchi kama Hospitali Teule ya Wilaya ya Morogoro Kusini?

Supplementary Question 1

MHE. PROSPER J. MBENA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi hii ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na napenda kumpa taarifa kwamba tayari vikao hivyo vimeshafanyika na tayari mkataba kati ya Kanisa Katoliki pamoja na Halmashauri ya Wilaya Morogoro umeshakamilika na nitampatia nakala ya mkataba huo. Baada ya hatua hiyo kufikiwa. Je, Mheshimiwa Waziri sasa atashughulikia lini? Itachukua muda gani kushughulikia suala la kupatikana kwa watumishi pamoja na kada nyingine zinahitajiwa kwa hospitali hiyo? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu kama mchakato huu tayari umeshaanza, basi ina maana kwamba walikuwa mbele ya tukio zaidi. Kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni jukumu la Serikali sasa kwamba mara baada ya mchakato huo kukamilika, sasa ni kuangalia kipi kinachohitajika katika eneo lile hasa tukitoa kipaumbele katika suala zima la watumishi kama alivyozungumza. Kuhusu lini, naomba niseme ni katika kipindi kifupi kijacho. Kwa kuwa lengo letu kubwa ni kuhakikisha kwamba tunaongeza kada katika maeneo mbalimbali, basi Wilaya yake tutaipa kipaumbele hasa katika eneo hili ambapo nami nilifika kule katika Wilaya yake nikaona kwamba ni kweli, wananchi wanaotoka kule Mvuha mpaka kuja Morogoro Mjini ni kilomita nyingi zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tuna kila sababu ya kuiwezesha hospitali hii. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni commitment ya Serikali kuwezesha kituo kile katika vifaa tiba na wataalam. Lengo kubwa ni kwamba wananchi wa eneo lile wapate huduma.

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:- Wananchi wa Wilaya ya Morogoro Vijijini kwa muda mrefu wamekuwa wakikosa huduma nzuri za matibabu katika hospitali ya Wilaya kama vile X-Ray, MRI, TSCAN dawa za kutosha, Madaktari Bingwa na Wauguzi kwa sababu tu Wilaya na Halmashauri yake zimechelewa kuhamia Mvuha suala ambalo Ofisi ya Rais, TAMISEMI inalishughulikia:- (a) Je, Serikali itakuwa tayari kuanza kujenga Hospitali ya Wilaya Mvuha mahali ambapo ndipo patakapojengwa Makao Makuu ya Wilaya? (b) Je, Serikali kwa sasa iko tayari kukiteua Kituo cha Afya cha Lukange ambacho ni bora sana kimejengwa na Kanisa Katoliki na kukikabidhi kitoe huduma kwa wananchi kama Hospitali Teule ya Wilaya ya Morogoro Kusini?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Changamoto za Morogoro Kusini zinafanana na Changamoto za Jimbo la Karagwe. Katika Hospitali ya DDH Nyakahanga tuna tatizo kubwa la upungufu wa madawa, vifaa tiba na Wauguzi.
Mheshimiwa Naibu Spka, swali langu ni je, Naibu Waziri, Mheshimiwa Jafo kaka yangu, anaweza kuambatana nami baada ya Bunge hili kwenda kusaidiana nami kutatua changamoto za Hospitali ya DDH ya Nyakahanga
pamoja na kuanza mchakato wa kujenga Hospitali ya Wilaya ukizingatia DDH ya Nyakahanga inahudumia Wilaya mbili; Karagwe na Kyerwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri wazi kwamba miongoni mwa Wabunge ambao walikuwa wakinisumbua sana katika Sekta ya Afya ni Mbunge huyu wa Karagwe. Ni kweli kabisa, naomba niseme kuwa, pale ana Daktari wake anaitwa Dkt. Sobo ambaye ni kijana mwenzake; naamini kwamba watashirikiana vya kutosha kuhakikisha mchakato wa Jimbo lile unakaa vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, commitment yetu ni kwamba, katika kipindi hiki nitakuwa na ziara katika Mikoa yetu mitano nikianzia Mkoa wa Tanga, Lindi, Pwani Morogoro pamoja na Mtwara, lakini nitapita Ruvuma. Vile vile Mkoa wa Kagera niliupa kipaumbele kwa zoezi maalum katika kutembelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni imani kwamba kabla ya Bunge lijalo, basi nitajitahidi kwa kadiri iwezekanavyo tufike eneo lile kubaini changamoto za wananchi wa eneo lile la Jimbo la Karagwe ili mwisho wa siku wananchi wa eneo lile waweze kupata huduma bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni commitment ya Serikali, tutajitahidi kwa kadiri iwezekanavyo, hasa nikijua nawe ni mpiganaji mkubwa katika Sekta ya Afya katika eneo lako, tutasukuma kwa kadiri iwezekanavyo wananchi pale wapate huduma bora.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:- Wananchi wa Wilaya ya Morogoro Vijijini kwa muda mrefu wamekuwa wakikosa huduma nzuri za matibabu katika hospitali ya Wilaya kama vile X-Ray, MRI, TSCAN dawa za kutosha, Madaktari Bingwa na Wauguzi kwa sababu tu Wilaya na Halmashauri yake zimechelewa kuhamia Mvuha suala ambalo Ofisi ya Rais, TAMISEMI inalishughulikia:- (a) Je, Serikali itakuwa tayari kuanza kujenga Hospitali ya Wilaya Mvuha mahali ambapo ndipo patakapojengwa Makao Makuu ya Wilaya? (b) Je, Serikali kwa sasa iko tayari kukiteua Kituo cha Afya cha Lukange ambacho ni bora sana kimejengwa na Kanisa Katoliki na kukikabidhi kitoe huduma kwa wananchi kama Hospitali Teule ya Wilaya ya Morogoro Kusini?

Supplementary Question 3

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Miongoni mwa matatizo ambayo tunayapata katika Wilaya ya Babati kwa Hospitali ya Mrara ni ranking ya hospitali hiyo ambapo mpaka sasa inaitwa Kituo cha Afya wakati hospitali hiyo imekuwa ikihudumia watu wa Kondoa na watu wa Babati Vijijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, mara nyingi tumekuwa tukipendekeza kwamba hospitali hii tuipandishe rank iwe Hospitali Teule ya Wilaya, lakini Serikali imekuwa haitupi ushirikiano. Je, sasa wako tayari kutusaidia ili hospitali hiyo ipate dawa na vifaa tiba kuhudumia watu wote hao?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Gekul kwamba Serikali lazima inatoa kipaumbele na ndiyo maana naye anakumbuka juzi juzi tulikuwa pamoja jimboni kwake tukikagua miradi mbalimbali katika Mkoa wa Manyara. Nimeweza kubaini changamoto mbalimbali kimkoa, kiujumla wake kwamba kuna mambo mengi ya kuweka kipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama jambo hili lililetwa kama request Serikalini, lakini bado halijafanyiwa kazi, sasa ni jukumu letu kukumbushana tuone jinsi gani tutafanya ili pale ambapo pamepungua tusukume kwa sababu mwisho wa siku tunataka wananchi wapate huduma.
Kwa hiyo, ni commitment ya Serikali kwamba tutaangalia ni kitu gani kilichokuwa kinakwamisha mwanzo, jambo gani (gap) ambalo inabidi tuliweke vizuri ili tuboreshe eneo na mwisho wa siku wananchi wapate huduma ya afya, kwani ni commitment ya Serikali kuwahudumia wananchi wake.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:- Wananchi wa Wilaya ya Morogoro Vijijini kwa muda mrefu wamekuwa wakikosa huduma nzuri za matibabu katika hospitali ya Wilaya kama vile X-Ray, MRI, TSCAN dawa za kutosha, Madaktari Bingwa na Wauguzi kwa sababu tu Wilaya na Halmashauri yake zimechelewa kuhamia Mvuha suala ambalo Ofisi ya Rais, TAMISEMI inalishughulikia:- (a) Je, Serikali itakuwa tayari kuanza kujenga Hospitali ya Wilaya Mvuha mahali ambapo ndipo patakapojengwa Makao Makuu ya Wilaya? (b) Je, Serikali kwa sasa iko tayari kukiteua Kituo cha Afya cha Lukange ambacho ni bora sana kimejengwa na Kanisa Katoliki na kukikabidhi kitoe huduma kwa wananchi kama Hospitali Teule ya Wilaya ya Morogoro Kusini?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii. Naomba kuuliza swali la nyongeza. Nashukuru sana kwa majibu ya Naibu Waziri kwa swali la msingi, lakini ningependa kuuliza kuwa kwa sababu Morogoro Vijijini hatuna mpaka sasa hivi Hospitali ya Wilaya na majibu yametolewa, naomba kuulizia je, inawezekana pia kuboresha Kituo cha Afya cha Dutumi ambacho mpaka sasa hivi na chenyewe kinatumika kwa kutupatia vitendea kazi? Ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Ishengoma ni Mbunge wa Viti Maalum kule na nimesema kwamba katika ziara yangu nina mpango wa kuja Mkoa wetu wa Morogoro. Lengo ni kutembelea Mkoa mzima wa Morogoro na kubaini changamoto zake.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Ishengoma najua ni mpiganaji wa siku nyingi sana katika eneo hili. Naomba nimhakikishie kwamba katika ziara yangu eneo hili tutakwenda kulitembelea na licha ya kulitembelea na kuangalia mipango ya pamoja jinsi tutakavyofanya, lakini nina maslahi mapana ya Mkoa wa Morogoro kwa sababu najua mkoa ule wananchi wanapata shida, wanatembea mbali, siyo jambo la kufichaficha.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuna kila sababu, kipindi cha ziara yangu tufike eneo hilo, tushauriane kwa pamoja na linalotakiwa kufanywa kwa sasa tutalifanya, lakini linalotakiwa kuwekewa mipango mbadala kwa siku za usoni, tutalijadili kwa pamoja. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Ishengoma kwamba, katika hilo tutashirikiana kwa pamoja Mheshimiwa wangu.