Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leonidas Tutubert Gama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Primary Question

MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Wananchi wa Songea Mjini wamekuwa wakiitumia Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma kama Hospitali yao ya Wilaya hivyo kufanya kuwepo na mgongano wa kiutendaji kati ya Mamlaka ya Mkoa inayoitambua Hospitali hiyo kama Rufaa ya ngazi ya Mkoa na Mamlaka ya Wilaya. Tarehe 10 Januari, 2016, Mheshimiwa Waziri wa Afya alifika kuona hali halisi na juhudi za wananchi wa Songea Mjini za kujenga Kituo cha Afya Mji Mwema ambacho kimefikia hatua kubwa, hivyo wakamwomba Waziri kituo hicho kipandishwe hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya, Songea Mjini. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuiacha Hospitali ya Mkoa ifanye kazi ya Rufaa Kimkoa? (b) Je, Serikali haioni haja ya kupunguza msongamano katika hospitali hiyo kwa kuanzisha Hospitali ya Wilaya Songea Mjini? (c) Je, ni lini basi Serikali itakipa hadhi Kituo cha Afya cha Mji Mwema, Songea Mjini ya kuwa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. LEONIDAS T. GAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake, lakini nataka nimjulishe kwamba Hospitali ya Rufaa hiyo ya Mkoa wa Ruvuma ina msongamano mkubwa sana wagonjwa na hasa akinamama wajawazito na watoto. Kwa mfano, hivi sasa Hospitali ya Mkoa ina vitanda 13 tu kwa ajili ya akinamama wajawazito na watoto. Akinamama hawa kwa wastani wa siku ni wagonjwa 25 mpaka 35 wakitumia vitanda 13.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile lipo tatizo la msingi kweli kweli; pale katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa akinamama wajawazito wananunua dawa, damu, mipira ya kujifungulia na vifaa vingine vyote vya kujifungulia, wananunua wenyewe. Sasa nauliza: Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba huduma zinazotolewa za akinamama wajawazito na watoto zinatolewa katika kiwango kinachotakiwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa vile hivi sasa tunategemea sana Kituo cha Afya cha Mji Mwema ambacho Mheshimiwa Naibu Waziri amesema bado hakijafika mahali kikapandishwa hadhi ya kuwa hospitali kamili. Je, Serikali ni lini italeta gari ya wagonjwa kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wanaofika katika Kituo cha Afya cha Mji Mwema hasa akinamama wajawazito na watoto?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nipokee malalamiko ya Mheshimiwa Mbunge kwamba pale akinamama wananunua dawa, vifaa tiba na mambo mengine; hili Mheshimiwa Mbunge kwa sababu ameshali-cite pale, ina maana jambo hilo lipo. Katika ziara zangu kwa maeneo mbalimbali nilikuwa nikitoa maelekezo kwamba Serikali inapeleka fedha katika Vituo vya Afya hasa katika Halmashauri zetu; lengo kubwa watu wapate dawa na vifaa tiba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimezungumza hapa mara kadhaa kwamba kwa kipindi cha sasa suala la uzembe kwamba Serikali inatoa fedha lakini watu hawazitumii kama inavyokusudiwa (kununua dawa na vifaa tiba), niliwaeleza DMOs wote na Waganga Wakuu wa Mikoa sehemu nilizopita kwamba wahakikishe fedha zinazokwenda lazima ziweze kutumika kama inavyokusudiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nichukue concern hii, lakini hata hivyo, nafahamu kwamba Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alitoa fedha kwa ajili ya kununua vitanda katika Halmashauri zetu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na hivi vitu vimeshakuwa tayari, naomba na yeye avipokee aende akakabidhi mwenyewe pale. Lengo kubwa ni kupunguza changamoto katika maeneo yako. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kwamba hakuna ambulance; mara kadhaa nimekuwa nikitoa ufafanuzi hapa ikiwezekana mchakato uanze katika Halmashauri zetu. Naomba niseme kwamba kilio hiki cha Mheshimiwa Mbunge tumekisikia, japokuwa suala la ambulance lazima lianzishwe katika Halmashauri kuonesha yale mahitaji, lakini tutaangalia nini kifanyike sasa kushirikiana pamoja Serikali Kuu na Halmashauri ya Songea ili tupate ambulance. Wapi itakapotoka, hiyo haijalishi, lakini cha msingi tupate ambulance kwa ajili ya wakazi wengi sana nikijua wazi kwamba hata watu kutoka eneo la Namtumbo wanakuja pale Songea kwa ajili ya kupata huduma ya afya.(Makofi)

Name

Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Wananchi wa Songea Mjini wamekuwa wakiitumia Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma kama Hospitali yao ya Wilaya hivyo kufanya kuwepo na mgongano wa kiutendaji kati ya Mamlaka ya Mkoa inayoitambua Hospitali hiyo kama Rufaa ya ngazi ya Mkoa na Mamlaka ya Wilaya. Tarehe 10 Januari, 2016, Mheshimiwa Waziri wa Afya alifika kuona hali halisi na juhudi za wananchi wa Songea Mjini za kujenga Kituo cha Afya Mji Mwema ambacho kimefikia hatua kubwa, hivyo wakamwomba Waziri kituo hicho kipandishwe hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya, Songea Mjini. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuiacha Hospitali ya Mkoa ifanye kazi ya Rufaa Kimkoa? (b) Je, Serikali haioni haja ya kupunguza msongamano katika hospitali hiyo kwa kuanzisha Hospitali ya Wilaya Songea Mjini? (c) Je, ni lini basi Serikali itakipa hadhi Kituo cha Afya cha Mji Mwema, Songea Mjini ya kuwa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 2

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa uzito unaoikabili Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma ni uzito ule ule unaoikabili Hospitali ya Wilaya ya Mbinga hasa ikizingatiwa Wilaya ile inahudumia Halmashauri kubwa tatu, yaani Halmashauri ya Nyasa, Halmashauri ya Mbinga Mjini na Halmashauri ya Mbinga Vijijini, lakini vile vile sehemu ya Halmashauri ya Songea Vijijini: Mheshimiwa Waziri haoni sasa kuna haja ya kutimiza ile ahadi yake aliyoiahidi ya kuiboresha ile hospitali ili kuweza kupunguza mzigo mkubwa kwenda Hospitali ya Mkoa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa Mbunge anakumbuka kwamba tulikuwepo kule Mbinga na tumebaini hizo changamoto, ndiyo maana katika mipango yetu ya sasa, tumeamua kwamba Kituo cha Afya cha Kalembo ambacho ukiangalia mahitaji, sasa yamekuwa makubwa.
Kwanza tuboreshe Kituo cha Afya cha Kalembo ambacho siyo muda mrefu sana tutaenda kufanya ukarabati mkubwa sana wa theater na wodi ya watoto pale; lengo kubwa ni kwamba huduma ziweze kupatikana vizuri zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, ndiyo maana wenzetu kule wa Nyasa tume-cite Kituo cha Afya cha Mkiri ambacho tunaenda kufanyia huduma hiyo hiyo vilevile. Lengo letu kubwa ni katika maeneo hayo mawili, Nyasa na pale Mbinga, tukiweka huduma za kutosha zitasaidia wananchi wa eneo hilo waweze kupata huduma vizuri.

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Wananchi wa Songea Mjini wamekuwa wakiitumia Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma kama Hospitali yao ya Wilaya hivyo kufanya kuwepo na mgongano wa kiutendaji kati ya Mamlaka ya Mkoa inayoitambua Hospitali hiyo kama Rufaa ya ngazi ya Mkoa na Mamlaka ya Wilaya. Tarehe 10 Januari, 2016, Mheshimiwa Waziri wa Afya alifika kuona hali halisi na juhudi za wananchi wa Songea Mjini za kujenga Kituo cha Afya Mji Mwema ambacho kimefikia hatua kubwa, hivyo wakamwomba Waziri kituo hicho kipandishwe hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya, Songea Mjini. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuiacha Hospitali ya Mkoa ifanye kazi ya Rufaa Kimkoa? (b) Je, Serikali haioni haja ya kupunguza msongamano katika hospitali hiyo kwa kuanzisha Hospitali ya Wilaya Songea Mjini? (c) Je, ni lini basi Serikali itakipa hadhi Kituo cha Afya cha Mji Mwema, Songea Mjini ya kuwa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 3

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Hospitali ya Wilaya ya Njombe, Kibena ni hospitali ambayo sasa inasomeka kama Hospitali ya Mkoa na inahudumia watu wengi sana. Pale kuna tatizo kubwa la watoto njiti na hakuna chumba cha kutunzia watoto hawa njiti. Je, Serikali iko tayari kutusaidia kupata chumba cha watoto njiti pale ili tuweze kuokoa maisha ya hawa watoto? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuchukue concern hiyo, kwa sababu Mheshimiwa Mbunge anafahamu tulikuwepo pale Hospitali ya Kibena. Tutajadili kwa pamoja ili tuone nini tufanye ili eneo lile ambalo ni Makao Makuu ya Mkoa pale sasa, japo katika hospitali ile angalau tuweze kupata centre maalum kwa ajili ya watoto njiti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakaa pamoja kujadili nini tufanye kwa ajili ya Hospitali ya Kibena pale iweze kutoa huduma kwa ajili ya wananchi wetu.

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Wananchi wa Songea Mjini wamekuwa wakiitumia Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma kama Hospitali yao ya Wilaya hivyo kufanya kuwepo na mgongano wa kiutendaji kati ya Mamlaka ya Mkoa inayoitambua Hospitali hiyo kama Rufaa ya ngazi ya Mkoa na Mamlaka ya Wilaya. Tarehe 10 Januari, 2016, Mheshimiwa Waziri wa Afya alifika kuona hali halisi na juhudi za wananchi wa Songea Mjini za kujenga Kituo cha Afya Mji Mwema ambacho kimefikia hatua kubwa, hivyo wakamwomba Waziri kituo hicho kipandishwe hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya, Songea Mjini. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuiacha Hospitali ya Mkoa ifanye kazi ya Rufaa Kimkoa? (b) Je, Serikali haioni haja ya kupunguza msongamano katika hospitali hiyo kwa kuanzisha Hospitali ya Wilaya Songea Mjini? (c) Je, ni lini basi Serikali itakipa hadhi Kituo cha Afya cha Mji Mwema, Songea Mjini ya kuwa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 4

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Tatizo la Songea Mjini linafanana sana na tatizo lililopo katika Wilaya ya Mafia. Wilaya nzima ya Mafia haina hata Kituo kimoja cha Afya. Ukizingatia kwamba alipokuja Waziri Mkuu tulimwomba suala hili na mchakato tumeshauanza katika ngazi ya Wilaya. Je, ni lini sasa Serikali itatupatia Kituo cha Afya angalau kimoja pale Kilongwe kwa kuongeza hadhi ile zahanati iliyopo pale?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tulipofika Mafia tulienda katika hicho Kituo cha Afya na nikatoa mapendekezo kadhaa likiwemo suala zima la makazi ya watu katika maeneo yale, lakini tulikubaliana kwamba wafanye mchakato na Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Dau, kwa sababu Mafia jiografia yake lazima tuboreshe huduma ya afya na nilitoa maelekezo pale mbele ya DC na mbele ya Mkurugenzi nini kifanyike kituo kile kiweze kuboreshwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimwambie Mheshimiwa Dau kwamba Serikali imechukua ile, tutafanya kila liwezekanalo hasa eneo la Mafia katika kile Kituo cha Afya ambacho nimekitembelea mwenyewe, tutafanya uboreshaji mkubwa katika kipindi kinachokuja.

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. LEONIDAS T. GAMA aliuliza:- Wananchi wa Songea Mjini wamekuwa wakiitumia Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma kama Hospitali yao ya Wilaya hivyo kufanya kuwepo na mgongano wa kiutendaji kati ya Mamlaka ya Mkoa inayoitambua Hospitali hiyo kama Rufaa ya ngazi ya Mkoa na Mamlaka ya Wilaya. Tarehe 10 Januari, 2016, Mheshimiwa Waziri wa Afya alifika kuona hali halisi na juhudi za wananchi wa Songea Mjini za kujenga Kituo cha Afya Mji Mwema ambacho kimefikia hatua kubwa, hivyo wakamwomba Waziri kituo hicho kipandishwe hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya, Songea Mjini. (a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuiacha Hospitali ya Mkoa ifanye kazi ya Rufaa Kimkoa? (b) Je, Serikali haioni haja ya kupunguza msongamano katika hospitali hiyo kwa kuanzisha Hospitali ya Wilaya Songea Mjini? (c) Je, ni lini basi Serikali itakipa hadhi Kituo cha Afya cha Mji Mwema, Songea Mjini ya kuwa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 5

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Halmashauri ya Manispaa ya Moshi imekuwa na maombi ya muda mrefu ya Hospitali ya Wilaya na tulikuwa tayari na majibu ya Serikali kwamba wakati wowote watajibu maombi yetu, lakini mpaka sasa hatuoni mwelekeo wowote. Nini tamko la Wizara ya TAMISEMI katika suala hilo la Hospitali ya Wilaya ya Manispaa ya Moshi? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu kweli Halmashauri mbalimbali hazina Hospitali ya Wilaya na siyo Moshi peke yake. Ndiyo maana wakati fulani nilikuwa naongea na dada yangu Mheshimiwa Esther hapa, alileta special request na Mheshimiwa Mbunge najua tupo karibu sana. Tukaona kwamba basi angalau tuongeze suala zima la kimkakati la afya katika eneo hilo, japokuwa tuna hospitali yetu kubwa pale ambayo tunaitegemea, ipo chini ya Kanisa ya KCMC, lakini ni lazima tuboreshe huduma ya afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana tukaona katika kipindi cha sasa tuboreshe kwanza Kituo cha Afya cha Uru Mashariki ambapo siyo muda mrefu, ndani ya miezi miwili tutapeleka fedha za kutosha pale kufanya marekebisho makubwa sana. Tutajenga theater na wodi nyingine pale na vifaa mbalimbali vitawekwa pale. Lengo kubwa ni kupunguza changamoto za wananchi katika eneo lile.