Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY (k.n.y. MHE. HAJI KHATIB KAI) aliuliza:- Arusha International Conference Center ni miongoni mwa taasisi ya iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kuvunjika kwa Jumuiya hiyo mwaka 1977, hivyo hii inaonyesha kwamba taasisi hiyo ina sura ya Muungano. Je, ni kwa nini taasisi hii haionyeshi ushiriki wa Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa hiki ni kituo cha pamoja au cha ubia kama ambavyo ingepaswa kuonekana wazi wazi katika taasisi mbalimbali za Muungano. Swali langu linakuja, je, Naibu Waziri anaweza kutuambia pamoja na kueleza kwamba nafasi za ushindani kuna Wazanzibari wangapi walioajiriwa katika taasisi hiyo? (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba vituo hivi ni pamoja na kufanya biashara na biashara huwa na faida na hasara. Je, Zanzibar imewahi kupata mgao wake wa faida japo nyama ya sungura ya 4.5%?

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kwamba kuna Wazanzibari wangapi wameajiriwa katika kituo hicho nimekwisha sema kwamba kwa uelewa wangu mpaka sasa hivi sijaona kama kuna Mzanzibari ambaye ameajiriwa maana yake nimesema kwamba ajira zinatolewa na watu wanatakiwa kuchangamkia fursa hizo na kama wana uwezo na capacity na wanaofanyiwa interview wakishinda basi wataajiriwa. Lakini pia tunawahamasisha zinapotokea fursa na nafasi zinapotangazwa basi watu kutoka Zanzibar waombe nafasi hizo. Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu suala la pili ambalo Mheshimiwa Mbunge ameliuliza kwamba kituo kinafanya biashara, je, Zanzibar imepata gawio kiasi gani katika miaka yote hiyo. Kama anavyofahamu kwamba kama hii ni taasisi ya Muungano tunajua kwamba gawio huwa linakwenda katika Mfuko Mkuu wa Serikali kwa hiyo, kutokana na huo Mfuko Mkuu wa Serikali kwa ujumla wake wanapata lile gawio kutokana na Sheria inavyotutaka. Ahsante.

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, naomba kuongezea na hasa kile kipengele cha pili kuhusu gawio. AICC haijawahi kupata gawio na hivi sasa Joint Finance Commission na Ofisi ya Msajili wa Hazina wameunda kikosi kazi ambacho kitachambua na kukisaidia kile kituo ili kiweze kupata faida na kuleta gawio Serikalini kuanzia mwaka ujao wa fedha.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY (k.n.y. MHE. HAJI KHATIB KAI) aliuliza:- Arusha International Conference Center ni miongoni mwa taasisi ya iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kuvunjika kwa Jumuiya hiyo mwaka 1977, hivyo hii inaonyesha kwamba taasisi hiyo ina sura ya Muungano. Je, ni kwa nini taasisi hii haionyeshi ushiriki wa Zanzibar?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa suala hili linahusu Jumuiya ya Afrika Mashariki, nilitaka kujua je, wastaafu wa Afrika Mashariki wa nchi nyingine walishalipwa lakini Tanzania imekuwa inasuasua na kuna sintofahamu wakati ambapo wengine wanasema wameshalipwa, bado tunatambua kuna wastaafu wengi wa Tanzania hawajalipwa. Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nataka tamko la Serikali, je, wastaafu hao ni kweli wamelipwa wote na kama bado kuna mkakati gani wa kuhakikisha kwamba wastaafu wao au warithi wao wanapata fedha zao? Ahsante.

Name

Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, wastaafu hao wamelipwa na kama kuna madai zaidi wayawasilishe Serikalini tutayashughulikia kwa mujibu wa taratibu.

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY (k.n.y. MHE. HAJI KHATIB KAI) aliuliza:- Arusha International Conference Center ni miongoni mwa taasisi ya iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kuvunjika kwa Jumuiya hiyo mwaka 1977, hivyo hii inaonyesha kwamba taasisi hiyo ina sura ya Muungano. Je, ni kwa nini taasisi hii haionyeshi ushiriki wa Zanzibar?

Supplementary Question 3

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa majengo haya ya Arusha International Conference Center (AICC) yalikuwa yakitumiwa na Mahakama ya Kimataifa (ICTR) na kwa hivi sasa Mahakama hii ina majengo yake na imehama katika majengo haya ya AICC. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba heshima iliyokuwepo kwa majengo haya inaendelea kuwepo kwasababu hivi sasa wapangaji wakubwa hao wamekwishahama?

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Amina Mollel kwa swali lake la nyongeza kwamba Serikali tutahakikisha majengo haya yanasimamiwa vizuri na kuhakikisha hayaharibiki. Mheshimiwa Mwenyekiti, kama jana Mheshimiwa Amina Mollel ulisikiliza vizuri kwenye taarifa ya Kamati ya Uwekezaji ya Mashirika ya Umma jana kituo kinafanya kila inachoweza kuhakikisha kinapata watu ambao wanaweza kuja kupanga katika ofisi zile na sisi kama Wizara tutahakikisha tunafuatilia hilo ili kuhakikisha majengo hayaharibiki na yanabaki katika kiwango kinachotakiwa.