Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

Halmashauri ya Mbeya ina vijiji vingi ambavyo havijapata umeme katika Mpango wa REA na pia utekelezaji wa REA II uko nyuma sana:- (a) Je, ni vijiji vingapi vya Halmashauri ya Mbeya vimo kwenye REA II na mradi utakamilika lini? (b) Je, Kwa nini mradi wa REA II haujalenga kupeleka umeme kwenye huduma za kijamii kama vile Shule, Zahanati, Nyumba za ibada na vyuo? (c) Je, ni lini sasa vijiji vilivyobaki vitapewa umeme wa REA?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJENZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana, kwanza napenda kumshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri na vilevile kuipongeza Wizara hii kwa kazi nzuri inayoifanya kwa kusambaza umeme karibu vijiji vyote vya Tanzania hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia napenda kuwapongeza Mainjinia wa TANESCO waliopo pale Mbeya akiwemo Engineer Maze na Engineer Kiduko pamoja na Engineer Mbalamwezi. Pamoja na hayo, napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, Wizara ina mpango gani wa kusambaza umeme pamoja na hii REA kwenye vitongoji vilivyobaki katika vijiji hivyo vilivyotajwa? (Makofi)
Swali la pili, kutokana na ongezeko la usambazaji wa umeme vijijini, inaelekea capacity ya watumishi wa TANESCO ikiwemo vifaa, haitoshelezi tena.
Je, Wizara ina mkakati wa kuhakikisha kuwa inaongeza capacity ya watumishi ili iendane pamoja na usambazaji wa umeme vijijini?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika pamoja na Mheshimiwa Mbunge, ni kweli kabisa, pamoja na mradi huu kabambe wa REA kuendelea kufanya kazi yake, lakini bado kuna miradi mingine itaendelea kwa ajili ya kukamilisha shughuli zinazoachwa na REA. Baadhi ya kazi zinazoendelea hapa sambamba na miradi ya REA ni pamoja na mradi wa Underline. Mradi wa Underline unaendelea kupita kukamilisha maeneo ambayo yanaachwa na TANESCO pamoja na REA.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusiana na uwezo na capacity pamoja na management, ni kweli kabisa, kama mnavyojua, TANESCO ni shirika la zamani, lakini tuwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge pamoja Serikali ya Awamu ya Tano, ni kwamba tunapata uwezo wa kuongezewa nguvu. Kwa sasa hivi tunaongezewa nguvu Shirika letu la TANESCO kwa maana ya kulinunulia vifaa vya kutosha kama transfoma pamoja na generetors ambako tunatumia mafuta. Kwahiyo, Mheshimiwa Mbunge nimhakikishie kwamba Shirika la TANESCO pamoja na REA pamoja na miradi mingine, itaendelea kuimarishwa ili ifanye kazi zake vizuri.

Name

Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Primary Question

Halmashauri ya Mbeya ina vijiji vingi ambavyo havijapata umeme katika Mpango wa REA na pia utekelezaji wa REA II uko nyuma sana:- (a) Je, ni vijiji vingapi vya Halmashauri ya Mbeya vimo kwenye REA II na mradi utakamilika lini? (b) Je, Kwa nini mradi wa REA II haujalenga kupeleka umeme kwenye huduma za kijamii kama vile Shule, Zahanati, Nyumba za ibada na vyuo? (c) Je, ni lini sasa vijiji vilivyobaki vitapewa umeme wa REA?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Suala hili la Mbeya Vijijini linafanana sana na tatizo sugu la umeme katika Jimbo letu la Mikumi.
Swali langu ni kwamba, je, ni lini Serikali itapeleka umeme huu wa REA kwenye Kata za Tindiga, Mabwerebwere, Ulaya, Zombo, Muhenda, Uleling’ombe na Vidunda?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa hapa tulipofika REA Awamu ya Pili tunatarajia ikamilike mwezi Juni mwaka huu. Vijiji vyote ambavyo vitakuwa vimesalia bila ya kuwa na umeme pamoja na vijiji alivyovitaja Mheshimiwa Mbunge vya kwenye Wilaya pamoja na Jimbo la Mikumi, vyote tunatarajia tuvifikishie umeme kwenye REA Awamu ya Tatu. Kwahiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba vijiji vyake vyote vitapata umeme wa REA Awamu ya Tatu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niwapongeze sana Waheshimiwa Wabunge, kama tutakavyoleta bajeti yetu, tuna matumaini makubwa kwamba bajeti yetu ya kupeleka umeme vijijini itapitishwa na Waheshimiwa Wabunge na ikishapitishwa, kama tunavyosema siku zote, kwa sababu suala la umeme ni la kufa na kupona, dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kupeleka umeme kwenye vijiji vyote.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka kwenye Awamu ya Tano ifikapo 2025 vijiji ambavyo vitakuwa havina umeme vitakuwa ni vya kutafuta. Kwahiyo, vijiji vyote vitapata umeme wa REA Awamu ya Tatu. Ahsante.

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

Halmashauri ya Mbeya ina vijiji vingi ambavyo havijapata umeme katika Mpango wa REA na pia utekelezaji wa REA II uko nyuma sana:- (a) Je, ni vijiji vingapi vya Halmashauri ya Mbeya vimo kwenye REA II na mradi utakamilika lini? (b) Je, Kwa nini mradi wa REA II haujalenga kupeleka umeme kwenye huduma za kijamii kama vile Shule, Zahanati, Nyumba za ibada na vyuo? (c) Je, ni lini sasa vijiji vilivyobaki vitapewa umeme wa REA?

Supplementary Question 3

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi nami niulize swali moja dogo la nyongeza. Katika usambazaji wa umeme kwenye hii REA Phase II, Makao Makuu ya Wilaya ya Chemba, umeme ule umepelekwa kwenye nyumba ya Mkuu wa Wilaya tu. Pia katika vijiji vya Gwandi, Farko na Kwamtoro ambavyo vilikuwepo kwenye programu hii havijapelekewa hata nguzo. Mheshimiwa Waziri naomba anihakikishie hapa kwamba je, mpaka kufika Juni miradi hii itakuwa imekamilika?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa baadhi ya maeneo ambayo yamepelekewa umeme tumepeleka kwenye vituo vikubwa hatujaanza kusambaza kwenye vijiji, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Nkamia kwamba ni kweli vijiji ambavyo vimesalia kwenye ile awamu ya pili sasa hivi kazi inayofanyika ni kuvihakiki ili tubaini ni vituo gani na vijiji gani havijapata umeme kwenye REA Awamu ya Pili.
Mheshimiwa Naibu Spika, azma yetu ya kwanza ni kuhakikisha kwamba vijiji vyote vilivyokuwa kwenye scope ya REA Awamu ya Pili kwanza vinakamilika ifikapo Juni mwaka huu, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili kama itaoneka kwa dosari za kibinadamu vijiji vitasalia, vyote vitakavyokuwa vimebaki vitaingia kwenye REA Awamu ya Tatu pamoja na vijiji vya Mheshimiwa Nkamia.