Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Kijiji cha Mtisi katika Kata ya Sitalike hakuna eneo la kilimo:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapa wananchi hao maeneo kwa ajili ya kilimo?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, wananchi wa Kijiji cha Mtisi wanapata shida sana, hawana kabisa eneo la kilimo. Nafikiri umeona kabisa hapa jinsi gani eneo la hifadhi ni kubwa zaidi kuliko eneo la kilimo na kaya zimeonekana hapa. Naishukuru Serikali imepanga kuwapa ardhi Novemba mwishoni lakini wananchi wa Mtisi wanahitaji kulima sasa, sasa hivi ndiyo kipindi cha maandalizi ya kilimo, wanatakiwa waandae mashamba yao. Je, Serikali haioni ni vema kubadilisha hii Novemba mwishoni wafanye Novemba hii mwanzoni ili wananchi wale waweze kupata maeneo ya kilimo waweze kupata chakula ndani ya familia zao? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, ndani ya Kata hii ya Sitalike kwenye Vijiji vya Matandalani na Igongwe kutokana na ardhi ndogo wako ndani ya ramani toka 1972, lakini Serikali ilienda kuwabomolea nyumba zao na mpaka leo hii imekuwa tafrani, wala hawaelewi hatma ya maisha yao. Je, Serikali ina mpango gani na wananchi wa Matandalani na Igongwe? Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kwenda kwenye Kata ya Sitalike kuona adha hii? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kurejea majibu yangu ya swali la msingi katika kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Anna Lupembe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jibu langu la msingi nimesema kwamba ifikapo mwishoni lakini hadi sasa kazi za kuwapatia ardhi wananchi hao zinaendelea. Hadi jana kaya 200 zilikuwa zimeshatambuliwa na zilikuwa zimeshatengewa eneo maalum. Kwa hiyo, bado zoezi hilo linaendelea ile mwishoni mwa Novemba ni kumalizia kazi, kazi itakuwa imekamilika. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge asiwe na wasiwasi wowote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili amesema kwamba wananchi wa Kijiji cha Matandalani na Igongwe walibomolewa nyumba ni kwa sababu walikuwa kwenye hifadhi. Natoa wito kwa wananchi ambao wako kwenye maeneo ya hifadhi kwamba wanatakiwa waondoke wenyewe badala ya kusubiri kuondolewa kwa nguvu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa shida hiyo iliyopo kule Matandalani na Igongwe na Halmashauri ya Nsimbo kwa ujumla, nilipita juzi lakini niko tayari kwenda tena kama matatizo yataendelea kuzidi kuwepo.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Kijiji cha Mtisi katika Kata ya Sitalike hakuna eneo la kilimo:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapa wananchi hao maeneo kwa ajili ya kilimo?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Mkoa wa Katavi ni kimbilio la wananchi wengi ambao wamekosa ardhi ya kilimo na wakati huohuo ardhi iliyopo Mkoa wa Katavi asilimia themanini imemilikiwa na misitu ya Serikali kiasi kwamba wananchi walio wengi wamekosa kupata nafasi ya kufanya shughuli zao za kiuchumi kupitia sekta ya kilimo hasa katika kata za Sibwesa, Kasekese, Katuma, Bulamata ambako kuna migogoro mingi ya ardhi. Je, Serikali imejipanga vipi kutatua kero ya ukosefu wa ardhi ili wananchi waweze kuitumia ipasavyo kujikwamua kiuchumi?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama alivyozungumza katika Mkoa wa Katavi sehemu kubwa ya ardhi ni misitu na maeneo ya hifadhi. Ni lengo la Serikali kuendeleza maeneo hayo katika msingi wa kuendeleza misitu na hifadhi kwa ajili ya ustawi wa mazingira lakini vilevile kwa ajili ya kuendeleza ile hali nzuri ya hewa ikiwemo mvua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni kwamba katika halmashauri na vijiji vyote tuendelee kuhakikisha kwamba kila kijiji kinakuwa na mpango ardhi wa eneo lake ambao unaainisha maeneo ya kulima, maeneo ya kuishi kama kijiji, maeneo ya mifugo na malisho ili kusudi tuwe na mipango endelevu ya maisha yetu. Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo ndilo jibu langu.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Kijiji cha Mtisi katika Kata ya Sitalike hakuna eneo la kilimo:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapa wananchi hao maeneo kwa ajili ya kilimo?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Wilaya ya Siha kwenye Kata Ngarenairobi na Ndumeti wananchi hawana maeneo ya kulima pamoja na makazi, wamekaa kwenye mabonde wakati wamezungukwa na heka zaidi ya elfu hamsini na sita za Serikali lakini kukiwepo na mashamba makubwa sana ya ushirika ndani ya Wilaya ya Siha ambayo hayatumiki kama inavyotakiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kumwomba Waziri kama atakuwa tayari kufuatana na mimi baada ya Bunge hili tukatizame mazingira ya Wilaya ya Siha na huko Ndumeti pamoja Ngarenairobi na maeneo mengine tuweze kuamua namna ya kupanga hiyo ardhi kubwa sana iliyoko Siha kwa matumizi ya wananchi kwa ajili ya kilimo, makazi lakini vilevile kutenga maeneo ya viwanda na uwekezaji mwingine kwa ajli ya Serikali na sera iliyopo? Ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo kubwa la Siha na maeneo kama hayo ni uwekezaji mkubwa ambao unafanywa na wananchi wachache. Kwa hiyo, tungependa tupate kwanza mpango wa Halmashauri yake halafu ndiyo tuweze kuufanyia kazi. Ahsante sana.