Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Kati ya mwezi Juni – Desemba, 2015 wananchi wapatao sita walishambuliwa na kuuawa na wanyamapori na Shirika la Hifadhi Tanzania (TANAPA) halikushiriki mazishi ya watu hawa, wala hakuna fidia yoyote waliyopata ndugu wa marehemu, hali inayoonesha mahusiano mabaya kati ya jamii na Mamlaka ya Hifadhi, zaidi ya hayo wanyama kama tembo, wamesababisha hasara kubwa sana kwa kuharibu mazao katika Tarafa ya Daudi, Kata za Marangwa, Daudi, Bargish na Gehandu. • Je, ni lini Serikali itawalipa fidia ndugu wa hao watu sita waliouawa na wanyama wakali katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu? • Je, ni lini Serikali kupitia TANAPA italipa fidia kwa wale wote walioharibiwa mazao shambani mwaka 2014/ 2015?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii niseme kwamba kwanza Serikali haitutendei haki sisi Wabunge. Neno italipa fedha au kifuta machozi pindi hela itakapopatikana haliwafurahishi Watanzania kwa tukio lililotokea la Watanzania kupoteza maisha yao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, kadhia hii kwa Jimbo la Mbulu Mjini ina changamoto kadhaa ikiwemo ukosefu wa Askari Wanyamapori na pia ratiba isiyoonekana ya wenzetu wa TANAPA na jamii zinazopakana na mipaka ya hifadhi na makazi ya watu. Tukio hili la mwaka 2015 lilipoteza maisha ya wananchi saba, siyo watano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pengine niishukuru Serikali kwa sababu, Mheshimiwa Waziri ameleta tu majibu ambayo hajayafanyia kazi kwa sababu, hadi sasa muda mchache uliopita, kama miezi miwili, mitatu, Serikali tayari imetoa fidia kwa wahanga hao wapatao wanne, lakini wale wengine hawakupatiwa hata fidia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu sasa, kwa kuwa tatizo hili linagusa maisha ya Watanzania, je, ni kiasi gani cha fidia au cha kifuta machozi kinatolewa kwa wale wote waliopoteza maisha yao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Kwa kuwa tatizo hili linavunja mahusiano kati ya wananchi na wenzetu wa TANAPA ama Serikali, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuandaa ratiba rasmi itakayowaunganisha wadau wa mpakani katika Tarafa yangu ya Daudi ili waweze kujadiliana matukio yanayotokea na hatimaye kudumisha uhusiano kati ya Shirika la TANAPA na wananchi wa Jimbo la Mbulu Mjini? (Makofi)

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kweli kama alivyosema tayari Serikali imekwishaanza utaratibu wa kulipa bakaa au madeni ambayo yamekuwepo ya muda mrefu yanahusiana na kifuta jacho na kifuta machozi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muda mrefu sana madeni haya yamekuwa hajalipwa, lakini napenda kumpa taarifa Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu kwa ujumla kwamba Serikali katika awamu hii imeshalipa madeni yaliyokuwa yanafikia kiasi cha shilingi bilioni 2.1 na hata sasa kuwa yamebaki jumla ya shilingi takriban milioni 500 peke yake. Mbulu ni mojawapo kati ya Wilaya ambazo zimelipwa malipo hayo na jumla ya fedha kiasi cha shilingi milioni 7,100,000 zimelipwa kwa madhumuni hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maswali yake mawili ya nyongeza; la kwanza, anazungumzia ni kiasi gani cha fedha kilichobaki kwa ajili ya malipo kwa Halmshauri ya Wilaya ya Mbulu? Katika takwimu nilizonazo, nina takwimu za ujumla wa kiasi chote ambacho fedha zinadaiwa kwa Serikali, lakini mahususi kwa ajili ya Mbulu, ukiacha hiki nilichotaja, kilicholipwa tukionana mchana naweza kumpa taarifa juu ya kifuta jasho na kifuta machozi kilichobaki kwa ajili ya Wilaya ya Mbulu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili la kuweka ratiba na utaratibu wa kuweza kujadiliana, kuisharisha mahusiano zaidi baina ya TANAPA na wananchi wanaoishi katika maeneo yanayozunguka hifadhi, hili ni jambo jema na Serikali inalipokea. Tutakwenda kufanya hivyo na tutamshirikisha Mheshimiwa Mbunge ili kuona kwamba tunaimarisha zaidi mahusiano hayo kwa ajili ya uendelevu katika utaratibu mzima wa hifadhi.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Kati ya mwezi Juni – Desemba, 2015 wananchi wapatao sita walishambuliwa na kuuawa na wanyamapori na Shirika la Hifadhi Tanzania (TANAPA) halikushiriki mazishi ya watu hawa, wala hakuna fidia yoyote waliyopata ndugu wa marehemu, hali inayoonesha mahusiano mabaya kati ya jamii na Mamlaka ya Hifadhi, zaidi ya hayo wanyama kama tembo, wamesababisha hasara kubwa sana kwa kuharibu mazao katika Tarafa ya Daudi, Kata za Marangwa, Daudi, Bargish na Gehandu. • Je, ni lini Serikali itawalipa fidia ndugu wa hao watu sita waliouawa na wanyama wakali katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu? • Je, ni lini Serikali kupitia TANAPA italipa fidia kwa wale wote walioharibiwa mazao shambani mwaka 2014/ 2015?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali ndogo la nyongeza.
Kwa kuwa hicho kinachoitwa kifuta jasho au kifuta machozi kwa mujibu wa Sheria ya Wanyamapori, imekuwa hailipwi kwa wakati pale ambapo wananchi wakipata uharibu wa mazao yao hasa katika maeneo ambayo yanapakana na hifadhi:-
Je, ni kwa nini Serikali sasa isifikirie kuanzisha mfuko wa fidia ambao utachangiwa na hizi mamlaka zote kama TANAPA, Ngorongoro ili wananchi wawe wanaweza kutapata fidia yao kwa wakati bila kucheleweshwa?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kuna changamoto kubwa sana kuhusiana na malipo ya vifuta jacho na vifuta machozi. Ukweli ambao ni wa kudumu, hakuna namna ambayo tunaweza tukalifanya zoezi hili kwa namna endelevu kwamba madai yote yanahusiana na vifuta jasho na vifuta machozi yakalipwa kwa kile kinachoitwa kwa wakati hata kama tukianzisha mfuko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili namna pekee ya kuweza kuliweka vizuri, namna bora zaidi ni kuzuia zaidi kuweka kinga na kupunguza matukio ambayo yanasabisha ulipaji wa vifuta jasho na vifuta machozi. Ndiyo maana pale awali wakati najibu swali la nyongeza nilisema wazo la kushirikisha jamii zinazozunguka maeneo ya hifadhi ni wazo la msingi zaidi. Ili kuweza kuona ni namna gani tunaweza kufanya uhifadhi kwa namna ambayo tunaweza kupunguza matokeo yanayolazimisha sasa Serikali ilipe vifuta jasho na vifuta machozi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima twende kwa utaratibu wa kuweka ushirikishi zaidi na kuanza kuangalia kwamba wananchi hawakai kwenye maeneo ambayo ni ya mapito ya wanyama hawakai kwenye maeneo ambayo ni ya mtawanyiko wa wanyama na kufanya shughuli za kilimo na ufugaji kwenye maeneo yale. Pale inapotokea kwamba wanyama wanahama kutoka kwenye maeneo yao, maeneo ambayo siyo yale ya mtawanyiko ya yale ya njia za mpito, basi tutakuwa tumepunguza kwa kiwango kikubwa matukio hayo, lakini pia tutaweka mbinu mbadala za kuweza kuzuia wanyama kuweza kuleta uharibifu kwenye mazao lakini pia kudhuru wananchi wanaozunguka maeneo hayo.

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Kati ya mwezi Juni – Desemba, 2015 wananchi wapatao sita walishambuliwa na kuuawa na wanyamapori na Shirika la Hifadhi Tanzania (TANAPA) halikushiriki mazishi ya watu hawa, wala hakuna fidia yoyote waliyopata ndugu wa marehemu, hali inayoonesha mahusiano mabaya kati ya jamii na Mamlaka ya Hifadhi, zaidi ya hayo wanyama kama tembo, wamesababisha hasara kubwa sana kwa kuharibu mazao katika Tarafa ya Daudi, Kata za Marangwa, Daudi, Bargish na Gehandu. • Je, ni lini Serikali itawalipa fidia ndugu wa hao watu sita waliouawa na wanyama wakali katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu? • Je, ni lini Serikali kupitia TANAPA italipa fidia kwa wale wote walioharibiwa mazao shambani mwaka 2014/ 2015?

Supplementary Question 3

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona. Pia katika Wilaya ya Karagwe kuna wahanga ambao wameathirika na wanyama waharibifu hasa tembo na viboko katika kata za Kihanga, Rugu, Nyakasimbi, Nyakabanga, Nyakakika na Bwelanyange, lakini pamoja na kushindwa kuwapa kifuta machozi wananchi hawa, pia vijiji katika hizi kata vinapakana na Pori la Akiba la Kimisi na Burigi na kuna asilimia ambayo inatakiwa kutoka kwenye mapato ya hifadhi kwenda kwenye vijiji ili kuwasaidia katika shughuli za maendeleo. Tumetuma madai katika Wizara kwa muda mrefu, lakini hatujawahi kupata hii fidia ili wananchi hawa nao wafaidike.
Je, ni lini Serikali itatoa kifuta machozi hicho pamoja na yale mapato? Ahsante.

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nilisema katika maombi ambayo yameifikia Wizara kwa ajili ya uhakiki, kiwango cha jumla ya fedha takribani shilingi milioni 500 pekee ndicho ambacho kimebaki bila kulipwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaenda kuangalia kwenye orodha ile ya wale ambao wanafanya jumla ya madai yawe shilingi milioni 500 nione kama wananchi wanaolizungumzia ni sehemu ya madai hayo. Kwa hiyo, ikiwa hivyo ndivyo, tumesema fedha hizi zinalipwa ndani ya mwaka wa fedha huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ikiwa siyo miongoni mwa wale ambao jumla ya fedha shilingi milioni 500 zinadaiwa, basi itakuwa wako katika mchakato; wale ambao bado taratibu hazijakamilika kwenye ngazi za Halmashauri na Mikoa, kwa hiyo, tutakwenda kuhimiza tu ifanyike haraka ili madai hayo yaweze kuifikia Wizara yawekwe kwenye orodha halafu tuweke utaratibu wa ratiba ya kuweza kuyalipa.