Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Primary Question

MHE. KAPT. (MST.) GEORGE H. MKUCHIKA Aliuliza:- Serikali iliwaahidi wananchi wa Mikoa ya Mtwara na Lindi umeme wa uhakika na wa kutosha baada ya kugundulika kwa gesi na baada ya neema ya muda mfupi hivi sasa kuna tatizo kubwa la kukatika kwa umeme mara kwa mara katika Mikoa hiyo ikiwemo na Wilaya ya Newala. Je, tatizo ni nini na Serikali inachukua hatua gani kumaliza kabisa tatizo hili?

Supplementary Question 1

MHE. KAPT. (MST.) GEORGE H. MKUCHIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kushukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Napenda kuipongeza Serikali kwa kusambaza umeme (REA II) vijiji karibu Tarafa zote sita za Wilaya ya Newala. Hata hivyo, nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, majibu ya Mheshimiwa
Naibu Waziri yanaonesha kwamba tatizo la umeme maeneo ya Mtwara Mjini, Lindi yataisha na tumeshuhudia juzi Rais ameweka jiwe la msingi, lakini upande mwingine Naibu Waziri
anakubali kwamba Wilaya za Tandahimba, Newala, Masasi, Nanyumbu, Nachingwea na Ruangwa hali ya upatikanaji wa umeme si nzuri na kule tatizo si kwamba umeme haupo tatizo
ni miundombinu. Nyaya zimekatika, ikinyesha mvua nguzo imeanguka, ni lini Serikali itachukua hatua madhubuti kuhakikisha kwamba kukatikakatika kwa umeme na kuanguka nguzo kuna malizwa mara moja ili Wilaya hizi nazo
zifaidi umeme kama wanavyofaidi Wilaya zingine?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili,
pamekuwepo na matamshi mengi upande wa Serikali juu ya gharama halisi za mwananchi wa kawaida kuingiza umeme katika nyumba yake. Nini kauli ya leo ya Serikali kwamba kijiji fulani kinataka kuingiza umeme pale Newala, yule mwananchi wa kawaida anatakiwa alipe shilingi ngapi kwa sababu matamko ya huko nyuma hayafanani na gharama halisi ambazo zimekuwa zikilipwa? Nakushukuru.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Mkuchika jinsi ambavyo anashughulikia maslahi ya umeme ya wananchi wa Newala Mjini, nampongeza sana. Lakini
pamoja na hayo, Mheshimiwa Mkuchika niseme tu maana hapa tutakaa tutajadiliana zaidi kwa sababu najua unafuatilia mambo yao sana na sisi kama Serikali tusingekuwa tayari kukuangusha, kwa hiyo, tunakuomba sana uendelee kutupa ushirikiano.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusiana na maswali yake mawili ya nyongeza; la kwanza kabisa, ni lini Serikali sasa itachukua hatua za kutatua tatizo la kukatikakatika kwa umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imechukua hatua zifuatazo katika maeneo hasaa ya Mtwara na Lindi na maeneo mengine. La kwanza kabisa, Serikali sasa inajenga miundombinu ya kusafirisha umeme, ule mkuwa kutoka Mtwara na kurekebisha miundombinu iliyoharibika hapa
ambayo tumesema ya urefu wa kilometa 2016. Njia za miundombinu kutoka Mtwara hadi Newala, Tandahimba na maeneo mengine ilikuwa ni ndefu sana, kwa hiyo, hatua ya kwanza Serikali inaanza kujenga transmission line ya umbali wa kilometa 80 ambayo itakamilika mwezi Mei mwaka huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hatua ya pili inajenga kituo cha kupoza umeme kitakachokuwa Mnazi Mmoja maeneo ya Lindi ambacho kitahudumia sana maeneo yote ya Newala, Tandahimba na maeneo mengine ili kupunguza
tatizo la kukatika kwa umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo lingine ni
kwamba inarekebisha pia mashine ambazo zilikuwa mbovu kama nilivyoeleza na kununua nyingine mpya ili kufikia mahitaji halisi ambayo ni megawati 30 kwa wananchi wa Mtwara na Lindi na Wilaya zake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na gharama za umeme. Gharama za umeme kwa manufaa ya wananchi wote ningependa niseme ifuatavyo; kwa vijijni kupitia mradi kabambe wa REA gharama za umeme za kuunganisha kwa wananchi ni shilingi 27,000/= tu basi hakuna gharama nyingine. Ningependa lieleweke hili ili kusudi wananchi
wengine wasibambikiziwe bei. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sambamba na hilo, zipo gharama za kutandaza nyaya kwenye nyumba. Hizo ni gharama zinaotegemea na ukubwa wa nyumba lakini pia zinategemea na mkandarasi waliokumbana nae. Tunachofanya kudhibiti hilo ni kuhakikisha sasa wakandarasi wote wanaounganisha nyaya kwenye numba za wateja sharti la kwanza lazima waidhinishwe na TANESCO na majina yao yabandikwe katika Ofisi za TANESCO ili ikitokea ulaghai tuweze kuwafuatilia. Hizo ni gharama za vijijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini upo mpango
mwingine kwa wananchi wa kawaida ambao nyumba zao zina chumba kimoja hadi vinne. Tunawaptia chombo kinachoitwa UMETA yaani maana yake Umeme Tayari Ukikiweka. Gharama yake ni shilingi 36,000. Kwa hiyo, nataka kuweka wazi kuhusu gharama kijijini. Lakini gharama halisi kwa maeneo ya mijini kwa umbali usiozidi nguzo moja ni shilingi 177,000/= na kwa mijini ni shilingi 320,000/=.
Mheshimiwa Naibu Spika, haya ni mambo muhimu ningependa kuyafafanua, lakini pia mambo mengine inategemea sasa na mambo ambayo mteja pia anahitaji. Ahsante sana.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. KAPT. (MST.) GEORGE H. MKUCHIKA Aliuliza:- Serikali iliwaahidi wananchi wa Mikoa ya Mtwara na Lindi umeme wa uhakika na wa kutosha baada ya kugundulika kwa gesi na baada ya neema ya muda mfupi hivi sasa kuna tatizo kubwa la kukatika kwa umeme mara kwa mara katika Mikoa hiyo ikiwemo na Wilaya ya Newala. Je, tatizo ni nini na Serikali inachukua hatua gani kumaliza kabisa tatizo hili?

Supplementary Question 2

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika,
nashukuru na mimi kunipa nafasi niulize nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali inafanya kazi nzuri ya kuwapelekea umeme wananchi katika nchi yetu; na kwa kuwa kipindi kilichopita Serikali kwenye Jimbo la Makambako hususan vijiji vya Ikwete, Nyamande, Manga, Utengule, Mlowa, Mahongole, Kitandililo na Kifumbe iliahidi kutuletea umeme katika Awamu ya Pili na mkandarasi ambaye tulikuwa tumepewa alikuwa ni LAC Export na mkandarasi huyu baadae Serikali kupitia Bunge hili walisema
wamemuondoa kwa sababu alikuwa hakidhi vigezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini sasa Serikali
itatupeleka katika vijiji hivi nilivyovitamka umeme Awamu hii ya Tatu ili wananchi hawa waweze kupata umeme kama ambavyo wanapata sehemu zingine? Nakushukuru.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nikubaliane na Mheshimiwa Sanga na nampongeza, kweli nilipomtembelea alinipa
ushirikiano mkubwa na inaonesha Mheshimiwa Sanga pamoja na kwamba wananchi wanakuoenda, lakini na sisi tunakupenda kwa kazi unayowafanyia.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ni kweli kabisa vijiji saba katika eneo la Makambako ikiwemo pamoja na vijiji alivyovitaja vya Ikwete pamoja na Kifumbe ilikuwa vipatiwe umeme kupitia mpango huo. Na kama utakumbuka Mheshimiwa Sanga, uko mradi unaojenga usafirishaji wa umeme kutoka Makambako kupitia Madaba hadi Songea
na ndiyo vijiji vilitakiwa vipatiwe umeme kutoka utaratibu ule.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hata vijiji vyote vile, saba pamoja na vitongoji vyako vyote imeingia katika mpango wa REA ulioanza kutekelezwa katika maeneo ya Makambako pamoja na Njombe kuanzia tarehe 15 Januari,
2017.
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kuwamabia Waheshimiwa Wabunge na Watanzania kwa ujumla kwamba utekelezaji wa Mradi wa REA Awamu ya Tatu umeanza rasmi tangu tarehe 15 Januari, 2017 na tunachofanya sasa na wananchi na Wabunge ni kuzindua Mkoa hadi Mkoa ili kuwakabidhi wakandarasi Waheshimiwa Wabunge mliko ili na ninyi wote mkitusaidia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Deo Sanga tumeshazinfua tangu tarehe 15 Januari na wananchi wako wa vijiji hivyo saba pamoja na kijiji cha Kifumbe wataanza kupata umeme kupitia mradi huu wa REA wa Awamu ya Tatu.

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. KAPT. (MST.) GEORGE H. MKUCHIKA Aliuliza:- Serikali iliwaahidi wananchi wa Mikoa ya Mtwara na Lindi umeme wa uhakika na wa kutosha baada ya kugundulika kwa gesi na baada ya neema ya muda mfupi hivi sasa kuna tatizo kubwa la kukatika kwa umeme mara kwa mara katika Mikoa hiyo ikiwemo na Wilaya ya Newala. Je, tatizo ni nini na Serikali inachukua hatua gani kumaliza kabisa tatizo hili?

Supplementary Question 3

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la kukatika kwa umeme katika Mikoa ya Lindi na Mtwara halitofautiani na tatizo la kukatika kwa umeme katika Mkoa wa Kilimanjaro hasa Jimbo la Moshi Mjini. Je, Serikali inatoa tamko gani kuhusu kuhakikisha kwamba
wanatatua tatizo la ukatikaji wa umeme katika Jimbo la Moshi Mjini?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa katika Mikoa ya Kilimanjaro, Dar es Salaam na Arusha kulikuwa na tatizo la mara kwa mara la umeme. Lakini uko mradi mmoja unaoitwa Trade Up unaotekeleza ukarabati wa miundombinu katika mikoa hiyo mitatu. Mheshimiwa Japhary nikuambie tarehe 22 Mei taratibu kabisa za kukamilisha ujenzi na ukarabati wa miundombinu katika Mji wa Kilimanjaro utakamilika kupitia
mpango huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, na kwa hatua ya pili
tunajenga pia mradi wa kusafirisha umeme unaotoka Kinyerezi kwenda Tanga, unakwenda mpaka Namanga, lakini uko unaotoka hapa sasa kutoka SInginda kupita Manyara na kwenda mpaka Kilimanjaro wa kilovoti 400 ambao pia utaongeza nguvu ya umeme na kupunguza sasa
kukatika katika kwa umeme kwa sababu ya low voltage.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Mheshimiwa
Japhary kuanzia mwezi Mei tunaweka kwamba kukatika umeme katika Mkoa wa Kilimanjaro utapungua kwa kiasi kikubwa.

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. KAPT. (MST.) GEORGE H. MKUCHIKA Aliuliza:- Serikali iliwaahidi wananchi wa Mikoa ya Mtwara na Lindi umeme wa uhakika na wa kutosha baada ya kugundulika kwa gesi na baada ya neema ya muda mfupi hivi sasa kuna tatizo kubwa la kukatika kwa umeme mara kwa mara katika Mikoa hiyo ikiwemo na Wilaya ya Newala. Je, tatizo ni nini na Serikali inachukua hatua gani kumaliza kabisa tatizo hili?

Supplementary Question 4

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Mkwajuni ambao ndiyo makao makuu ya Wilaya ya Songwe, kila wiki umeme upo siku tatu na umeme haupo siku nne mpaka hivi ninavyoongea, hata wiki iliyopita nilikuwa huko. Nini tatizo la
kukatika katika kwa umeme hasa ule unaotoka Mbeya Lwanjilo, Chunya, Makongolosi mpaka Mkwajuni. Tatizo ni nini kila mwaka maana huu ni mwaka wa nne sasa hatuna umeme wa uhakika pale Mkwajuni?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa maeneo mengi umeme tulionao haujitoshelezi ndiyo maana tunarekebisha na kuimaisha miundombinu ikiwemo Mkoa wa Mbeya pamoja na mikoa
ya jirani.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua tuliyochukua kwa
sasa tunajenga mradi wa kusafirisha umeme wa KV 400 kutoka Mbeya kupita Sumbawanga kwenda Kigoma hadi Nyakanazi, lakini huo huo utakwenda mpaka Bulyanhulu na Geita umbali wa kilometa 1,108. Kwa hiyo, hatua hii itakapokamilika katika Mkoa wa Mbeya tatizo la umeme litapungua sana. Matarajio yetu, kufikia mwezi Julai, 2018 matayarisho, ujenzi pamoja na
uimarishaji wa njia za kuimarisha umeme katika Mkoa wa Mbeya utakuwa umekamilika. Kwa hiyo, kuanzia Julai mwakani kukatika kwa umeme katika Mkoa wa Mbeya kutapungua au kutakoma kabisa kwasababu ya kutekelezwa kwa mradi huu.

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. KAPT. (MST.) GEORGE H. MKUCHIKA Aliuliza:- Serikali iliwaahidi wananchi wa Mikoa ya Mtwara na Lindi umeme wa uhakika na wa kutosha baada ya kugundulika kwa gesi na baada ya neema ya muda mfupi hivi sasa kuna tatizo kubwa la kukatika kwa umeme mara kwa mara katika Mikoa hiyo ikiwemo na Wilaya ya Newala. Je, tatizo ni nini na Serikali inachukua hatua gani kumaliza kabisa tatizo hili?

Supplementary Question 5

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa tatizo la kukatika katika kwa umeme lililopo Mtwara na Lindi linafanana kabisa na hali ilivyo katika Halmashauri ya Wilaya ya Temeke hasa katika Kata za Kurasini, Mtoni, Keko, Chang’ombe, Tandika Sandari, Buza na
maeneo yote ya Yombo ambapo kila siku ni lazima umeme ukatike na pale inapokuwa na hali ya mawingu au mvua basi umeme hukatika kwa muda mrefu zaidi. Sasa wananchi wa Temeke wangependa kusikia majibu ya Serikali, ni lini tatizo hili litakoma?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza katika kujibu swali la nyongeza katika Mkoa wa Kilimanjaro, mtekelezaji anayerekebisha mitambo pamoja na miundombinu katika maeneo ya Temeke, Kurasini, Kigamboni pamoja na Kiwalani
ni mradi mmoja. Lakini katika maeneo ya Temeke mwezi uliopita nilifatana na Mheshimiwa Mbunge wa Temeke, nimeenda kukagua mradi wa Temeke na Kurasini. Kinachofanyika sasa wanaimarisha na kuweka vikombe vipya kwa sababu maeneo ya Temeke, Kurasini yamezidiwa. Kwa hiyo, tunaongeza nguvu ya umeme ya kilovolti 220
kutoka 132, lakini kadhalika tunafupisha umbali wa nyaya uliokuwepo wa zaidi ya kilometa 57 ili ziwe chini ya kilometa 50 katika maeneo ya Temeke, Kurasini, Kigamboni pamoja
na Kiwalani.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa utaratibu wa
kukamilisha tarehe 27 Aprili, 2017 mradi utakamilika. Kwa hiyo, baada ya kukamilika kwa mradi huu maeneo ya Temeke, Kurasini, Kigamboni na maeneo ya jirani tatizo la umeme
litapungua sana kwa kiasi kikubwa.