Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. MUSUKUMA J. KASHEKU Aliuliza:- Wakala wa Misitu Tanzania amehamisha vigingi vya mipaka ya misitu vilivyowekwa tangu mwaka 1974 na kuviweka katikati ya vijiji kwa kufuata ramani ya mwaka 1984, vijiji ambavyo vina GN ya Serikali na vinatambuliwa na hata Mheshimiwa Rais amezuia zoezi hilo, lakini hakuna kilichofanyika hivyo kuwafanya wananchi wa vijiji hivyo kuishi maisha ya mashaka na sintofahamu. Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya tatizo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. MUSUKUMA J. KASHEKU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nilitaka tu kumwambia kwamba, yale aliyoyajibu hapa si sawa na uhalisia ulioko kule Jimboni.
Wananchi wangu wa vijiji vya Bugurula, Kasota, Nyawirimila, Sungusila na Kakubiro, wamewekewa matangazo mwezi mmoja uliopita na wakapelekewa barua za kuondoka kwenye vijiji ambavyo tayari vina shule na sasa Waziri anasema wao hawakuwa na huo mpango na hawajafanya wanaendelea na utaratibu na wameweka vigingi. Nilikuwa nataka kujua Waziri kama hizi taarifa alizozitoa ni sahihi ili niwaambie wale wananchi wangu kule wayang’oe yale matangazo yaliyowekwa kule? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kutokana na mkanganyiko wa mipaka ya vijiji na mapori ya hifadhi kumesababisha mpaka tunavyozungumza sasa kuna operesheni zinafanyika kwenye Mkoa wa Geita na Mkoa wa Biharamulo, Serikali ilitoa tangazo la siku tatu wananchi waondoe mifugo iliyopo kwenye hifadhi; siku tatu ng’ombe zitoke kwenye eneo la hifadhi kana kwamba hizi ng’ombe sijui zina mota miguuni, lakini wananchi wa Kisukuma hawakuwa na tatizo walitii amri bila shuruti.
Na kwa kuwa waliopo kule wahifadhi wameidanganya Serikali kwa kuwaambia kuna mifugo milioni 60 na kule hakuna mifugo milioni 60; wamezikosa baada ya kupewa hiyo bajeti ya operesheni wakaikosa mifugo wananza kukamata sasa kilometa saba kwenye vijiji na wakati kuna beacon zinazoonesha mipaka ya kijiji. Je, Waziri
husika anatoa kauli gani kwa wananchi ambao
wamekamatiwa ng’ombe zao Ngara, Katente na Chato walioko mahakamani na wameshapewa hukumu ya ng’ombe zao?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Mheshimiwa Mbunge ni Mjumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii na kwa hiyo kwa kiasi kikubwa anafahamu uzito, upana na ukubwa wa changamoto inayohusiana na suala la uhifadhi na
muingiliano wa shughuli za kibinadamu katika maeneo mbalimbali nchi nzima.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto hii ni kubwa na haifanani kutoka mahali pamoja hata mahali pengine. Yapo matatizo yanayohusiana na wakulima na yapo matatizo yanayohusiana na wafugaji. Katika swali lake la msingi Mheshimiwa Mbunge alizungumzia juu ya suala la maeneo ya vijiji ambayo yamo ndani ya hifadhi ya Geita na kweli lilikuwa ni suala la mipaka baina ya vijiji na maeneo hayo husika. Na kama nilivyojibu kwenye jibu la msingi ni kwamba Wizara yangu kwa niaba
ya Serikali haijafanya operesheni yoyote ya kuondoa wanavijiji katika maeneo hayo. Lakini nimesikia alivyosema kwamba kuna matangazo yamebandikwa huko ambayo sisi kama Wizara hata ninaposimama wakati huu mahali hapa
bado hatuwezi kuthibitisha uwepo wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya hapa kwa kuwa Serikali ni pana iko mamlaka ya Wilaya, Mkoa na ipo Serikali Kuu kupitia Wizara, sote sisi ni Serikali. Baada ya hapa nikutane naye ili tuweze kufuatilia matangazo hayo juu ya uwepo wake na
uhalali wake ili tuweze kujua namna ya kuweza kushughulikia tatizo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusu swali lake la wale wafugaji na mifugo katika maeneo ya Geita, Biharamulo na maeneo mengine ambapo zipo operesheni zinaendelea sasa hivi zikiendeshwa na mamlaka za Mikoa na Wilaya huko zilipo, kama nilivyotoa maelezo katika jibu langu la msingi, migogoro ipo katika maeneo mengi, lakini kila mahali, kila mgogoro ni wa aina yake; chanzo tofauti, ukubwa tofauti na kwa hiyo tarajia kwamba utatuzi wake pia utakuwa upo
tofauti. Katika maeneo aliyoyataja uingiaji wa mifugo katika maeneo yaliyohifadhiwa ni mkubwa sana tena uliopelekea hata kuingia kwa mifugo kutoka nchi jirani na yeye amesema.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Serikali kupitia
Mamlaka ya Mkoa imeendelea kufanya operesheni hizo kwa sababu kimsingi hatua za Serikali tulizotangaza kwamba zinaendelea kuchukuliwa haziwezi kukamilika leo au kesho
kwa sababu zinafuata taratibu za kushughulikia changamoto za Kiserikali ambazo aghalabu huchukua muda mrefu. Katika kipindi hicho tukiacha ng’ombe waendelee kubaki katika
maeneo hayo ya hifadhi, wakati utakapofika
tumekwishapata ufumbuzi wa nini kifanyike hifadhi hizo hazitakuwepo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimuombe
Mheshimiwa Mbunge utaratibu ambao unaendelea hivi sasa wa Serikali wa kushughulikia changamoto hizo kwa uzito wake na katika maeneo ambayo athari ni kubwa huo utakuwa ni
utaratibu wa Serikali na aendelee kuunga mkono jitihada za Serikali za kuamua kusimamia uhifadhi kwa maslahi ya nchi yetu hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama kutakuwa na jambo lingine ambalo ni mahususi kuhusiana na hatua hizo ambazo Serikali inachukua katika ngazi hizo za Mikoa na Wilaya basi anaweza kulileta, nimesema yeye ni Mjumbe wa Kamati
inayosimamia maliasili kwahiyo tunaweza kupokea maoni yake juu ya namna bora zaidi ya kuweza kushughulikia tatizo hili lakini kwa mujibu wa sheria. Katika hili sheria, kanuni na taratibu zitazingatiwa katika kushughulikia changamoto hizi.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa nitoe majibu ya ziada pamoja na majibu mazuri ambayo yametolewa na Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la msitu katika Wilaya na eneo lilozunguka Mji wa Geita limefikishwa pia kwenye Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Geita na maazimio yaliyofikishwa yameletwa kwetu kwa ajili ya kufikiria ni namna
gani katika maeneo ambayo watu wanaishi tunaweza kupunguza eneo la msitu kwa ajili ya matumizi mengine ili kukidhi hali halisi ya Mji Mkuu wa Mkoa ambao sasa uko pale Geita.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, jambo hili
tunaendelea kulizungumza na Mheshimiwa Mbunge awe na subira wakati Serikali ya Mkoa na Wilaya inapoongea na Wizara kuhusu msitu huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la pili; wapo ng’ombe ambao ni wengi sana katika maeneo ya misitu ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja. Mifugo hii ipo kwenye maeneo ya hifadhi kinyume cha sheria zetu; kinyume cha Sheria ya Uhifadhi wa Misitu Na. 5 ya mwaka 2009 kifungu cha 21(1). Na wananchi hawa wanajua kwamba wapo kwenye Hifadhi za Taifa kinyume cha sheria; walipewa muda wa kuondoka na tangazo la Mkoa na muda ule ukamalizika. Huwezi kusema mtu ambaye anafanya makosa ya kisheria kwamba hakupewa muda wa kutosha wa kufanya makosa yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nitumie nafasi hii kuwashauri wafugaji wote ambao wana mifugo yao ndani ya maeneo ya Hifadhi za Taifa kinyume cha sheria zetu kwamba watoe mifugo hiyo mapema iwezekanavyo kabla Serikali haijachukua hatua ya kisheria kudhibiti mifugo hiyo.

Name

John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MUSUKUMA J. KASHEKU Aliuliza:- Wakala wa Misitu Tanzania amehamisha vigingi vya mipaka ya misitu vilivyowekwa tangu mwaka 1974 na kuviweka katikati ya vijiji kwa kufuata ramani ya mwaka 1984, vijiji ambavyo vina GN ya Serikali na vinatambuliwa na hata Mheshimiwa Rais amezuia zoezi hilo, lakini hakuna kilichofanyika hivyo kuwafanya wananchi wa vijiji hivyo kuishi maisha ya mashaka na sintofahamu. Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya tatizo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. JOHN H. WEGESA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa mara nyingine kwa kuniona na kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza kwa niaba ya watu wa Tarime.
Mheshimiwa Naibu Spika, GN hizi zilizotangaza haya maeneo na kuweka mipaka ya mapori ni ya miaka 1984; vijiji vingi ni vya miaka ya 1970, 1975 na kuendelea. Kwa hiyo, GN hizi zimetangazwa vijiji vikiwepo ukichukua Kata kwa mfano ya Kwihancha, Goronga na Nyanungu vimepakana na Pori la Serengeti; vijiji vyote vya maeneo haya ni vya miaka ya 1970 na vimesajiliwa vina usajili. Lakini watu wa Serikali wameanza kuhamisha kwa kutumia GN miaka ya 1990 mpaka sasa hivi wanazidi kurudisha watu nyuma, watu hawana maeneo ya kulima wala ya kuchungia.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba Waziri watatue hili tatizo kwa haraka ili watu waendelee kuishi maisha yao ya kawaida na wasiendelee kuona wafugaji kwamba ni wahaini katika nchi yao, wawaruhusu ng’ombe wao waendelee kuchunga kwenye maeneo ambayo ni ya vijiji vyao kihalali na kisheria.

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ulivyosema kwa kiwango kikubwa yale yalikuwa ni maoni au ushauri lakini ni vyema sauti ya Serikali ikasikika na kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii napenda kufanya marekebisho madogo tu kwamba sio vyema kujumuisha au kutoa kauli ya jumla kwamba GN zote ni za miaka 1980. Nadhani katika eneo mahususi analolitaja inawezekana ipo hivyo lakini utaratibu ambao utaweza kutufikisha mahali ambapo patakuwa ndio pana usahihi zaidi ni kwa kuchambua kila kesi kwa kesi na kila hoja kwa hoja kwamba eneo fulani linahusishwa na GN namba fulani,
tutakwenda kuiangalia kwamba ni ya mwaka gani ili tuweze kujua eneo lililohifadhiwa na kijiji kilichopo kipi kilitangulia.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hata hivyo kutangulia au kuja baadae pengine inaweza kuwa sio hoja ya msingi sana; hoja ya msingi itakuwa ni uhifadhi kwa maslahi ya Taifa. Na hivyo ndio maana tumesema kwamba tunayo tume
ambayo inaendelea kufanya kazi ambayo itahusisha pia na kufanya mapitio ya hayo yote tunayoyazungumzia. Kamati ambayo nimesema jana wakati najibu swali, lakini narudia tena leo ipo katika hatua ya kupitiwa na Makatibu Wakuu
na baada ya pale itakwenda kwenye hatua ya Mawaziri halafu baadae kwenye ngazi za mamlaka za juu za Serikali.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. MUSUKUMA J. KASHEKU Aliuliza:- Wakala wa Misitu Tanzania amehamisha vigingi vya mipaka ya misitu vilivyowekwa tangu mwaka 1974 na kuviweka katikati ya vijiji kwa kufuata ramani ya mwaka 1984, vijiji ambavyo vina GN ya Serikali na vinatambuliwa na hata Mheshimiwa Rais amezuia zoezi hilo, lakini hakuna kilichofanyika hivyo kuwafanya wananchi wa vijiji hivyo kuishi maisha ya mashaka na sintofahamu. Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya tatizo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa tatizo lililopo katika misitu ya Geita linafanana sana na tatizo lililopo katika Msitu wa Shume ambapo katika vijiji vya Shume, Nywelo na Mkuhnyi ambavyo vipo katika Kata ya Manolo navyo eneo la Msitu wa Hifadhi wa Shume umeingia katika maeneo ya vijiji ambako wananchi mara nyingi ndiko wanakofanya shughuli zao za kiuchumi.
Mheshimiwa Naibu Spika, na tatizo la mgogoro huu pia limeripotiwa katika Randama ya Wizara ya Ardhi. Je, ni lini sasa Serikali itakaa na wananchi hawa wa vijiji vya Shume, Nywelo pamoja na Mkunki ili angalau waweze kutatua tatizo hili?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, tumesikia, tumepokea shamba la msitu wa kupandwa wa Shume uliopo katika maeneo yale ya vijiji alivyovitaja vya Shume, Nywelo na Mkunki. Ni suala ambalo kama alivyosema mwenyewe limeorodheshwa kwenye
orodha ya maeneo ambayo yanatakiwa kushughulikiwa chini ya orodha ya migogoro ya ardhi iliyoandaliwa na Wizara ya Ardhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana kwa
kutukumbusha licha ya kwamba lipo kwenye orodha na kwa kweli kwa namna ambavyo anaweza kuwasemea wananchi ya maeneo haya kama mwakilishi wao na nimuahidi sambamba na kazi inayoenda kufanyika chini ya kamati iliyoundwa; mimi na yeye tutapanga tutaweza kwenda kwenye hili eneo tukaangalie uhalisia ili tuweze hata kuishaurihiyo kamati.

Name

Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSUKUMA J. KASHEKU Aliuliza:- Wakala wa Misitu Tanzania amehamisha vigingi vya mipaka ya misitu vilivyowekwa tangu mwaka 1974 na kuviweka katikati ya vijiji kwa kufuata ramani ya mwaka 1984, vijiji ambavyo vina GN ya Serikali na vinatambuliwa na hata Mheshimiwa Rais amezuia zoezi hilo, lakini hakuna kilichofanyika hivyo kuwafanya wananchi wa vijiji hivyo kuishi maisha ya mashaka na sintofahamu. Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya tatizo hilo?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kuna tatizo pia la mipaka kati ya TFS na vijiji Wilayani Kondoa; vijiji vya Mnenia, Masanga, Itolowe na Kasese ambapo beacon za TFS zimeingilia katika mashamba ya wanavijiji hawa. Sasa ningependa kujua Serikali ina mkakati gani au ni lini itarekebisha tatizo hili ambalo linawaacha wanavijiji hawa njia panda? Ahsante.

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikia akisema kwamba katika vijiji alivyovitaja beacons za TFS kwa kauli yake zimeingia katika mashamba ya wananchi kwenye vijiji hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nirudie tena kwamba hii
ndio sababu tumeunda kamati maalum kwa sababu kusema tu moja kwa moja kwamba beacons zimeingia kwenye maeneo ya mashamba ya watu bila kuangalia kwamba upo
uwezekano mashamba ya watu yameingia ndani ya maeneo ya hifadhi haitakuwa sahihi katika hatua hii. Kwa hiyo, tuipe nafasi Serikali iweze kuendelea kufanya kazi ya kwenda kufanya utafiti wa kwenye site wa kuangalia uhalisia ulivyo tukipima kwamba ni kipi kimeingia upande upi lakini wakati huo huo tukiangalia zaidi maslahi ya hifadhi ambayo ndio priority kwa Taifa.

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. MUSUKUMA J. KASHEKU Aliuliza:- Wakala wa Misitu Tanzania amehamisha vigingi vya mipaka ya misitu vilivyowekwa tangu mwaka 1974 na kuviweka katikati ya vijiji kwa kufuata ramani ya mwaka 1984, vijiji ambavyo vina GN ya Serikali na vinatambuliwa na hata Mheshimiwa Rais amezuia zoezi hilo, lakini hakuna kilichofanyika hivyo kuwafanya wananchi wa vijiji hivyo kuishi maisha ya mashaka na sintofahamu. Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya tatizo hilo?

Supplementary Question 5

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana; lipo tatizo kubwa kati ya Uwanda Game Reserve na vijiji vya Kilangawana, Maleza, Legeza, Mpande, Ilambo, Mkusi, Iweliamvula na Ngomeni. Kwa watu wa TFS
kuhamisha mipaka inayotambulika toka enzi za nyuma na kusogeza katikati ya vijiji. Tatizo hili ni kubwa sana na mimi nilishaenda mara kadhaa kumwambia Waziri kwamba naomba afike asikilize pande zote mbili kwa sababu ninachokiona hawa askari wa TFS ni kama wanagandamiza wananchi wakati jambo lipo wazi. Je, ni lini Serikali itatuma uongozi wa kwenda kuangalia haki juu ya wananchi wale?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, anazungumzia juu ya suala la Uwanda Game Reserve na ujirani wake na vijiji vilivyopo jirani na eneo hili la hifadhi. Na hoja yake inafanana na zile hoja zilizotangulia
pale mbele kwamba mipaka iliyowekwa na TFS katika miaka ya karibuni au katika siku za karibuni imeingia ndani ya maeneo ya vijiji.
Kama nilivyosema hapo awali kwamba sio vema
kwenda moja kwa moja na kutoa kauli ambayo inaonekana kama ni ya uthibitisho au ni ya ukweli kwamba mipaka ya hifadhi ndiyo iliyoingia kwenye maeneo ya vijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia niweze kusema jambo moja tu hapa kwamba tuelewane kitu kimoja kwamba mipaka tunayoizungumzia ya miaka mingi haikuwa na alama; kwa hiyo, kuna suala la kuweka mpaka kuwepo lakini kuna suala pia la mpaka kuwekewa alama.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika miaka ya karibuni kilichofanyika au kinachoendelea kufanyika ni kuweka alama za kudumu hizo beacons au maboya au unaweza kutafuta
lugha nyingine yoyote ya Kiswahili, lakini ni alama
zinazoonekana. Sasa wakati wa kuweka alama
zinazoonekana Serikali inafuata mipaka ambayo ipo kwa mujibu wa maandishi kwa kutumia GPS coordinates kwenye ramani ambayo haikuwa imewekewa alama. Sasa kwa kuwa wananchi hawakuiona ile mipaka kwa alama zinazoonekana
licha ya kwamba kwa mujibu wa sheria zipo kwenye ramani, sasa hivi wananchi wanadhani kwamba alama hizo zimehama.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukweli ni kwamba alama hizo zinawekwa mahali pale ambapo ndipo kwa mujibu wa sheria alama hizo ndipo zilipo na kwa hiyo sasa ni vema tukasubiri utaratibu unaofanyika na Serikali wa kwenda kuweka alama kwenye maeneo hayo kwa sabau kuweka alama sio maana yake tayari hatua za mwisho zimeshafanyika za kuweza kuwahamisha wananchi; tunaweka kwanza alama kutambua maeneo hayo halafu baada ya pale tunaweza kuendelea na kuelimishana kwamba kwa nini mpaka upo hapa na sio pale.