Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza:- Katika Mkoa wa Mtwara kuna tatizo kubwa la kukatika kwa umeme mara kwa mara jambo ambalo linaathiri wananchi ikiwemo wafanyabiashara ambao wanategemea sana umeme na hivyo kusababisha wakati mwingine biashara hizo kuharibika na kuwasababishia hasara wananchi hao. Je, ni lini Serikali itawahakikishia wananchi wa Mtwara kupata umeme wa uhakika?

Supplementary Question 1

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza, pamoja na kupita bomba la gesi katika maeneo mengi ya Mtwara na Lindi, bado vijiji na mitaa mingi haina mtandao wa umeme. Je, ni lini REA III itamaliza tatizo hili kwa mikoa ya kusini? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, mkandarasi aliyepewa kusambaza mtandao wa umeme Mtwara yupo slow sana. Je, Serikali inachukua uamuzi gani kwa mkandarasi huyo? (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge ameuliza; ni lini REA III itamaliza tatizo la kusambaza umeme katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mtwara. Nataka nimfahamishe Mheshimiwa Mbunge kuwa Mkandarasi wa Mkoa wa Mtwara ni JV Radi Service Limited na ameshalipwa asilimia kumi na yupo Mkoani Mtwara akiendelea na kazi ya upimaji wa njia ya umeme, na kwa kuwa Wizara tumetoa maelekezo kwamba vifaa vyote vya mradi huu REA III vipatikane ndani ya nchi, wakandarasi wanachoendelea nacho sasa ni namna ya kutafuta vifaa vyote na kuagiza ndani ya nchi, na nimhakikishie kazi hii itafanyika kwa mujibu wa ratiba iliyopangwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili anaulizia hatua gani zitachukuliwa dhidi ya mkandarasi huyu. Naomba nimwambie ratiba ya REA iko awamu mbili, awamu ya kwanza ni 2017 hii Julai mpaka 2019, kwa hiyo mkandarasi huyu yupo ndani ya muda. Na kwa kuwa amelipwa asilimia 10 na ameanza kazi, nimthibitishie tu zoezi la upelekaji umeme katika Mtwara kwa mkandarasi huyu JV Radi Service itakamilika kwa wakati.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza:- Katika Mkoa wa Mtwara kuna tatizo kubwa la kukatika kwa umeme mara kwa mara jambo ambalo linaathiri wananchi ikiwemo wafanyabiashara ambao wanategemea sana umeme na hivyo kusababisha wakati mwingine biashara hizo kuharibika na kuwasababishia hasara wananchi hao. Je, ni lini Serikali itawahakikishia wananchi wa Mtwara kupata umeme wa uhakika?

Supplementary Question 2

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali katika kutatua tatizo la umeme kwa Mikoa ya Lindi na Mtwara, baada ya mateso makubwa tuliyoyapata katika kipindi hiki cha miezi miwili/mitatu cha kukosa umeme kwa zaidi ya siku nne. Serikali inaambatanishaje juhudi hizo na ukarabati wa miundombinu hasa nguzo, kwenye yale maeneo ambayo nguzo zake ni mbovu. Kwa hiyo, hata wakikamilisha uzalishaji bado usambazaji wa umeme kwenye haya maeneo ambayo nguzo zake ni mbovu bado itakwama.
Sasa Serikali imejipangaje kuambatanisha juhudi hizo mnazoendelea nazo na ukarabati wa nguzo kwenye yale maeneo ambayo nguzo zimechoka?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Lakini niwape pole sana Waheshimiwa Wabunge wa Mikoa ya Mtwara na Lindi kwa kipindi ambacho Mheshimiwa Nape amezungumza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli zipo juhudi za makusudi ambazo sasa tunachukua kama Serikali, tuliporekebisha umeme katika Mkoa wa Mtwara tarehe 16 mwezi uliopita tuliacha feeder mbili ambazo matengenezo yake yanaendelea. Wananchi wa Mkoa wa Lindi kwa sasa wanapata umeme kutoka kwenye sub station ya Maumbika. Sasa sub station ya Maumbika marekebisho ya engine yake yanakamilika kesho. Kwa hiyo wananchi wa Mtwara, Lindi na maeneo mengine yategemee kupata umeme kuanzia kesho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la nguzo kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amezungumza, tumeagiza nguzo mpya kutoka hapa nchini, tumeacha sasa kuleta nguzo kutoka nje ambazo zilikuwa zinakaa kwa muda mrefu mipakani. Nguzo zitakuwa mpya, kwa hiyo, niwahakikishie wananchi watapata nguzo na ukarabati utaendelea vizuri. (Makofi)

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza:- Katika Mkoa wa Mtwara kuna tatizo kubwa la kukatika kwa umeme mara kwa mara jambo ambalo linaathiri wananchi ikiwemo wafanyabiashara ambao wanategemea sana umeme na hivyo kusababisha wakati mwingine biashara hizo kuharibika na kuwasababishia hasara wananchi hao. Je, ni lini Serikali itawahakikishia wananchi wa Mtwara kupata umeme wa uhakika?

Supplementary Question 3

MHE. AISHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Tatizo lililopo Mtwara halina tofauti na tatizo lililopo katika Jimbo la Singida Kaskazini. Vijiji vingi vya Jimbo la Singida Kaskazini ambavyo vilikuwa katika Mpango wa REA II mpaka sasa havijapatiwa umeme. Vijiji hivyo ni Mrama, Madasenga, Mipilo, Meria, Mitula na Msange. Kwa kuwa sasa tunaelekea kwenye Tanzania ya Viwanda; je, ni lini sasa Serikali itavipatia vijiji hivyo umeme ukizugatia kwamba tupo katika Mpango wa REA III? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Mkoa wa Singida mkandarasi ambaye alipewa kazi alikuwa na jukumu la kukamilisha masuala ya mikataba. Taratibu za mikataba amekamilisha juzi, siku ya Ijumaa, na hivyo ataanza kuingia site kuanzia Ijumaa wiki hii, kwa hiyo wananchi wa Singida na maeneo mengine watapata mkandarasi huyo.
Lakini cha pili Singida tunawapatia mkandarasi aliyeshindwa kukamilisha kazi katika REA II, Kampuni ya SPENCON iliondolewa kwa hiyo, tunawapa mkandarasi mwingine. Kwa hiyo, Mkoa wa Singida utapata wakandarasi wawili pamoja na mkandarasi wa REA III.

Name

Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza:- Katika Mkoa wa Mtwara kuna tatizo kubwa la kukatika kwa umeme mara kwa mara jambo ambalo linaathiri wananchi ikiwemo wafanyabiashara ambao wanategemea sana umeme na hivyo kusababisha wakati mwingine biashara hizo kuharibika na kuwasababishia hasara wananchi hao. Je, ni lini Serikali itawahakikishia wananchi wa Mtwara kupata umeme wa uhakika?

Supplementary Question 4

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa
Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi.
Kwa kuwa chanzo cha umeme pale Somanga Fungu kinashindwa kufanya kazi vizuri na kupelekea matatizo makubwa ya umeme kwa Wilaya ya Kilwa na Rufiji kwa sababu ya mitambo ile kuchelewa kufanyiwa ukarabati na kwa kuwa sasa tatizo hilo linaendea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itatuunganisha watu wa Kusini na Gridi ya Taifa kwasababu sasa umeme imeshafika pale Kilwa? (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge Ngombale kwamba mitambo ya Somanga Fungu inatarajia kufanyiwa ukarabati hivi karibuni na kampuni ya RENCO ya Italy. Na Serikali kupitia TANESCO wameshasaini mkataba na ukarabati huo utakamilika Desemba, 2018 ambapo mitambo itakuwa na uwezo wa kuzalisha megawati 7.5 na matumizi ya Kilwa ni megawati tatu. Kwa hiyo naomba nimtaharifu kwamba hilo linafanyiwa kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ameuliza ni liniā€¦